top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
01:05:42
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات🔴LIVE (I) باب فضل ضعفة المسلمين والفقراء والخاملين
Darsa ilifanyika Swafar 25, 1447H Jumanne Agosti 19, 2025 باب فضل ضعفة المسلمين والفقراء والخاملين Mlango wa Fadhila za Waislamu Wanyonge, na Mafakiri na Wasiojulikana قَالَ الله تَعَالَى وَاصْبِرْ نَفْسَكَ مَعَ الَّذِينَ يَدْعُونَ رَبَّهُم بِالْغَدَاةِ وَالْعَشِيِّ يُرِيدُونَ وَجْهَهُ ۖ وَلَا تَعْدُ عَيْنَاكَ عَنْهُمْ تُرِيدُ زِينَةَ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ۖ وَلَا تُطِعْ مَنْ أَغْفَلْنَا قَلْبَهُ عَن ذِكْرِنَا وَاتَّبَعَ هَوَاهُ وَكَانَ أَمْرُهُ فُرُطًا ﴿٢٨ " Na isubirishe nafsi yako pamoja na wale wanaomuomba Rabi wao asubuhi kabla jua kucha na jioni, wanataka Wajihi Wake; na wala macho yako yasiwavuke kwa kutaka pambo la uhai wa dunia; na wala usimtii Tuliyemghafilisha moyo wake na Ukumbusho Wetu akafuata hawaa zake, na jambo lake limekuwa la kuzidi kuvuka mipaka." Al-Kahf: 28.
Play Video
Play Video
01:06:13
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات🔴LIVE (II) باب الإصلاح بَيْنَ الناس
Darsa ilifanyika Swafar 24, 1447H Jumatatu Agosti 18, 2025 باب الإصلاح بَيْنَ الناس Mlango wa Kusuluhisha Baini ya Watu :قَالَ الله تَعَالَى وَإِنِ امْرَأَةٌ خَافَتْ مِن بَعْلِهَا نُشُوزًا أَوْ إِعْرَاضًا فَلَا جُنَاحَ عَلَيْهِمَا أَن يُصْلِحَا بَيْنَهُمَا صُلْحًا ۚ وَالصُّلْحُ خَيْرٌ ۗ ﴿١٢٨ "Na ikiwa mke atahofia kutoka kwa mumewe uonevu wa ndoa au kutengwa, basi si vibaya juu yake wakisikilizana baina yao kwa suluhu; na suluhu ni bora.." An-Nisaa 4:128. لَّا خَيْرَ فِي كَثِيرٍ مِّن نَّجْوَاهُمْ إِلَّا مَنْ أَمَرَ بِصَدَقَةٍ أَوْ مَعْرُوفٍ أَوْ إِصْلَاحٍ بَيْنَ النَّاسِ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ ابْتِغَاءَ مَرْضَاتِ اللَّـهِ فَسَوْفَ نُؤْتِيهِ أَجْرًا عَظِيمًا ﴿١١٤ "Hakuna heri katika minong’ono yao mingi isipokuwa anayeamrisha Sadaka, au maarufu (mema), au kusuluhisha baina ya watu; na atakayefanya hivyo (kwa gharadhi ya) kutaka Radhi za Allah, basi Tutampa ujira adhimu." An-Nisaa 4:114. يَسْأَلُونَكَ عَنِ الْأَنفَالِ ۖ قُلِ الْأَنفَالُ لِلَّـهِ وَالرَّسُولِ ۖ فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَصْلِحُوا ذَاتَ بَيْنِكُمْ ۖ وَأَطِيعُوا اللَّـهَ وَرَسُولَهُ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ﴿١ "Wanakuuliza (ewe Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusiana na ghanima/ngawira; sema: Ngawira ni ya Allah na Rasuli, basi mcheni Allah na tengenezeni yaliyo baina yenu; na mtiini Allah na Rasuli Wake mkiwa ni Waumini." Al-Anfaal:1. إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ فَأَصْلِحُوا بَيْنَ أَخَوَيْكُمْ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ﴿١٠ "Hakika Waumini ni ndugu, basi suluhisheni baina ya ndugu zenu; na mcheni Allah ili mpate kurehemewa." Al-Hujuraat:10.
