top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
59:16
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير 🔴 LIVE Aayah 148 -150 Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Shawwal 21, 1447H Alhamisi Aprili 09, 2026 Tafsiri ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة Kila Ummah una Qiblah لِكُلِّ أُمَّةٍ قِبْلَةٌ Kwa nini utajo wa kufutwa Qiblah umekaririwa mara tatu? لِمَاذَا تَكَرَّرَذِكْرُنَسْخِ القِبلةِ ثَلاَثَ مَرَّاتٍ ﴾وَلِكُلٍّ وِجْهَةٌ هُوَ مُوَلِّيهَا ۖ فَاسْتَبِقُوا الْخَيْرَاتِ ۚ أَيْنَ مَا تَكُونُوا يَأْتِ بِكُمُ اللَّـهُ جَمِيعًا ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١٤٨ "Na kila mmoja ana upande wa kuuelekea; basi shindaneni (katika) mambo ya kheri; popote mtakapokuwa Allah Atakuleteni pamoja jamia (Siku ya Qiyaamah); hakika Allah juu ya kila kitu ni Qadiru (Muweza)." [Al Baqarah 2:147] ﴾وَمِنْ حَيْثُ خَرَجْتَ فَوَلِّ وَجْهَكَ شَطْرَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ ۖ وَإِنَّهُ لَلْحَقُّ مِن رَّبِّكَ ۗ وَمَا اللَّـهُ بِغَافِلٍ عَمَّا تَعْمَلُونَ ﴿١٤٩ "Na popote utokako (ili kuswali), basi elekeza uso wako upande wa Masjidil-Haraam; na hiyo ni haki kutoka kwa Rabi wako; na Allah si Mwenye Kughafilika na yale myatendayo." [Al Baqarah 2:149] وَمِنْ حَيْثُ خَرَجْتَ فَوَلِّ وَجْهَكَ شَطْرَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ ۚ وَحَيْثُ مَا كُنتُمْ فَوَلُّوا وُجُوهَكُمْ شَطْرَهُ لِئَلَّا يَكُونَ لِلنَّاسِ عَلَيْكُمْ حُجَّةٌ إِلَّا الَّذِينَ ﴾ظَلَمُوا مِنْهُمْ فَلَا تَخْشَوْهُمْ وَاخْشَوْنِي وَلِأُتِمَّ نِعْمَتِي عَلَيْكُمْ وَلَعَلَّكُمْ تَهْتَدُونَ ﴿١٥٠ "Na popote utokako (ili kuswali), elekeza uso wako upande wa Masjidil-Haraam, na popote mtakapokuwa, elekezeni nyuso zenu upande wake, ili watu wasiwe na hoja juu yenu isipokuwa wale waliodhulumu miongoni mwao; basi msiwaogope bali Niogopeni Mimi, na ili Nitimize Neema Yangu juu yenu na ili mpate kuhidika." [Al Baqarah 2:150]
Play Video
Play Video
57:55
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير 🔴 LIVE Aayah 145 -147 Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Shawwal 20, 1447H Jumatano Aprili 08, 2026 Tafsiri ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة Inadi -ukaidi na upingaji- na ukanushaji wa Mayahudi عِنَادُ اليَهُود وجُحُودُهُم وَلَئِنْ أَتَيْتَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ بِكُلِّ آيَةٍ مَّا تَبِعُوا قِبْلَتَكَ ۚ وَمَا أَنتَ بِتَابِعٍ قِبْلَتَهُمْ ۚ وَمَا بَعْضُهُم بِتَابِعٍ قِبْلَةَ بَعْضٍ ۚ وَلَئِنِ اتَّبَعْتَ أَهْوَاءَهُم مِّن بَعْدِ ﴾مَا جَاءَكَ مِنَ الْعِلْمِ ۙ إِنَّكَ إِذًا لَّمِنَ الظَّالِمِينَ ﴿١٤٥﴾ "Na hata ukiwaletea wale waliopewa Kitabu Aayah (Ishara, Dalili) za kila aina, hawatofuata Qiblah chako; na wewe hutofuata Qiblah chao; na wala baadhi yao hawatofuata Qiblah cha wengineo; na kama ukiyafuata matamanio yao baada ya kukufikia ilimu, hakika