top of page

Darsa 
na Mihadhara Online

Mosque

ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ

Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Durusu na Mazingatio kutokana na Suratul Hujuraati دروس وعبر من سورة الحجرات 🔴 LIVE | Ust Kassa
02:06:38

Durusu na Mazingatio kutokana na Suratul Hujuraati دروس وعبر من سورة الحجرات 🔴 LIVE | Ust Kassa

Darsa ilifanyika Shawwal 22, 1446 H Jumapili April 20, 2025 دروس وعبر من سورة الحجرات Durusu na Mazingatio kutokana na Suratul Hujuraati Umuhimu wa Suratul-Hujuraat Suratil Hujuraat ni muhimu sana kwa sababu ya kanuni na maadili ya jumla ya Kiislamu, miongozo, na adabu za kimaadili iliyomo katika kiwango cha nafsi na jamii. Sura imemeweka mipaka ya mahusiano, imehifadhi haki za kila mwanadamu, na kuunda katiba kamili katika elimu, maadili na sheria. Kupitia kwayo, inajenga jamii iliyo bora, yenye uaminifu inayofurahia tabia njema na ladha nzuri, pamoja na kufurahia hekima na busara na kutobebwa na uvumi na maneno bila ya kuthibitisha na kubainisha ukweli. Huu ndio wasiwasi wa umma wa Kiislamu unaohifadhi haki za Allah na haki za waja Wake. Suratul-Hujuraat ina durusu -mafunzo- na mazingatioa -maadili- mengi: 1. Wajibu wa kutanguliza Amri ya Allah na ya Rasuli Wake; kwa kushikamana na Kitabu cha Allah na Sunnah za Rasuli Wake, na kwamba yana maamuzi na yenye kutawala katika maisha ya Muislamu, na yanatanguliza juu ya mila, desturi, na kadhalika. 2. Kuwafunza Waislamu baadhi ya maadili na adabu wanazopaswa kuwa nazo mbele ya Rasuli wa Allah katika jinsi ya kuamiliana naye, kuzungumza naye, na hata kumwita, ili kuitukuza hadhi yake ya utukufu na kuheshimu nafasi yake, kwani yeye si kama watu wa kawaida. 3. Kuadhimisha ibada ya kuleta suluhu -maupatanisho- baina ya Waislamu, kwa kutafuta njia munasaba za kuwapatanisha wale wanaohitilafiana, kwa kuzingatia dhana ya udugu unaowaunganisha. 4. Sura inabainisha maadili yanayotakiwa kujipamba nayo jamii ya Kiislamu, ambamo usalama na utu wa watu hauvunjwa kwa njia yoyote ile. 5. Surah inaonya dhidi ya dhihaka, masengenyo, kashfa, na kupachikana majina. 6. Surah inakataza kusengenya, kufanyiana ujasusi na kuwadhaniana. 7. Surah inaweka wazi kwamba Allah Aliumba viumbe kutokana na mwanamume na mwanamke, na akawagawanya katika mataifa na makabila kwa madhumuni ya kuishi pamoja na kuelewana, na si kwa ajili ya kubaguana na kujifakhari, iwe kwa ​​nasaba au nchi. 8. Surah inabainisha kwamba kiwango cha ubora mbele ya Muumba ni uchamungu na si kitu kingine chochote kile.
Nini baada ya Ramadhani ماذا بعد رمضان؟ 🔴 LIVE DARSA  Ust. Hassan A Hakeem Saeed
02:12:28

Nini baada ya Ramadhani ماذا بعد رمضان؟ 🔴 LIVE DARSA Ust. Hassan A Hakeem Saeed

Darsa ilifanyika Shawwal 15, 1446 H Jumapili April 13, 2025 ماذا بعد رمضان؟ Nini baada ya Ramadhani? Tumeuaga mwezi wa Ramadhano, tumeuaga mwezi wa Qur-aani, mwezi wa takwa, mwezi wa jihad, mwezi wa maghufira, mwezi wa dua, mwezi wa kutolewa watu Motoni. Kila Muislamu aliyeingia katika mwezi wa Ramadhani atakuwa ameingia na ametoka katika madrasa ya takwa. Na mtu anapoingia katika madrasa yoyote ile, hutoka humo akiwa ametunukiwa shahada ya lile somo alilolisoma, na baada ya hapo huitumia ile elimu aliyoisoma kumsaidia katika kuendesha maisha yake ya kila siku. Hivyo basi ni vyema kwa Muislamu ni vyema aendelee na kushikamana na yale aliyoyapata kwenye Ramadhani hadi atakapokutana na Rabi wake. Allah Anasema: وَاعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّى يَأْتِيَكَ الْيَقِينُ "Na muabudu Rabi wako mpaka ikufikie yakini (mauti)" Al Hijr : 99. Kinachotakikana kwa Muislamu ni istiqaamah (kuendelea kuwa thabiti/imara) فَاسْتَقِيمُوا إِلَيْهِ وَاسْتَغْفِرُوهُ "Basi thibitikeni imara Kwake, na muombeni maghufira" Fusswilat: 6. : أبي عَمْرَةَ، سُفْيَانَ بْنِ عَبْدِ اللهِ الثّقَفيِّ رَضيَ اللهُ عَنْهُ قَال: قُلْتُ: يا رَسُولَ الله، قُلْ لي في الإِسْلاَمِ قَوْلاً، لاَ أَسْأَلُ عَنْهُ أَحَداً غَيْرَكَ. قَال: ((قُلْ: آمَنْتُ باللهِ ثُمَّ اسْتَقِمْ)). Kutokana na Abu Amr, vile vile (anajulikana kama) Abu Amrah Sufyan bin Abdillah (Allah Awe Radhi Nae) amesema: Nilisema: Ewe Rasuli wa Allah! Niambie neno katika Uislamu ambalo sitoweza kumuuliza mmoja yeyote yule ghari yako wewe. Rasuli wa Allah akasema:"Sema; Namemuamini Allah, kisha kuwa na istiqamah (mwenye kunyooka; kwa kuendelea kushikamana na ibaada na kuwa na msimamo madhubuti)"Muslim. Kuhakikisha kuwa umewafikishwa kuweza kufikia kuwa na istiqamah, ni vyema jiulize maswali yafuatayo: 1. Je, unaendelea kufunga (kuna Saumu nyingi tu za Sunnah)? 2. Je, unaendekea na kisimamo cha usiku (Qiyamul-Layl)? 3. Je, unaendelea na usomaji na usikilizaji wa Qur-aani? 4. Je, unaendelea na uombaji wa dua? 5. Je, unaendelea na kububujikwa na machozi kwa kukumbuka dhambi zako na kuihofu adhabu ya Allah? Ni vyema ieleweke kwamba Allah Anapenda amali zinazoendeleza japokuwa ni chache kuliko amali nyingi zisizokuwa zenye kuendelezwe: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((أَحَبَّ الْأَعْمَالِ إِلَى اللَّهِ أَدْوَمُهَا وَإِنْ قَلَّ)) متفق ع Rasuli wa Allah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: "Amali zinazopendaza zaidi kwa Allah ni zile zinazodumishwa japokuwa ni kalilii". Wamewafikiana Bukhari na Muslim. (Ee Allaah! Ee Muelekezaji wa nyoyo, Elekeza nyoyo zetu katika utii Wako
Contact
bottom of page