top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
40:42
Darsa: Mirathi:أَقْسَامُ الوَرَثَةِ بِاعْتِبَارِالإِرْثِ 🔴 LIVE UMMU أُمٌّ (II) Dr. Ibrahim Bulushi
Darsa ilifanyika Swafar 11, 1448H Jumamosi Julai 25, 2026 أَقْسَامُ الوَرَثَةِ بِاعْتِبَارِالإِرْثِ َMakundi (vigawanyo) vya Warithi kwa kuzingatia (namna za) KURITHI KUNDI LA KWANZA Wenye Kurithi kwa FAR-DHU PEKEE من يَرِثُ بِالْفَرْضِ فَقَط Warithi wenye kustahiki kurithi kwa FAR DHU PEKEE ni SABA (7) 1. UMMU أُمٌّ 2. MUME الزَّوْجُ 3. MKE زوْجَةٌ 4. BIBI (NYANYA) KWA MAMA جَدَّةٌ 5. BIBI (NYANYA) KWA BABA جَدَّةٌ 6. AKH KWA MAMA MMOJA الأخُ لأمِّ 7. UKHTI KWA MAMA MMOJA الأُخْت لأمّ Mrithi wa kwanza mwenye kustahiki kurithi kwa FAR DHU PEKEE MAMA/UMMU أُمٌّ UMMU hustahiki kurithi FAR DHU TATU (3) PEKEE: 1. SUDUSI (1/6) السُّدُسُ 2. THELUTHI (1/3) الثُّلُثُ 3. THELUTHI ILIYOBAKI ثلث الباقي UMMU/MAMA HUSTAHIKI KURITHI KWA FAR DHU KATIKA HALI NNE (4): HALI YA KWANZA ﴾وَلِأَبَوَيْهِ لِكُلِّ وَاحِدٍ مِّنْهُمَا السُّدُسُ مِمَّا تَرَكَ إِن كَانَ لَهُ وَلَدٌ ﴿١١ “Na WAZAZI WAKE WAWILI (UMMU/MAMA NI MMOJA WA HAO WAZAZI WAWILI) kila mmoja wao atastahiki SUDUSI (1/6) katika alichoacha (MRITHIEWA) IKIWA (MRITHIWA) ANA WALAD ....” [An Nisaa 4:11] HALI YA PILI : ﴾فَإِن كَانَ لَهُ إِخْوَةٌ فَلِأُمِّهِ السُّدُسُ ۚ ﴿١١ "Na ikiwa (mrithiwa) ana Ikhwah (yaani: ndugu: wa kike au wa kiume) basi UMMU/MAMA wake atastahiki SUDUSI (1/6) ..” [An Nisaa 4:11] HALI YA TATU: ﴾وَوَرِثَهُ أَبَوَاهُ فَلِأُمِّهِ الثُّلُثُ ۚ ﴿١١ “Na (ikiwa) WAZAZI WAKE WAWILI NDIO WARITHI WAKE (MRITHIWA: YAANI HAKUNA MRITHI ISIPOKUWA WAZAZI WAWILI PEKEE), BASI UMMU/MAMA YAKE ATASTAHIKI THELUTHI (1/3)..” [An Nisaa 4:11] HALI YA NNE: مسألة العمريتين MAS-ALA ZENYE KUELEWEKA KWA JINA LA: AL UMARIYYATAYNI AMBAYO YAKO NA HALI MBILI
Play Video
Play Video
58:01
Darsa: (VI) نَوَاقِضُ لَا إِلَهَ إِلاَّ اللهِ 🔴 اعْلَمْ أنَّ مِنْ أَعْظَمِ نَوَاقِضِ الإِسْلَامِ
Darsa ilifanyika Swafar 10, 1448 H Ijumaa Julai 24, 2026 SEHEMU YA SITA Utangulizi تَمْهِيد Vitenguzi vya kalimat -neno laTawhidi نَوَاقِضُ لَا إِلَهَ إِلاَّ اللهِ Vitenguzi vya Tawhidi نَوَاقِضُ التَّوْحِيد Vitenguzi vya Uislamu نَوَاقِضُ الِإسْلاَم اعْلَمْ أنَّ مِنْ أَعْظَمِ نَوَاقِضِ الإِسْلَامِ عَشْرَةَ Elewa kwamba katika vitenguzi VIKUBWA kabisa vya Uislamu ni mambo KUMI. Elewa na tambua na uwe na yakini ya kwamba Uislamu wa mtu unatenguka kwa kufanya moja lolote lile miongoni mwa mambo kumi yenye kutengua Uislamu.