hapo utakuwa miongoni mwa madhalimu." [Al Baqarah 2:145] مَعْرِفَةُ اليَهُودِ بِالنَّبِيَّ مُحَمَّدٍ صَلَّى اللهُ عَلَيْه وآله وسَلَّم وَكِتْمَانُهُمُ الحَقَّ Ujuzi wa Mayahudi kuhusu Nabii Muhammad صَلَّى اللهُ عَلَيْه وآله وسَلَّم na kuficha kwao ukweli. ﴾الَّذِينَ آتَيْنَاهُمُ الْكِتَابَ يَعْرِفُونَهُ كَمَا يَعْرِفُونَ أَبْنَاءَهُمْ ۖ وَإِنَّ فَرِيقًا مِّنْهُمْ لَيَكْتُمُونَ الْحَقَّ وَهُمْ يَعْلَمُونَ ﴿١٤٦ "Wale Tuliowapa Kitabu wanamtambua (Nabiy Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kama wanavyowatambua watoto wao, na hakika kundi miongoni mwao wanaficha haki na hali wao wanaelewa" [Al Baqarah 2:146]. ﴾الْحَقُّ مِن رَّبِّكَ ۖ فَلَا تَكُونَنَّ مِنَ الْمُمْتَرِينَ ﴿١٤٧ "(Ni) Haki kutoka kwa Rabi wako, basi kamwe usiwe miongoni mwa wenye shaka." [Al Baqarah 2:147]
Play Video
Play Video
59:56
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير 🔴 LIVE Aayah 144 Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Shawwal 19, 1447H Jumanne Aprili 07, 2026 afsiri ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة Kitu cha kwanza kilichofutwa kwenye Qur-aan kilikuwa ni Qiblah أَوَّلُ مَا نُسِخَ مَن القُرآنِ القِبْلَةُ هَلِ قِبْلَةُ عَيْنُ الكَعْبَةِ أَمْ جِهَةُ الكَعْبَةِ؟ Je, Qibla ni kulielekea Kaaba lenyewe au kuelekea upande wa Kaaba? مَسْأَلةُ تَحْوِيلِ القِبْلَةِ كَانَتْ مَعْلُومَةً عِنْدَ اليَهُوْدِ Suala la kubadilisha Qibla lilikuwa ni lenye kueleweka na kujulikana kwa Mayahudi. قَدْ نَرَىٰ تَقَلُّبَ وَجْهِكَ فِي السَّمَاءِ ۖ فَلَنُوَلِّيَنَّكَ قِبْلَةً تَرْضَاهَا ۚ فَوَلِّ وَجْهَكَ شَطْرَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِۚ وَحَيْثُ مَا كُنتُمْ فَوَلُّوا وُجُوهَكُمْ شَطْرَهُ ۗ وَإِنَّ ﴾الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ لَيَعْلَمُونَ أَنَّهُ الْحَقُّ مِن رَّبِّهِمْ ۗ وَمَا اللَّـهُ بِغَافِلٍ عَمَّا يَعْمَلُونَ ﴿١٤٤ "Kwa yakini Tunaona unavyogeuzageuza uso wako mbinguni; basi Sisi bila shaka Tutakuelekeza Qiblah unachokiridhia; kwa hiyo, elekeza uso wako upande wa Masjid Al-Haraam (Ka’bah; Makkah); na popote mtakapokuwepo (mkataka kusali), basi elekezeni nyuso zenu upande wake; na hakika wale waliopewa Kitabu bila shaka wanajua kwamba hivyo ni haki kutoka kwa Rabi wao; na Allah si Mwenye Kughafilika na yale wayatendayo." [Al Baqara 2:144]
Play Video
Play Video
01:04:40
Darsa: سنن أبي داود 🔴 LIVE | DARSA (II) رَاوِي الحَدِيثِ : حماد بن سلمة بن دينار Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Shawwal 18, 1447H Jumatatu Aprili 06, 2026 Sunan Abu Daud سنن أبي داود Kitabu cha Twahara كتاب الطهارة Mlango wa Rajuli kuchagua pahala pazuri pa kukojoa باب الرَّجُلِ يَتَبَوَّأُ لِبَوْلِهِ حَدَّثَنَا مُوسَى بْنُ إِسْمَاعِيلَ، حَدَّثَنَا حَمَّادٌ، أَخْبَرَنَا أَبُو التَّيَّاحِ، حَدَّثَنِي شَيْخٌ، قَالَ لَمَّا قَدِمَ عَبْدُ اللَّهِ بْنُ عَبَّاسٍ الْبَصْرَةَ فَكَانَ يُحَدَّثُ عَنْ أَبِي مُوسَى، فَكَتَبَ عَبْدُ اللَّهِ إِلَى أَبِي مُوسَى يَسْأَلُهُ عَنْ أَشْيَاءَ، فَكَتَبَ إِلَيْهِ أَبُو مُوسَى إِنِّي كُنْتُ مَعَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ذَاتَ يَوْمٍ فَأَرَادَ أَنْ يَبُولَ فَأَتَى دَمِثًا فِي أَصْلِ جِدَارٍ فَبَالَ ثُمَّ قَالَ صلى الله عليه وسلم " إِذَا أَرَادَ أَحَدُكُمْ أَنْ يَبُولَ فَلْيَرْتَدْ لِبَوْلِهِ مَوْضِعًا " . Wapokezi wa Hadithi hii رُوَاةُ هَذَا الحَدِيثِ 1. Musa bin Ismail (Rahimahullahu) مُوسَى بْنُ إِسْمَاعِيلَ 2. Hammad (Rahimahullahu) حَمَّادٌ 3. Abut Tiyyah (Rahimahullahu) أَبُو التَّيَّاحِ 4. Shaikh (Rahimahullahu) شَيْخٌ 5. Abu Musa (Allah Awe Radhi Nae) أَبُو مُوسَى Msimulizi wa Hadithi: Hammad bin Abu Salamah حماد بن سلمة بن دينار الاسم: حماد بن سلمة بن دينار الكنية: أبو سلمة النسب: البصري، الخزاز, التميمى، ويقال: القرشي مولاهم، وقد قيل: إنه حميري, السلمى, مولى بني ربيعة بن مالك بن حنظلة بلد الإقامة: البصرة علاقات الراوي: مولى تميم، ويقال: مولى قريش، ويقال: مولى ربيعة بن مالك بن حنظلة، ويقال: مولى حميري بن كرامة ويقال: مولى حميد بن كراثة، ابن أخت حميد الطويل تاريخ الوفاة: 167 هـ، أو 165 هـ بلد الرحلة: واسط طبقة رواة التقريب: من كبار الثامنة الرتبة عند ابن حجر: ثقه عابد، أثبت الناس في ثابت، وتغير حفظه بآخره الرتبة عند الذهبي: أحد الأعلام، ثقة صدوق يغلط، وليس في قوة مالك
Play Video
Play Video
01:00:09
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير 🔴 LIVE Aayah 142 -143 Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Shawwal 18, 1447H Jumatatu Aprili 06, 2026 SEHEMIU YA NNE Tafsiri ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة Katika hekima za kubadilishwa Qiblah مِنْ حكْمَةِ تَحْوِيلِ القِبْلَةِ ﴾سَيَقُولُ السُّفَهَاءُ مِنَ النَّاسِ مَا وَلَّاهُمْ عَن قِبْلَتِهِمُ الَّتِي كَانُوا عَلَيْهَا ۚ قُل لِّلَّـهِ الْمَشْرِقُ وَالْمَغْرِبُ ۚ يَهْدِي مَن يَشَاءُ إِلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ ﴿١٤٢ "Watasema masafihi miongoni mwa watu: Nini kilichowageuza (Waislamu) kutoka Qiblah chao ambacho walikuwa wakikielekea?! Sema: Mashariki na Magharibi ni ya Allah, Anamwongoza Amtakaye kuelekea sirati mustaqima (iliyonyooka)" [Al Baqarah 2:142] وَكَذَٰلِكَ جَعَلْنَاكُمْ أُمَّةً وَسَطًا لِّتَكُونُوا شُهَدَاءَ عَلَى النَّاسِ وَيَكُونَ الرَّسُولُ عَلَيْكُمْ شَهِيدًا ۗ وَمَا جَعَلْنَا الْقِبْلَةَ الَّتِي كُنتَ عَلَيْهَا إِلَّا لِنَعْلَمَ مَن يَتَّبِعُ الرَّسُولَ مِمَّن يَنقَلِبُ عَلَىٰ عَقِبَيْهِ ۚ وَإِن كَانَتْ لَكَبِيرَةً إِلَّا عَلَى الَّذِينَ هَدَى اللَّـهُ ۗ وَمَا كَانَ اللَّـهُ لِيُضِيعَ إِيمَانَكُمْ ۚ إِنَّ اللَّـهَ بِالنَّاسِ لَرَءُوفٌ رَّحِيمٌ ﴿١٤٣ "Na ndivyo hivyo Tumekufanyeni ummah bora na adilifu ili muwe mashahidi juu ya watu na awe Rasuli shahidi juu yenu; na Hatukukifanya Qiblah ambacho ulikuwa ukikielekea (Baytul-Maqdis) isipokuwa Tupate kupambanua nani anayemfuata Rasuli kikweli, na nani atakayegeuka arudi nyuma; na hakika ilikuwa ni jambo gumu isipokuwa kwa wale ambao Allah Amewaongoza; na Allah Hakuwa Mwenye Kupoteza imani (Sala) zenu; hakika Allah ni Raufu Rahimu" [Al Baqarah 2:143]
Play Video
Play Video
01:01:26
Darsa: صحيح مسلم 🔴LIVE | DARSA (III) رَاوِي الحَدِيثِ : حَمَّادُ بْنُ زَيْدٍ Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Shawwal 17, 1447H Jumapili Aprili 05, 2026 Kitabu cha Imani كتاب الإيمان باب بيان الإيمان والإسلام والإحسان ووجوب الإيمان بإثبات قدر الله سبحانه وتعالى وبيان الدليل على التبري ممن لا يؤمن بالقدر وإغلاظ القول في حقه Sanad ya PILI YA HADITHI YA Jibril عليه السلام Wapokezi wa Hadithi hii رُوَاةُ هَذَا الحَدِيثِ Hadithi ina wapokezi wafuatao: 1. Muḥammad bin Ubayd al-Ghubari (Rahimahullahu) مُحَمَّدُ بْنُ عُبَيْدٍ الْغُبَرِيُّ 2. Abu Kamil al-Jaḥdari (Rahimahullahu) أَبُو كَامِلٍ الْجَحْدَرِيُّ 3. Aḥmad bin Abdah (Rahimahullahu) أَحْمَدُ بْنُ عَبْدَةَ 4. Ḥammad bin Zayd (Rahimahullahu) حَمَّادُ بْنُ زَيْدٍ 5. Maṭwar al-Warraq (Rahimahullahu) مَطَرٍ الْوَرَّاقِ 6. Abdullah bin Buraydah (Rahimahullahu) عَبْدِ اللَّهِ بْنِ بُرَيْدَةَ 7. Yaḥya bin Yaʿmar (Rahimahullahu) يَحْيَى بْنِ يَعْمَرَ Msimulizi wa Hadithi: Ḥammad bin Zayd (Rahimahullahu) حماد بن زيد بن درهم لاسم: حماد بن زيد بن درهم اللقب: الأزرق الكنية: أبو إسماعيل النسب: الأزدي، الجهضمي، البصري، الأزرق بلد الإقامة: البصرة علاقات الراوي: مولى آل جرير بن حازم الجهضمي، كان جده درهم من سبي سجستان، أخو سعيد بن زيد المذهب العقدي وقال عبيد الله بن يوسف الحبيري، عن فطر بن حماد بن واقد: سألت حماد بن زيد قلت: يا أبا إسماعيل إمام لنا يقول: القرآن مخلوق، أصلي خلفه ؟ قال: لا، ولا كرامة وقال أبو بكر بن أبي الدنيا، عن خالد بن خداش: سمعت حماد بن زيد يقول لئن قلت: إن عليا أفضل من عثمان، لقد قلت: إن أصحاب رسول الله صلى الله عليه وسلم قد خانوا تاريخ الميلاد: 98 هـ، أو زمن سليمان بن عبد الملك، أو زمن عمر بن عبد العزيز تاريخ الوفاة: 177 هـ، وقيل 179 هـ طبقة رواة التقريب: من كبار الثامنة الرتبة عند ابن حجر: ثقة ثبت، فقيه الرتبة عند الذهبي أحد الأعلام أضر، وكان يحفظ حديثه كالماء، قال ابن مهدي: ما رأيت أحدا لم يكتب أحفظ منه وما رأيت بالبصرة أفقه منه، ولم أر أعلم بالسنة منه
Play Video
Play Video
01:05:22
Darsa: حَقُّ الوَلِدَينِ 🔴 LIVE | DARSA Haki za Wazazi Wawili (II) Ust. Abu Raifah
Darsa ilifanyika Shawwal 17, 1447H Jumapili Aprili 05, 2026 Haki za Wazazi Wawili حَقُّ الوَلِدَينِ Jambo la Pili: Kujiepusha kuwakata na kuwafanyia vitu vibaya. تجنب عقوقهما، والإساءة إليهما Muradi wa kutowatii wazazi wawili ni kuwafanyia chochote kile chenye kuwaudhi na kinachosababisha madhara kwao iwe kwa maneno au matendo; nalo ni haramu na ni katika dhambi kubwa. ﴾إِمَّا يَبْلُغَنَّ عِندَكَ الْكِبَرَ أَحَدُهُمَا أَوْ كِلَاهُمَا فَلَا تَقُل لَّهُمَا أُفٍّ وَلَا تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلًا كَرِيمًا ﴿٢٣ "Kama mmoja wao akifikia uzee naye yuko pamoja nawe, au wote wawili basi usiwaambie, Uff! Na wala usiwakemee, na waambie maneno ya heshima." [Al