Play Video
Play Video
04:31:14
Mhadhara: Kuishi na Tawhidi Ughaibuni 🔴LIVE التوحيد ونواقضه
Mhadhara ulifanyika Swafar 23, 1447H Jumapili Agosti 17, 2025 التوحيد ونواقضه Maana ya Tawhidi ما هو التوحيد؟ Vitenguzi vya Tawhidi ما هي ونواقض التوحيد؟ Ushirikina Mitandaoni!
Play Video
Play Video
58:54
Darsa: Usuli Sunnah موقف الأمة الإسلامية من المبتدعة 🔴 LIVE | Darsa (III)
Darsa ilifanyika Swafar 23, 1447H Jumapili Agosti 17, 2025 موقف الأمة الإسلامية من المبتدعة Msimamo wa ummah wa Kiislamu kuhusiana na wazushi موقف الأمة الإسلامية من المبتدعة كيفية مواجهتهم لأصحابها Msimamo wa umma wa Kiislamu juu ya wazushi na jinsi ya kukabiliana na sahiba wa bidaa الفترة الأولى (٠٠٠ - ٣٧ه) فقد كانت فترة سليمة من تلك البدع Kipindi cha kwanza (000 - 37 H) ndio kipindi kilichokuwa safi kwa kuwa hakikuwa na aina yoyote ile ya bidaa. ولهذا تعتبر فترة ذهبية لوحدة الأمة واجتماعها على عقيدة واحدة Na kwa hilo ndio ikawa inachukuliwa kuwa ni kipindi cha dhahabu kwa umoja wa umma wa Kiislamu na ule mkusanyiko wake juu ya akida moja. فمن لم يقتد بالصحابة رضوان الله عليهم أجمعين ويسلك سبيلهم فإنه على شفا جرف هار Yeyote asiyefuata nyayo za Swahaba (Allah Awe Radhi Nao Jamia) na (akaachana na) Sabili njia yao, basi huyo yuko ukingoni mwa shimo. الفترة الثانية من سنة ٣٦ - ١٠٠ هـ Kipindi cha pili (37 - 100 H) ndio kipindi kulichoanza kudhuhiri vichwa vya bidaa: 1 Khawarij الخوارج 2. Shia الشيعة 3. Qadariyyah القدرية 4. Mur-jiah المرجئة الفترة الثالثة: ١٠١ - ١٧٧هـ Kipindi cha tatu (100 - 177H) ndio kipindi kulichodhihiri vichwa vya dhalala: 1. Al Ja'd bin Dirham الجعد بن درهم توفي بعد عام ١١٨هـ 2. Al Jahm bin Swaf-wan الجهم بن صفوان (١٢٨هـ) 3. Waasil bin Atwaa واصل بن عطاء (١٣١هـ) 4. Muqatil boin Sulaiman مقاتل بن سليمان (١٥٠هـ) الفترة الرابعة: ١٧٨ - ٣٠٠هـ Kipindi cha nne (178 - 300H) في هذه الفترة تبلورت كثير من البدع وتداخل بعضها في بعض، وأصبح لبعض المبتدعة قوة وسلطاناً، ولبعض البدع مدارس ومناهج Katika kipindi hiki, bidaa zilikuwa nyingi na kuunganika baadhi yake kwa baadhi na baadhi ya wazushi wakawa ni wenye mamlaka na sultani na kusikilizwa na wenye kushika hatamu za dola, na baadhi ya bidaa zikawa madrasah na mitaala yake. وقد ورد التعيين لأصول البدع لأول مرة في هذه الفترة على لسان يوسف ابن أسباط ثم عبد الله بن المبارك Asili za bidaa kwa mara ya kwanza ziliainishwa katika kipindi hiki na Yusuf Ibn Asbat na kisha Abdullah Ibn Al-Mubarak (Rahimahumullahu) Wakasema: Misingi ya bidaa ni mine: قالا: أصول البدع أربعة Rawaafidh الروافض Khawaarij والخوارج Qadariyyah والقدرية Mur-jiah والمرجئة الفترة الخامسة: ٢٣٢ - ٣٢٤هـ Kipindi cha tano (232 - 324H) Watu wenye kauli ambazo kwayo ndio msingi wa bidaa أشخاص لهم أقوال قامت عليها بدع 1. Ibn Kullab ابن كلاب 2. Muhammad ibn Karam al-Sijistani محمد بن كرام بن عراق أبي عبد الله السجستاني المتوفي سنة ٢٥٥هـ 3. Abul Hasan Al Ash'ari أبو الحسن الأشعري Mama ya makundi/mapote potovu أمهات الفرق الضالة 1 Khawaarij الخوارج 2. Shia الشيعة 3. Qadariyyah القدرية 4. Mur-jiah المرجئة 5. Aswufiyyah ( Masufi) الصوفية 6. Mu'tazila المعتزلة
Play Video
Play Video
58:55
Darsa حديث جبريل عليه السلام 🔴 LIVE Darsa مَراتِبِ شَهادةِ لا إلهَ إلَّا اللهُ
Darsa ilifanyika Swafar 21, 1447H Jumatano Agosti 15, 2025 مِن مَراتِبِ شَهادةِ لا إلهَ إلَّا اللهُ: العِلْمُ Elimu/Ujuzi ni miongoni mwa daraja za Kalima ya Tawhidi لا إلهَ إلَّا اللهُ Allah Amesema: شَهِدَ اللَّـهُ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ وَالْمَلَائِكَةُ وَأُولُو الْعِلْمِ قَائِمًا بِالْقِسْطِ ۚ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿١٨ "Allah Ameshuhudia kwamba hapana ilahi (mwenye kustahiki kuabudiwa kwa haki) isipokuwa Yeye, na (pia) Malaika na wenye ilimu (wameshuhudia hilo); na Yeye mbali ya hilo, Anasifika kwa uadilifu; hapana ilahi (mwenye kustahiki kuabudiwa kwa haki) isipokuwa Yeye Al Azizu Al Hakimu." Aal Imrani 3:18. لَّـٰكِنِ اللَّـهُ يَشْهَدُ بِمَا أَنزَلَ إِلَيْكَ ۖ أَنزَلَهُ بِعِلْمِهِ ۖ وَالْمَلَائِكَةُ يَشْهَدُونَ ۚ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ شَهِيدًا ﴿١٦٦ "Lakini Allah Anayashuhudia Aliyoyateremsha kwako, kwamba Ameyateremsha kwa Ilimu Yake, na Malaika pia wanashuhudia (hilo); na Anatosheleza Allah kuwa Mwenye Kushuhudia." An Nisaa 4:166
Play Video
Play Video
01:08:22
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات🔴LIVE باب الإصلاح بَيْنَ الناس
Darsa ilifanyika Swafar 19, 1447H Jumatano Agosti 13, 2025 باب الإصلاح بَيْنَ الناس Mlango wa Kusuluhisha Baini ya Watu :قَالَ الله تَعَالَى وَإِنِ امْرَأَةٌ خَافَتْ مِن بَعْلِهَا نُشُوزًا أَوْ إِعْرَاضًا فَلَا جُنَاحَ عَلَيْهِمَا أَن يُصْلِحَا بَيْنَهُمَا صُلْحًا ۚ وَالصُّلْحُ خَيْرٌ ۗ ﴿١٢٨ "Na ikiwa mke atahofia kutoka kwa mumewe uonevu wa ndoa au kutengwa, basi si vibaya juu yake wakisikilizana baina yao kwa suluhu; na suluhu ni bora.." An-Nisaa 4:128. لَّا خَيْرَ فِي كَثِيرٍ مِّن نَّجْوَاهُمْ إِلَّا مَنْ أَمَرَ بِصَدَقَةٍ أَوْ مَعْرُوفٍ أَوْ إِصْلَاحٍ بَيْنَ النَّاسِ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ ابْتِغَاءَ مَرْضَاتِ اللَّـهِ فَسَوْفَ نُؤْتِيهِ أَجْرًا عَظِيمًا ﴿١١٤ "Hakuna heri katika minong’ono yao mingi isipokuwa anayeamrisha Sadaka, au maarufu (mema), au kusuluhisha baina ya watu; na atakayefanya hivyo (kwa gharadhi ya) kutaka Radhi za Allah, basi Tutampa ujira adhimu." An-Nisaa 4:114. يَسْأَلُونَكَ عَنِ الْأَنفَالِ ۖ قُلِ الْأَنفَالُ لِلَّـهِ وَالرَّسُولِ ۖ فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَصْلِحُوا ذَاتَ بَيْنِكُمْ ۖ وَأَطِيعُوا اللَّـهَ وَرَسُولَهُ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ﴿١ "Wanakuuliza (ewe Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusiana na ghanima/ngawira; sema: Ngawira ni ya Allah na Rasuli, basi mcheni Allah na tengenezeni yaliyo baina yenu; na mtiini Allah na Rasuli Wake mkiwa ni Waumini." Al-Anfaal:1. إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ فَأَصْلِحُوا بَيْنَ أَخَوَيْكُمْ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ﴿١٠ "Hakika Waumini ni ndugu, basi suluhisheni baina ya ndugu zenu; na mcheni Allah ili mpate kurehemewa." Al-Hujuraat:10.
