Darsa ya Hadithi za Riyadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴 LIVE (IV) باب الأمر بالمعروف والنهي عن المنكر
Darsa ilifanyika Dhul Hijjah 28, 1446 H Jumanne Juni 24, 2025
باب الأمر بالمعروف والنهي عن المنكر
Mlango wa Kuamrisha Mema na Kukataza Munkari (maovu)
قَالَ اللهُ تَعَالَى
وَلْتَكُن مِّنكُمْ أُمَّةٌ يَدْعُونَ إِلَى الْخَيْرِ وَيَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ ۚ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفلِحُونَ ﴿١٠٤
"Na watokeze kutoka kwenu umati wa watu wataolingania kwenye heri na wataoamrisha mema na wataokataza munkari; na hao ndio waliofaulu." Aal-Imraan 3:104.
كُنتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ تَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَتَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ
"Mmekuwa Ummah bora kabisa uliotolewa (mfano) kwa watu; mnaamrisha mema na mnakataza munkari…" Aal-Imraan 3:110.
خُذِ الْعَفْوَ وَأْمُرْ بِالْعُرْفِ وَأَعْرِضْ عَنِ الْجَاهِلِينَ ﴿١٩٩
"Shikamana na usamehevu, na amrisha mema na jiepushe na majahili." Al-A’raaf: 199.
وَالْمُؤْمِنُونَ وَالْمُؤْمِنَاتُ بَعْضُهُمْ أَوْلِيَاءُ بَعْضٍ ۚ يَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ
"Na Waumini wanaume na Waumini wanawake ni marafiki wandani wao kwa wao; wanaamrisha mema na wanakataza munkari…" At-Tawbah: 71.
لُعِنَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن بَنِي إِسْرَائِيلَ عَلَىٰ لِسَانِ دَاوُودَ وَعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ ۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَوا وَّكَانُوا يَعْتَدُونَ ﴿٧٨
"Wamelaaniwa wale waliokufuru miongoni mwa wana wa Israil kwa lisani ya (Nabii) Daud na Isa mwana wa Maryam; hivyo ni kwa sababu ya kuasi kwao na walikuwa wakipindukia mipaka."Al Maaidah 5:77.
كَانُوا لَا يَتَنَاهَوْنَ عَن مُّنكَرٍ فَعَلُوهُ ۚ لَبِئْسَ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ ﴿ ٧٩
"Walikuwa hawakatazani munkari waliyofanya; uovu ulioje waliyokuwa wakiyafanya." Al- Maaidah 5: 79.
وَقُلِ الْحَقُّ مِن رَّبِّكُمْ ۖ فَمَن شَاءَ فَلْيُؤْمِن وَمَن شَاءَ فَلْيَكْفُرْ ۚ
"Na sema: “(Hii ni) Haki kutoka kwa Rabi wenu; basi anayetaka aamini, na anayetaka akufuru.” Al-Kahf: 29.
فَاصْدَعْ بِمَا تُؤْمَرُ وَأَعْرِضْ عَنِ الْمُشْرِكِينَ﴿٩٤
"Basi tangaza wazi yale uliyoamrishwa na jitenge na washirikina." Al-Hijr: 94.
فَلَمَّا نَسُوا مَا ذُكِّرُوا بِهِ أَنجَيْنَا الَّذِينَ يَنْهَوْنَ عَنِ السُّوءِ وَأَخَذْنَا الَّذِينَ ظَلَمُوا بِعَذَابٍ بَئِيسٍ بِمَا كَانُوا يَفْسُقُونَ ﴿١٦٥
"Waliposahau yale waliyokumbushwa nayo; Tuliwaokoa wale wanaokataza uovu, na Tukawachukua wale waliodhulumu kwa adhabu mbaya kabisa kwa yale waliyokuwa wakifanya ufasiki." Al-A’raaf: 165.