Is-raa 17:23] عَنْ عَبْدِ الرَّحْمَنِ بْنِ أَبِي بَكْرَةَ، عَنْ أَبِيهِ ـ رضى الله عنه ـ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم " أَلاَ أُنَبِّئُكُمْ بِأَكْبَرِ الْكَبَائِرِ ". قُلْنَا بَلَى يَا رَسُولَ اللَّهِ. قَالَ " الإِشْرَاكُ بِاللَّهِ، وَعُقُوقُ الْوَالِدَيْنِ ". Kutokana na Abdur Rahmaan bin Abu Bakrah kutokana baba ake رضى الله عنه amesema kuwa: 'Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم amesema: "Je, hivi nikujulisheni dhambi kubwa kabisa?! Tukasema: Ndio (yaani: tujulishe) ewe Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم! Basi Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم akasema: "Kumshirikisha Allah, na kuwaasi -kuwakata- wazazi wawili .." Wamewafikiana Bukhari na Muslim. Kuwaasi -kuwakata/kutowatii wazazi wawili kuko aina mbili: Ya Kwanza: Kwa kauli Ya Pili: Kwa vitendo Hatari ya kuwakata wazazi wawili خطر عقوق الوالدين
Play Video
Play Video
01:33:18
Darsa مَاذَا بَعْدَ رَمَضَانَ 🔴 DARSA: أَحَبُّ الْأَعْمَالِ إِلَى الله أدومها وَإِن قل Ust. Hassan
Darsa ilifanyika Shawwal 17, 1447H Jumapili Aprili 05, 2026 Nini baada ya Ramadhani? مَاذَا بَعْدَ رَمَضَانَ Shahari ya Ramadhani imekwishatuaga, Shahari yenye kheri nyingi; michana yake ilikuwa ni subira ya Saumu, na nyakati za usiku wake zilikuwa ni nyakati za Qiyamul (kusimamo cha usiku). Shahari ya Qur-aani imetuaga, Shahari ya tak-wa, na Jihaad, na maghufira, Shahari ya kuomba dua kwa wingi, Shahari ya kutolewa Nari na kutunukiwa Jannah. Amefaulu aliyetimiza funga yake, na kisimamo chake na kisimamo cha Usiku wa Qadri kwa imani na kutarajia malipo Kwa bahati mbaya amehasirika yule aliyejinyima kuchangamkia fursa zilizokuwemo ndani ya Shahari ya Ramadhani kwa kutoweza kufikia kuelewa umuhimu wake na wala fadhila zake. Gharadhi kuu ya Shahari ilikuwa kutufikisha kwenye Taq-wa; kwa Kauli Yake Allah: ﴾يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣ "Enyi mlioamini! Mmefaridhishwa Siyamu kama ilivyofaradhishwa kwa wale ambao wa kabla yenu mpate kuwa na Taq-wa" [Baqarah 2:183]. Muislamu aliyejaaliwa kuingia katika Shahari ya Ramadhani na kutoka alitarajiwa aelewe kuwa aliingia katika madrasa ya Taq-wa. Na mwenye kuingia katika madrasa yoyote ile, hutarajiwa kutoka humo huku akiwa amepata manufaa au shahada ya lile somo alilolisoma, na baada ya hapo huitumia ile elimu aliyoisoma kumsaidia katika kuendesha maisha yake; pia huendelea kuitumia hiyo elimu katika maisha yake yote hadi kifo kumfikie. Anasema Allaah Subhanahu wa Ta’alaa: وَاعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّى يَأْتِيَكَ الْيَقِينُ "Na muabudu Rabi wako mpaka ikufikie yakini (mauti)" [Al-Hijr 16: 99]. Kuthibitika -kuendelea- katika ibada baada ya Shahari ya Ramadhani ni moja kati ya alama au sababu zenye kuonyesha kutakabaliwa kwa amali zilizikuwemo kwenye Shahari ya Ramadhani. Ni vyema tuwe tunajiuliza maswali kama haya: 1. Je, Umekufikia mchana mmoja ukiwa katika kufunga za Sunnah? 