top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
59:04
Darsa: سنن أبي داود 🔴LIVE | (I) كتاب الطهارة :حديث: كانَ إذا ذَهَبَ المذهَبَ أبعدَ Abu Raifah
Darsa ilfanyika Jumadath Thaniyah 24, 1447H Jumatatu Disemba 15, 2025 Sunan Abu Daud سنن أبي داود Mlango wa Kujiweka mbali (kujitenga) wakati wa kwenda kujisaidia باب التَّخَلِّي عِنْدَ قَضَاءِ الْحَاجَةِ حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ مَسْلَمَةَ بْنِ قَعْنَبٍ الْقَعْنَبِيُّ، حَدَّثَنَا عَبْدُ الْعَزِيزِ، - يَعْنِي ابْنَ مُحَمَّدٍ - عَنْ مُحَمَّدٍ، - يَعْنِي ابْنَ عَمْرٍو - عَنْ أَبِي سَلَمَةَ عَنِ الْمُغِيرَةِ بْنِ شُعْبَةَ، أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا ذَهَبَ الْمَذْهَبَ أَبْعَدَ . Ametusimulia Abdullah bin Maslamah bin Qa'nabi Al Qa'nabiyu, ametuhadithia Abdulazizi -yaani: Ibn Muhammad- kutokana na Muhammad -yaani: Ibn Amru- kutokana na Abu Salamah kutokana na Al Mughirah bin Shu’bah (Allah Awe Radhi Nae) kwamba: 'Nabii صلى الله عليه وسلم alikuwa anapotaka kwenda haja, huenda mbali (kujisaidia).'
Play Video
Play Video
01:04:04
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴 LIVE (VII) باب الرجاء Sh Salima
Darsa ilfanyika Jumadath Thaniyah 24, 1447H Jumatatu Disemba 15, 2025 باب الرجاء Mlango wa Kuwa na Matumaini :قَالَ الله تَعَالَى ﴾قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ لَا تَقْنَطُوا مِن رَّحْمَةِ اللَّـهِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعًا ۚ إِنَّهُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ﴿٥٣ "Sema: Enyi waja Wangu ambao wamepindukia mipaka juu ya nafsi zao: Msikate tamaa na rehmah ya Allah; hakika Allah Anaghufuria dhambi zote; hakika Yeye Ndiye Ghafuru Rahimu". Az-Zumar:53. ﴾وَهَلْ نُجَازِي إِلَّا الْكَفُورَ ﴿١٧ "Na Hatuadhibu isipokuwa anayekufuru." Sabaa:17. ﴾إِنَّا قَدْ أُوحِيَ إِلَيْنَا أَنَّ الْعَذَابَ عَلَىٰ مَن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ ﴿٤٨ "Hakika tumefunuliwa Wahyi ya kwamba adhabu itakuwa kwa yule atakayekadhibisha na akakengeuka." Twahaa:48. ﴾وَرَحْمَتِي وَسِعَتْ كُلَّ شَيْءٍ ۚ ﴿١٥٦ "Na Rehma Yangu imekienea kila kitu." At-A'raaf:106.
Play Video
Play Video
43:06
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير🔴LIVE Aayah 113 -114 Ust Abu Raifah
Darsa ilfanyika Jumadath Thaniyah 24, 1447H Jumatatu Disemba 15, 2025 Tafsiri ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة تَنَازُعُ اليَّهُودِ وِالنَّصَارى فِيْما بَيْنَهُم كُفْراً وَعِنَاداً Mayahudi na Nasara wanazozana wao kwa wao kwa ukafiri na ukaidi. وَقَالَتِ الْيَهُودُ لَيْسَتِ النَّصَارَىٰ عَلَىٰ شَيْءٍ وَقَالَتِ النَّصَارَىٰ لَيْسَتِ الْيَهُودُ عَلَىٰ شَيْءٍ وَهُمْ يَتْلُونَ الْكِتَابَ ﴾كَذَٰلِكَ قَالَ الَّذِينَ لَا يَعْلَمُونَ مِثْلَ قَوْلِهِمْ ۚ فَاللَّـهُ يَحْكُمُ بَيْنَهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ فِيمَا كَانُوا فِيهِ يَخْتَلِفُونَ ﴿١١٣ "Na Mayahudi wakasema kuwa: Nasara hawana lao jambo; na Nasara (pia) wakasema kuwa: Mayahudi hawana lao jambo; na hali wao (wote) wanasoma Kitabu (Taurat na Injili); hivyohivyo ndivyo walivyosema wale wasiojua mfano wa kauli yao (hii); basi Allah Atawahukumu baina yao Siku ya Qiyaamah katika yale waliyokuwa wakihitilafiana." ظُلْمُ مَنْ مَنَعَ عَنْ المَسَاجِدِ وَسَعَى فِي خَرَابِهَا Dhulma ya wale wanaowazuia watu kwenda Masjidini na kujitahidi kuiangamiza. وَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّن مَّنَعَ مَسَاجِدَ اللَّـهِ أَن يُذْكَرَ فِيهَا اسْمُهُ وَسَعَىٰ فِي خَرَابِهَا ﴾أُولَـٰئِكَ مَا كَانَ لَهُمْ أَن يَدْخُلُوهَا إِلَّا خَائِفِينَ ۚ لَهُمْ فِي الدُّنْيَا خِزْيٌ وَلَهُمْ فِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴿١١٤ "Na ni nani aliye dhalimu zaidi kuliko yule anayezuia Masajidi ya Allah kutajwa ndani yake Jina Lake na akajitahidi katika kuiharibu? Hao haitawafaa kuingia humo isipokuwa wakiwa ni wenye hofu; watapata duniani hizaya na Akhera watapata adhabu kuu kabisa."