Play Video
Play Video
01:05:42
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات🔴LIVE (II) باب الكرم والجود والإنفاق في وجوه الخير Sh Salim
Darsa ilifanyika Swafar 08, 1448 H Jumatano Julai 22, 2026 باب الكرم والجود والإنفاق في وجوه الخير ثقةً بالله تعالى Mlango wa ukarimu na kutoa katika njia za heri na kuwa na matumaini na Allah تعالى SEHEMU YA PILI :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَمَا أَنفَقْتُم مِّن شَيْءٍ فَهُوَ يُخْلِفُهُ ۖ ﴿٣٩ "Na kitu chochote mtoacho, basi Yeye Atakilipa..". [Sabaa 34: 39] ﴾وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَلِأَنفُسِكُمْ ۚ وَمَا تُنفِقُونَ إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ اللَّـهِ ۚ وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ يُوَفَّ إِلَيْكُمْ وَأَنتُمْ لَا تُظْلَمُونَ ﴿٢٧٢ "Na chochote cha heri mtoacho basi ni kwa ajili ya nafsi zenu; na hamtoi isipokuwa kutaka Wajhi wa Allah; na chochote mtoacho katika heri mtalipwa kamilifu nanyi hamtodhulumiwa." [Al-Baqarah 2: 272] ﴾ وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٢٧٣ "Na chochote mtoacho katika heri basi Allah kwacho ni Alimu (Mjuzi)." [Al-Baqarah 2:273]
Play Video
Play Video
01:00:16
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات🔴LIVE (I) باب الكرم والجود والإنفاق في وجوه الخير Sh Salim
Darsa ilifanyika Swafar 07, 1448 H Jumanne Julai 21, 2026 باب الكرم والجود والإنفاق في وجوه الخير ثقةً بالله تعالى Mlango wa ukarimu na kutoa katika njia za heri na kuwa na matumaini na Allah تعالى SEHEMU YA KWANZA :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَمَا أَنفَقْتُم مِّن شَيْءٍ فَهُوَ يُخْلِفُهُ ۖ ﴿٣٩ "Na kitu chochote mtoacho, basi Yeye Atakilipa..". [Sabaa 34: 39] ﴾وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَلِأَنفُسِكُمْ ۚ وَمَا تُنفِقُونَ إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ اللَّـهِ ۚ وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ يُوَفَّ إِلَيْكُمْ وَأَنتُمْ لَا تُظْلَمُونَ ﴿٢٧٢ "Na chochote cha heri mtoacho basi ni kwa ajili ya nafsi zenu; na hamtoi isipokuwa kutaka Wajhi wa Allah; na chochote mtoacho katika heri mtalipwa kamilifu nanyi hamtodhulumiwa." [Al-Baqarah 2: 272] ﴾ وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٢٧٣ "Na chochote mtoacho katika heri basi Allah kwacho ni Alimu (Mjuzi)." [Al-Baqarah 2:273]
Play Video
Play Video
01:05:38
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات🔴LIVE باب جواز الأخذ من غير مسألة وَلاَ تطلع إليه Sh Salim
Darsa ilifanyika Swafar 06, 1448 H Jumatatu Julai 20, 2026 باب جواز الأخذ من غير مسألة وَلاَ تطلع إليه Mlango wa ruhusu ya kuchukua pasina kuomba na wala kuwa na tamaa ya kupata :عن سالم بن عبد الله بن عمر ـ رضى الله عنه ـ عن أبيه عبد الله بن عمر ـ رضى الله عنه ـ عن عمر رضي الله عنه قَالَ كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم يُعْطيني العَطَاءَ فَأقُولُ : أعطِهِ مَنْ هُوَ أفْقَرُ إِلَيْهِ مِنّي فَقَالَ : (( خُذْهُ ، إِذَا جَاءكَ مِنْ هَذَا المَال شَيْءٌ وَأنْتَ غَيْرُ مُشْرِفٍ وَلاَ سَائِلٍ فَخُذْهُ فَتَمَوَّلْهُ ، فَإنْ شِئْتَ كُلْهُ ، وَإنْ شِئْتَ تَصَدَّقْ بِهِ ، وَمَا لا ، فَلاَ تُتبعهُ نَفْسَكَ قَالَ سَالِمٌ : فَكَانَ عَبدُ الله لاَ يَسألُ أحَداً شَيْئاً ، وَلاَ يَرُدُّ شَيْئاً أُعْطِيَه . متفقٌ عَلَيْهِ Kutokana na Salim bin Abdillah bin Omar ـ رضى الله عنه ـ kutokana na babake Abdillah bin Omar ـ رضى الله عنه ـ kutokana na Omar ـ رضى الله عنه ـ amesema kuwa: "Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسل alikuwa akinipatia vitu (zawadi), nami nilikuwa nikisema: 'Mpatie aliye fukara kuliko mimi.' Basi Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسل akasema: "Chukua ikiwa utapewa katika mali hii kitu chochote bila ya wewe kutamani wala kuuliza (kuomba); ichukue na uitie katika rasilimali au ukitaka itumie na ukitaka unaweza kuitoa sadaka, usitamani kupata kitu kwa njia nyengine.' Salim amesema: 'Alikuwa Abdillah ـ رضى الله عنه ـ (yaani babake) hamuulizi (hamuombi) yeyote yule kitu chochote wala harudishi kitu alichopatiwa'." [Wamewafikiana Bukhari na Muslim] باب الحث عَلَى الأكل من عمل يده والتعفف به عن السؤال والتعرض للإعطاء Mlango wa Kuhimiza kula kwa amali -kazi- ya mkono wake na kujizuilia kuomba na kupenda kutoa :قَالَ الله تَعَالَى ﴾فَإِذَا قُضِيَتِ الصَّلَاةُ فَانتَشِرُوا فِي الْأَرْضِ وَابْتَغُوا مِن فَضْلِ اللَّـهِ ﴿١٠ "Na inapomalizika Sala, basi tawanyikeni katika ardhi, na tafuteni katika Fadhila za Allah.." [Al-Jumu'ah:10].
Play Video
Play Video
01:14:47
Tadabburul Qur- aani تَدَبُّرُ القُرْآن 🔴LIVE DARSA دروسٌ وعِبرٌ من قصة العِجل والبقرة
Darsa ilifanyika Swafar 05, 1448 H Jumapili Julai 19, 2026 تأملات في سورة البقرة : دروسٌ وعِبرٌ من قصة العِجل والبقرة Tadabbur Surat Al-Baqarah (2:67–93): Kisa cha Ndama na Ng'ombe - Mazingatio kwa Kila Muumini - Surat Al-Baqarah, Surah ndefu katika Qur aani - Kwanini ikaitwa Baqarah (Ng'ombe)? - Je, ng'ombe ana umuhimu gani kiasi cha Surah ndefu katika Qur aani kuitwa kwa jina lake?
Play Video
Play Video
01:15:45
Mhadhara: هَجْرُ القرآنِ الكريمِ 🔴 LIVE | Kuihama -kuihajiri- Qur aani Ust Salim Khatib
Darsa ilifanyika Swafar 03, 1448 H Ijumaa Julai 17, 2026 Kuihama -kuihajiri/kuigura- Qur aani هَجْرُ القرآنِ الكريمِ Kuhusiana na kuihajiri Qur aani; amesema Ibn Al Qayyum رَحِمَهُ اللهُ kuwa: Kuihama -kuihajiri/kuigura- Qur aani kuko kwa namna :هَجْرُ القرآنِ أنواعٌ Aina ya Kwanza: Kuacha kuisoma هَجْرُ تِلاوتِه Aina ya Pili: Kuacha kuisikiliza هَجْرُ استماعِه والإصغاءِ إليه Aina ya Tatu: Kuacha kuizingatia na kuielewa تَدبُّرِه وتَفهُّمِه Aina ya Nne: Kuacha kuitendea kazi هَجْرُ العَمَلِ به Aina ya Tano: Kuacha kutafuta shifaa na matibabu kwayo هَجْرُ الاستشفاءِ به والتَّداوي Aina ya Sita: Kuihama kwa kutoifanya kuwa ndio muamuzi هَجْرُ تحكيمِهِ والتَّحاكُمِ إليه Na aina zote hizi zinaingia kwenye Kauli Yake: ﴾وَقَالَ الرَّسُولُ يَا رَبِّ إِنَّ قَوْمِي اتَّخَذُوا هَـٰذَا الْقُرْآنَ مَهْجُورًا ﴿٣٠ "Na Rasuli akasema: “Rabi wangu! Hakika watu wangu wameifanya hii Qur-aani ni yenye kuhamwa." [Al-Furqaan 25:30].