Play Video
Play Video
01:06:33
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات🔴LIVE باب باب الشفاعة
Darsa ilifanyika Swafar 18, 1447H Jumanne Agosti 12, 2025 باب الشفاعة Mlango wa Uombezi (shifaa) :قَالَ الله تَعَالَى مَّن يَشْفَعْ شَفَاعَةً حَسَنَةً يَكُن لَّهُ نَصِيبٌ مِّنْهَا ۖ وَمَن يَشْفَعْ شَفَاعَةً سَيِّئَةً يَكُن لَّهُ كِفْلٌ مِّنْهَا ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ مُّقِيتًا ﴿٨٥ "Atakayeombea uombezi mzuri atapata fungu lake katika hayo; na atakayeombea uombezi mbaya atapata sehemu yake katika hayo; na Allah daima ni Mwenye kudhibiti na Mwangalizi wa kila kitu." An-Nisaa 4:85. Hadithi – 1 وعن أَبي موسى الأشعري رضي الله عنه، قَالَ: كَانَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم إِذَا أتاهُ طَالِبُ حَاجَةٍ أقبَلَ عَلَى جُلَسَائِهِ ، فَقَالَ (( اشْفَعُوا تُؤْجَرُوا ، وَيَقْضِي الله عَلَى لِسَانِ نَبِيِّهِ مَاأحبَّ)) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ وفي رواية : (( مَا شَاءَ )) Kutokana na Abu Musa Al Ash'ariy (Allah Awe Radhi Nae) amesema kuwa Rasuli wa Allah (Swallallahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuwa anajiwa na mwenye haja, huwaelekea walioketi naye akiwaambia: " Ombeni mtalipwa, na Allah Hukidhi (haja) kwa ulimi wa Rasuli Wake Anavyopenda." Bukhari na Muslim. Na katika riwayah nyingine: " Anavyotaka". Hadithi – 2 وعن ابن عباس رضي الله عنهما في قِصَّةِ برِيرَةَ وَزَوْجِهَا ، قَالَ قَالَ لَهَا النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( لَوْ رَاجَعْتِهِ ؟ )) قَالَتْ : يَا رَسُولَ اللهِ تَأمُرُنِي ؟ قَالَ : (( إنَّمَا أَشْفَع )) قَالَتْ : لاَ حَاجَةَ لِي فِيهِ رواه البخاري Kutokana na Ibn Abbaas (Allah Awe Radhi Nae) kuhusiana na kisa cha Bariyrah (Allah Awe Radhi Nae) na mumewe, Rasuli wa Allah (Swallallahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia: "Waonaje lau ungerudi kwake?" (Bariyrah) akasema: " Ewe Rasuli wa Allah! Unaniamuru?" Akamjibu: "Hakika mimi naombea." (Bariyrah) akasema: "Sina haja naye." Bukhari
Play Video
Play Video
01:06:39
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات🔴LIVE باب قضاء حوائج المسلمين
Darsa ilifanyika Swafar 17, 1447H Jumatatu Agosti 11, 2025 باب قضاء حوائج المسلمين Mlango wa Kuwakidhia Waislamu haja zao قَالَ الله تَعَالَى يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا ارْكَعُوا وَاسْجُدُوا وَاعْبُدُوا رَبَّكُمْ وَافْعَلُوا الْخَيْرَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ۩﴿٧٧ "Enyi mlioamini! Rukuuni, na sujuduni na mwabuduni Rabi wenu, na fanyeni (mambo) ya heri ili mpata kufaulu." Al-Hajj: 77. Hadithi وعن ابن عمر