Play Video
Play Video
01:10:56
Darsa: صحيح مسلم 🔴LIVE| DARSA (I) فأخبرني عن الإيمان : الإيمان بالله تعالى هو أصل الإيمان
Darsa ilfanyika Jumadath Thaniyah 23, 1447H Jumapili Disemba 14, 2025 Kumuamini Allah Ta'aala ndio msingi wa Imani الإيمان بالله تعالى هو أصل الإيمان
Play Video
Play Video
02:08:28
Darsa: Ujenzi wa familia na Jamii Imara 🔴 LIVE: Marudio (I) مراجعة الدروس السابقة
Darsa ilfanyika Jumadath Thaniyah 23, 1447H Jumapili Disemba 14, 2025 Darsa la Marudio: Kumbusho na Mapitio ya Mada Kumi Zilizofundishwa - Mental Health (Kulinda Afya ni Ibadah) by Ahmad - Children Mental Health (Khadija) - Domestic Violence/Abuse (Khadija) - Effects of Domestic Abuse (Salma) - Trauma (Khadija) - Effects of Trauma (Khadija) - Mambo yanayo Athiri Tabia za Watoto (Salma) - Positive Parenting (Salma) - Ruqyah: Hukmu ya Kutumia Majini (Ahmad) - Kinga Dhidi ya Sheytan (Hassan)
Play Video
Play Video
01:30:44
Darsa: الإيمان بعذاب القبر 🔴LIVE | (I) مراجعة الدروس السابقة Ust Abu Raifah
Darsa ilfanyika Jumadath Thaniyah 23, 1447H Jumapili Disemba 14, 2025 الإيمان بعذاب القبر Kuamini Adhabu ya Kaburi والإيمان بعذاب القبر وأن هذه الأمة تفتن في قبورها ، وتسأل عن الإيمان والإسلام ، ومن ربه ؟ ومن نبيه ؟ ويأتيه منكر ونكير ، كيف شاء الله ، وكيف أراد ، والإيمان به والتصديق به Na miongoni mwa usuli –misingi- ya Sunnah (Itikadi) inatakikana kuamini (kuwepo kwa) adhabu ya kaburi na kwamba umma huu utafitinishwa -utapewa mtihani- kwenye makaburi yao, wataulizwa juu ya: Imani na Uislamu, na nani Mola wake, na nani Nabii wake? Atajiwa na Munkar na Nakir, vile Atakavo Allah Atakapo, na (inatakikana) kuamini kwayo na kusadikishwa. Masuala (wingi na neno suala: yaani jambo linalojadiliwa) muhimu yanayotakiwa kuzingatiwa katika kipengele hichi ni : Suala la Kwanza: Kuamini kuwepo kwa adhabu ya kaburini kama ilivyothibiti Suala la Pili: Hili ni miongoni mwa mambo ya ghaibu: Muumini huamini mambo ya ghaibu yote ambayo Qur-aani imeyajumuisha na kuyataja, (na pia) yale yote ambayo Sunnah za Nabii Muhammad ﷺ zimeyajumuisha na kuyataja Suala la Tatu: Kwamba ummah huu utafitinishwa kwenye makaburi yao Suala la Nne: Maswali atayoulizwa mja kaburini Suala la Tano: Waulizaji ni Malaika kama ilivyokuja kwenye Athar Suala la Sita: Kuhusiana na vipi Malaika wataweza kuingia kaburini hilo ni suala la ghaibu na ndio likawa miongoni mwa Usuli Sunnah (itikadi) hivyo basi kinachotakiwa ni kuliamini kama lilivyothibiti na kupokelewa. Suala la Saba: Dalila za hilo kutokana na Qur aani Suala la Nane: Dalili za hilo kutokana na Sunnah Suala la Tisa: Muumini hutarajiwa kuwa atajiandaa na kumuomba Allah Amkinge na adhabu ya kaburini kila anapoleta Tahiyyatu na kila anapozuru makaburi na kadhalika. Suala la Kumi: Kuna makundi ya dhalala (vichwa vya bidaa) yanalikana suala hili zima la adhabu ya kaburi kwa hawaa na kutanguliza kwa akili mbele ya Nususi. Suala la Kumi na Moja: Kuacha kulumbana kuhusiana na suala hili kwa kuwa ni suala la ghaibu. Suala la Kumi na Mbili: Kitakachoneemeshwa au adhibiwa ni Roho ya mja SHARHU Imamu Ahmad (Rahimahullahu) amesema kuwa: (Na miongoni mwa usuli –misingi- ya Sunnah inatakikana) kuamini (kuwepo kwa) adhabu ya kaburiوالإيمان بعذاب القبر, (kuhusiana na) haya (yaani: adhabu ya kaburi) kumepokelewa Hadithi nyingi, na katika miongoni mwa Aayaat (zenye kuhusiana na adhabu ya kaburi) ni Kauli Yake Ta'alaa: ﴾النَّارُ يُعْرَضُونَ عَلَيْهَا غُدُوًّا وَعَشِيًّا ۖ وَيَوْمَ تَقُومُ السَّاعَةُ أَدْخِلُوا آلَ فِرْعَوْنَ أَشَدَّ الْعَذَابِ﴿٤٦ “Wanadhihirishiwa Moto (kwenye makaburi yao) asubuhi na jioni; na siku itakayosimama Saa [kutasemwa]: Waingizeni watu wa Firauna (katika) adhabu kali kabisa.” Basi Firauni na kaumu yake na kadhalika makafiri wengine (wote) wanadhihirishiwa (adhabu ya) Moto asubuhi na jioni; hii ni adhabu ya Barzakh , kisha akaegemezea adhabu ya siku ya Qiyaamah: ﴾وَيَوْمَ تَقُومُ السَّاعَةُ أَدْخِلُوا آلَ فِرْعَوْنَ أَشَدَّ الْعَذَابِ﴿٤٦ “Na siku itakayosimama Saa [kutasemwa]: Waingizeni watu wa Firauna (katika) adhabu kali kabisa.” , na Aayaat nyenginezo nyingi zinazoashiria jambo hili (la adhabu ya kaburini). Na kuhusiana na adhabu ya kaburi, imamu Bukhari na imamu Muslim (Rahimahumullahu) wamepokea kwenye sahihi zao mbili: عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ ـ رضى الله عنهما ـ قَالَ مَرَّ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم بِقَبْرَيْنِ فَقَالَ " إِنَّهُمَا لَيُعَذَّبَانِ، وَمَا يُعَذَّبَانِ فِي كَبِيرٍ أَمَّا أَحَدُهُمَا فَكَانَ لاَ يَسْتَتِرُ مِنَ الْبَوْلِ، وَأَمَّا الآخَرُ فَكَانَ يَمْشِي بِالنَّمِيمَةِ ". ثُمَّ أَخَذَ جَرِيدَةً رَطْبَةً، فَشَقَّهَا نِصْفَيْنِ، فَغَرَزَ فِي كُلِّ قَبْرٍ وَاحِدَةً. قَالُوا يَا رَسُولَ اللَّهِ، لِمَ فَعَلْتَ هَذَا قَالَ " لَعَلَّهُ يُخَفَّفُ عَنْهُمَا مَا لَمْ يَيْبَسَا ". Kutokana na Ibn Abbas (Allah Awe Radhi Nao) amesema kuwa: Nabiiﷺ aliyapitia makaburi mawili, basi akasema: “Hakika wawili hawa wanaadhibiwa, na hawaadhibiwi kwa jambo kubwa (la kuwashinda kulitekeleza na kujiepusha nalo, ama mmoja wao alikuwa hajikingi -hajilindi- na (cheche za) mkojo, na ambapo mwengine alikuwa akienda kufitinisha -kugombanisha watu-.” Kisha Nabiiﷺ akachukua jani bichi la mtende, akalipasua sehemu –pande- mbili, na kila kipande alikiweka –alikiatika- kwenye kila kaburi. (Swahaba Allah Awe Radhi Nao Jamia) wakauliza kwa kusema: Ewe Rasuli wa Allahﷺ! Kwanini umefanya hivi? Rasuli wa Allahﷺ akawajibu kwa kusema: “Nataraji –natumai- kwamba (adhabu) itahafifishwa kwao madama (vipande vya majani) havijakuwa yabisi.”