2. Je, Umekufikia usiku mmoja ukiwa katika kisimamo? 3. Je, Unaendelea kusoma Qur-aani kama ulivyokuwa ukisoma katika Ramadhani? 4. Je, Unaendelea kumdhukuru Allah kwa wingi kama ulivyokuwa ukimdhukuru katika Ramadhani? 5. Je, unaendelea kububujika machozi kwa kukumbuka dhambi zake na kuhofia adhabu za Allah kama ulivyokuwa kwenye Shahari ya Ramadhani? Je, tunaelewa kwamba Allah Anapenda zaidi amali zenye kuendeleza -zenye kudumu- japokuwa ni kalili -chache- kuliko amali nyingi zisizodumu?! قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((أَحَبَّ الْأَعْمَالِ إِلَى اللَّهِ أَدْوَمُهَا وَإِنْ قَلَّ)) متفق عليه Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم amesema kuwa: " Amali zinazopendeza zaidi mbele ya Allah ni zile zenye kudumu -zenye kuendelea-japokuwa ni kalili" [Wamewafikiana Bukhari na Muslim] Basi tujaribu kwa Tawfiki Yake Allah kuthibiti katika Shahari nyenginezo kwa amali ambazo tulikuwa tukizitekeleza kwenye Shahari ya Ramadhani ikiwemo kufunga Saumu za Sunnah kama hizi: i-Siku Sita za Shawwal ستة أيام من شوال Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: "من صام رمضان ثم أتبعه ستاً من شوال، كان كصيام الدهر" "Yeyote yule ataliyefunga Shahari ya Ramadhani, kisha akafuatia (Siku) Sita za Shawwal atapata ujira wa aliyefunga dahari -mwaka mzima-". ii-Siku za Jumatatu na Alhamisi صيام أيام الاثنين والخميس Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: " تُعْرَضُ الْأَعْمَالُ يَوْمَ الِاثْنَيْنِ وَالْخَمِيسِ فَأُحِبُّ أَنْ يُعْرَضَ عَمَلِي وَأَنَا صَائِمٌ " "Amali huwekwa mbele ya Allah kila Siku ya Jumatatu na Alhamisi, basi napenda amali yangu iwekwe mbele ya Allah nikiwa nimefunga" iii-Siku tatu katika kila Shahari الأيام البيض: الثالث عشر، والرابع عشر، والخامس عشر من كل شهر هجري Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: "يَا أَبَا ذَرٍّ، إِذَا صُمْتَ مِنَ الشَّهْرِ ثَلاثَةَ أَيَّامٍ فَصُمْ ثَلاثَةَ عَشَرَ وَأَرْبَعَةَ عَشَرَ وَخَمْسَةَ" "Ewe Abu Dharr! Endapo utafunga Siku tatu za katika Shahari, basi funga Siku ya 13, ya 14, na ya 15" iv-Siku ya Arafah صيام يوم عرفة (9 ذي الحجة): لغير الحاج Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: " يكفِّرُ السَّنَةَ المَاضِيةَ وَالبَاقِيَةَ" "Inafuta dhambi za mwaka uliopita na mwaka uliopo" v-Siku ya Ashuraa na Tasu'aa صيام يوم عاشوراء (10 محرم): ويستحب صيام يوم قبله (تاسوعاء) أو بعده Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: "صِيَامُ يَوم عاشوراء إنِّي أحْتَسبُ علَى اللهِ أن يُكفِّرَ السَّنةَ التِي قبلَه" "Saumu ya siku ya Ashuraa, nategemea kutoka kwa Allah Ayafute madhambi ya mwaka uliotangulia." vi- Kufunga Shahari ya Muharram صيام شهر محرم "أَفْضَلُ الصِّيَامِ بَعْدَ رَمَضَانَ شَهْرُ اللَّهِ الْمُحَرَّمُ "
Contact
bottom of page