رضي الله عنهما أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: المُسْلِمُ أخُو المُسْلِمِ ، لاَ يَظْلِمُهُ وَلاَ يُسْلِمُهُ . مَنْ كَانَ في حَاجَة أخِيه ، كَانَ اللهُ في حَاجَتِهِ وَمَنْ فَرَّجَ عَنْ مُسْلِمٍ كُرْبَةً، فَرَّجَ اللهُ عَنْهُ بِهَا كُرْبَةً مِنْ كرَبِ يَومِ القِيَامَةِ ، وَمَنْ سَتَرَ مُسْلِماً سَتَرَهُ اللهُ يَومَ القِيَامَةِ )). متفق عليه . Kutokana na Ibn Umar (Allah Awe Radhi Nao Jamia) kwamba Rasuli wa Allah (Swallallahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Muislamu ni ndugu wa Muislamu, hamdhulumu wala hamsalimishi (kwa adui), mwenye kumtekelezea haja nduguye, basi Allah Atamtekelezea haja yake, na mwenye kumuondolea Muislamu dhiki, basi Allah Atamuondolea dhiki miongoni mwa dhiki za Siku ya Qiyamah; na mwenye kumsitiri Muislamu, basi Allah Atamsitiri Siku ya Qiyamah." Al-Bukhari na Muslim. Hadithi – 2 وعن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: مَنْ نَفَّسَ عَنْ مُؤْمِنٍ كُرْبَةً مِنْ كُرَبِ الدُّنيَا ، نَفَّسَ الله عَنْهُ كُربَةً مِنْ كُرَبِ يَوْمِ القِيَامَةِ وَمَنْ يَسَّر عَلَى مُعْسِرٍ يَسَّرَ الله عَلَيهِ في الدُّنْيَا وَالآخِرَةِ ، وَمَنْ سَتَرَ مُسْلِماً سَتَرَهُ الله في الدُّنْيَا وَالآخِرَةِ والله في عَونِ العَبْدِ مَا كَانَ العَبْدُ في عَونِ أخِيهِ ، وَمَنْ سَلَكَ طَريقاً يَلْتَمِسُ فِيهِ عِلْماً سَهَّلَ اللهُ لَهُ طَريقاً إِلَى الجَنَّةِ وَمَا اجْتَمَعَ قَوْمٌ في بَيت مِنْ بُيُوتِ اللهِ تَعَالَى ، يَتْلُونَ كِتَابَ اللهِ ، وَيَتَدَارَسُونَهُ بَيْنَهُمْ إلاَّ نَزَلَتْ عَلَيْهِمُ السَّكِينَةُ ، وَغَشِيتْهُمُ الرَّحْمَةُ ، وَحَفَّتْهُمُ المَلاَئِكَةُ ، وَذَكَرَهُمُ الله فِيمَنْ عِندَهُ . وَمَنْ بَطَّأ بِهِ عَمَلُهُ لَمْ يُسْرِع بِهِ نَسَبُهُ رواه مسلم Kutokana na Abu Hurayrah (Allah Awe Radhi Nae) kutokana na Nabii (Swallallahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mwenye kumfariji Muumini dhiki miongoni mwa dhiki za duniani, Allah Atamfariji (na kumuondolea) dhiki miongoni mwa dhiki za Siku ya Qiyaamah, na mwenye kumsahilishia mwenye uzito, Allah Atamsahilishia duniani na Akhera, na mwenye kumsitiri Muislamu, basi Allah Atamsitiri duniani na Akhera, na Allah Humsaidia mja madama mja yu katika kumsaidia nduguye; na mwenye kufuata njia akitafuta elimu katika njia hiyo, basi Allah Atamsahilishia njia ya kwenda Jannah; na watu hawatakusanyika katika baiti miongoni mwa Baiti za Allah (Ta’alaa) wakisoma Kitabu cha Allah na wakidurusishana isipokuwa utulivu huwateremkia, na hufunikwa na Malaika na Allah Huwadhukuru kwa walio Kwake, na anayechelewesha amali yake hatopelekwa mbele kwa nasaba yake.” Muslim.
Contact
bottom of page