Play Video
Play Video
53:47
Darsa: صحيح البخاري 🔴 LIVE | (II) حديث: إنّمَا الأَعْمَالُ بالنِّيّاتِ Ust Abu Raifah
Darsa ilfanyika Jumadath Thaniyah 22, 1447H Ijumaa Disemba 13, 2025 Hadithi ya Kwanza: إنّمَا الأَعْمَالُ بالنِّيّاتِ، وَإِنَّمَا لِكُلِّ امرِئٍ مَا نَوَى، فَمَنْ كَانَتْ هجرته إلى الله ورسوله، فهجرته إلى الله ورسوله ومن كانت هِجْرَتُهُ لِدُنْيَا يُصيبُهَا، أَوْ امْرَأَةٍ يَنْكَحُهَا، فَهِجْرَتُهُ إِلى مَا هَاجَرَ إِلَيْه “Hakika kusihi kwa amali huzingatiwa na nia; na hakika kila mtu atalipwa kwa kile alichokinuia, hivyo basi yule ambaye hijrah yake ilikuwa kwa ajili ya Allah na Rasuli Wake, basi hijrah yake itakuwa kwa ajili ya Allah na Rasuli Wake; na yule ambaye hijrah yake ni kwa ajili ya kuiendea dunia ili aihodhi, au kumuendea mwanamke ili amuoe; basi hijrah yake itakuwa kwa aliloliendea.” Hadithi hii ni adhimu kwa kuwa ni msingi katika misingi ya Uislamu na ni usuli/asili na asasi katika misingi ya Sharia hata ikafikia kusemwa kuwa ni: Theluthi ya Elimu Hadithi imekusanya masuala adhimu ya Dini yakiwemo: Suala la Kwanza: Ukweli (uhakika) wa Nia المسألة الأولى: حقيقة النية Suala la Pili: Umuhimu wa Nia المسألة الثانية: أهمية النية Kauli za Salaf katika kuadhimisha hadhi (nafasi) ya Nia أقوال السلف في تعظيم قدر النية Suala la Tatu: Kusudio la Nia katika maneno ya wanazuoni المسألة الثالثة: المقصود بالنية في كلام العلماء Suala la Nne: Je,Nnia ni nguzo au sharti katika ibada? المسألة الرابعة: هل النية ركن أو شرط في العبادات؟ Suala la Tano: Shuruti za Nia المسألة الخامسة: شروط النية
Play Video
Play Video
52:02
DARSA: مَوْسُوعَة عُلُومِ الحَدِيْثِ وفُنُونِه 🔴 LIVE| (II) آدَابٌ المُحَدِّث
Darsa ilfanyika Jumadath Thaniyah 21, 1447H Ijumaa Disemba 12, 2025 SEHEMU YA PILI Adabu za Muhaddith (Mwenye kusimulia Hadithi) آدَابٌ المُحَدِّث 1. Nia safi (yaani: kuwa na Ikhlasi) katika kusimulia Hadithi إِخْلاَصُ النِّيَّةِ فِي رِوَايَةِ الحَدِيثِ 2. Kujipamba kwa akh-laq nzuri التَّحَلِّي بِمَكَاِرمِ الأَخْلاَقِ 3. Kutosimulia Hadithi kabla ya kuwa tayari (yaani: kabla ya kuhitimu) عَدَمُ التَّصَدِّي للِتَّحْدِيثِ قَبْلَ التَّأَهُّلِ لِذَلِكَ 4. Kile anachokihitajia Muhaddithi ما يَفْتَقِرُ إِلَيْهِ المُحَدِّثُ 5. Kujizuia kusimulia patapokuwa kuna hofu ya kuchanganyikiwa الإِمْسَاكُ عَنِ التَّحْدِيْثِ عِنْدَ خَوْفِ الاِخْتِلاَطِ 6. Kuwaheshimu wale wanaostahiki zaidi kuliko yeye na kuwaelekeza. تَوْقِير مَن هُوَ أَوْلَى مِنْهُ والدَْلاَلَةُ عَلَيْهِ 7. Kuheshimu majilisi na Hadithi تَوْقِيرمَجَالِسِ الحَدِيثِ
Contact
bottom of page