Play Video
Play Video
45:08
Darsa: سنن ابن ماجه 🔴 LIVE | DARSA (IV) رَاوِي الحَدِيثِ : ابْنِ الْمُبَارَكِ Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Swafar 02, 1448 H Alhamisi Julai 16, 2026 HADITHI YA NNE Sunan Ibn Maajah سنن ابن ماجه Kitabu cha Utangulizi كتاب المقدمة باب اتِّبَاعِ سُنَّةِ رَسُولِ اللَّهِ ـ صلى الله عليه وسلم ـ Mlango wa kufuata Sunnah za Rasuli wa Allah ـ صلى الله عليه وسلم ـ حَدَّثَنَا مُحَمَّدُ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ نُمَيْرٍ، حَدَّثَنَا زَكَرِيَّا بْنُ عَدِيٍّ، عَنِ ابْنِ الْمُبَارَكِ، عَنْ مُحَمَّدِ بْنِ سُوقَةَ، عَنْ أَبِي جَعْفَرٍ، قَالَ كَانَ ابْنُ عُمَرَ إِذَا سَمِعَ مِنْ، رَسُولِ اللَّهِ ـ صلى الله عليه وسلم ـ حَدِيثًا لَمْ يَعْدُهُ وَلَمْ يُقَصِّرْ دُونَهُ . Ametuhadithia Muhammad bin Abdullah bin Numayri, ametuhadithia Zakariya bin Adiy kutokana na Ibn Mubarak kutokana na Muhammad bin Suqah kutokana na Abu Ja'far amesema kuwa:' Alikuwa Ibn Omar (رضي الله عنه) kila pale anaposikia Hadithi kutoka kwa Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) basi hangefanya zaidi ya ilivyosemwa, na wala hangekusuru.' Wapokezi wa Hadithi hii رُوَاةُ هَذَا الحَدِيثِ 1. Muhammad bin Abdullah bin Numayri (Rahimahullahu) مُحَمَّدُ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ نُمَيْرٍ 2. Zakariya bin Adiy (Rahimahullahu) زَكَرِيَّا بْنُ عَدِيٍّ 3. Ibn Mubarak (Rahimahullahu) ابْنِ الْمُبَارَكِ 4. Muhammad bin Suqah (Rahimahullahu) مُحَمَّدِ بْنِ سُوقَةَ 5. Abu Ja'far (Rahimahullahu) أَبُوجَعْفَرٍ Msimulizi wa Hadithi: Ibn Mubarak (Rahimahullahu) ابْنِ الْمُبَارَكِ لاسم: عبد الله بن المبارك بن واضح الكنية: أبو عبد الرحمن النسب: الحنظلي مولاهم, التميمي مولاهم, المروزي بلد الإقامة: خراسان، الكوفة علاقات الراوي: مولى بني حنظلة، ومولى لعبد شمس من تميم تاريخ الميلاد: 118 هـ، أو 119 هـ تاريخ الوفاة: 181 هـ، أو 182 هـ بلد الوفاة: هيت، مات في السفينة في الفرات وأخرج منها فدفن بهيت بلد الرحلة: خرج عبد الله إلى العراق، بغداد، اليمن، الشام، البصرة، الكوفة تاريخ الرحلة: 141 هـ طبقة رواة التقريب: الثامنة الرتبة عند ابن حجر: ثقة ثبت، فقيه عالم، جواد مجاهد، جمعت فيه خصال الخير الرتبة عند الذهبي: شيخ خرسان
Contact
bottom of page