top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
01:07:04
DARSA: التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُهُ🔴DARSA:Kushikamana na Sunnah (VII) Abu Arqam
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 06, 1448 H Jumatano Agosti 19, 2026 SEHEMU YA SABA التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُ Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ na Athari Zake Sunnah ni shaqiqi -ndugu wa kwa baba na mama mmoja/mwenza- wa Qur aani katika kuwa hoja, hivyo basi ni wajibu kwetu kuifuata Sunnah kama ilivyo wajibu kwetu kuifuata Qur aani. Sunnah ni kila kilichothibiti kutokana na Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ kuanzia kauli yake, au kitendo chake , au kulikubaliNabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ jambo ambalo limefanywa mbele yake na yeye hakulikataza iliyopokelewa kwa usahihi kutoka kwa Mtume صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ. Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ni wajibu juu ya kila Muislamu kama vile ilivyo wajibu kwake kushikamana na Qur aani sawa kwa sawa. Hata hivyo, kwa yeyote yule anaeitumia Qur aani kama ni ushahidi wa mtazamo au hukumu fulani basi huwa anahitaji kuzingatia jambo moja pekee, walakini yule ambae anaitumia Sunnah kama ndio ushahidi wake basi huwa anahitaji kuzingatia mambo mawili. Mtu anapotoa Qur aani kama ndio ushahidi, huwa anapaswa kuangalia maana ya Aayah husika na jinsi inavyoashiria hukumu anayotafutia uthibitisho. Bila shaka yoyote ile, watu hutofautiana sana katika suala hili, kulingana na viwango vyao vya elimu na uelewa/ufahamu wao. Ama kwa yule mwenye kutohowa dalili kutoka katika Sunnah, huwa anahitaji kuangalia mambo mawili: Jambo la Kwanza: Uhalisi wa Hadithi husika, kwani kuna mapokezi mengi dhaifu na ya kubuni ambayo yameingia katika Sunnah. Hivyo, ni lazima kuihakiki Hadithi kabla ya kuitumia kama hoja. Kwa sababu hii, wanavyuoni رَحْمَهُمُ اللهُ waliandika vitabu kuhusu wapokezi wa Hadithi na istilahi zake na sanad zake, kwa lengo la kubainisha mapokezi sahihi na yale yasiyo sahihi. Jambo la Pili: Kama ilivyo katika suala la kutumia Qur aani kama hoja, yule anaetumia Sunnah kama hoja huwa anapaswa kuangalia maana inayoelekezwa na Hadithi husika na namna inavyoweza kutumika kuthibitisha hukumu husika; na watu hutofautiana sana katika jambo hili. Allah Akimhutubia Rasuli Wake صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ Amesema: ﴾وَأَنزَلَ اللَّـهُ عَلَيْكَ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَعَلَّمَكَ مَا لَمْ تَكُن تَعْلَمُ ۚ ... ﴿١١٣ "Na Allah Amekuteremshia Kitabu (Qur aani) na Hikmah (Sunnah) na Akakufunza yale ambayo hukuwa unayajua .." [An Nisaa 4:113]
Play Video
Play Video
01:09:03
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴 LIVE باب الورع وترك الشبهات Sh Salim
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 06, 1448 H Jumatano Agosti 19, 2026 SEHEMU YA PILI باب الورع وترك الشبهات Mlango wa Kujichunga na Kuacha Mambo Yenye Shaka (vidanganyifu) :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَتَحْسَبُونَهُ هَيِّنًا وَهُوَ عِندَ اللَّـهِ عَظِيمٌ ﴿١٥ "Na mnalidhania ni jambo jepesi; na hali hili mbele ya Allah ni adhimu (kubwa mno)". [An-Nur 24: 15] ﴾إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ ﴿١٤ "Hakika Rabi wako bila shaka Yu tayari Awavizia." [Al-Fajr 89: 14]
Play Video
Play Video
01:01:48
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير 🔴LIVE Aayah 183-184 Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 06, 1448 H Jumatano Agosti 19, 2026 Tafsiri/Tarjama ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة SEHEMU YA PILI Amri ya Kufunga الأَمْرُ بِالصَّوْمِ ﴾يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣ "Enyi mlioamini! Mmefaridhishwa Siyamu kama ilivyofaridhishwa kwa wale walio kabla yenu mpate kuwa na taqwa." [Al Baqarah 2:183] أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ ۚ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ ۚ ﴾وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ ۖ فَمَن تَطَوَّعَ خَيْرًا فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ ۚ وَأَن تَصُومُوا خَيْرٌ لَّكُمْ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿١٨٤ "(Siyamu yenyewe ni) Siku za kuhesabika, basi atakaekuwa mgonjwa miongoni mwenu, au yuko safarini, basi (itampasa kulipa) idadi sawa katika masiku mengineyo; na kwa wale wanaoiweza lakini kwa mashaka na kutaabika watoe fidia kulisha masikini; na atakayefanya wema kwa hiari yake, basi hivyo ni bora kwake; na mkifunga ni bora kwenu mkiwa mnaelewa." [Al Baqarah 2:184].
Play Video
Play Video
01:03:19
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴 LIVE باب كراهية تمني الموت بسبب ضرر نزل به
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 05, 1448 H Jumanne Agosti 18, 2026 SEHEMU YA PILI باب كراهية تمني الموت بسبب ضرر نزل به ولا بأس به لخوف الفتنة في الدين Mlango wa Karaha ya Kutamani Mauti Kwa Sababu ya Dhara Iliyomkumba na Haina Tatizo Ikiwa Anahofia Fitna Katika Dini SEHEMU YA KWANZA باب الورع وترك الشبهات Mlango wa Kujichunga na Kuacha Mambo Yenye Shaka (vidanganyifu) :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَتَحْسَبُونَهُ هَيِّنًا وَهُوَ عِندَ اللَّـهِ عَظِيمٌ ﴿١٥ "Na mnalidhania ni jambo jepesi; na hali hili mbele ya Allah ni adhimu (kubwa mno)". [An-Nur 24: 15] ﴾إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ ﴿١٤ "Hakika Rabi wako bila shaka Yu tayari Awavizia." [Al-Fajr 89: 14]
Play Video
Play Video
59:29
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير 🔴LIVE Aayah 183-184 Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 05, 1448 H Jumanne Agosti 18, 2026 Tafsiri/Tarjama ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة SEHEMU YA KWANZA Amri ya Kufunga الأَمْرُ بِالصَّوْمِ ﴾يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣ "Enyi mlioamini! Mmefaridhishwa Siyamu kama ilivyofaridhishwa kwa wale walio kabla yenu mpate kuwa na taqwa." [Al Baqarah 2:183] أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ ۚ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ ۚ ﴾وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ ۖ فَمَن تَطَوَّعَ خَيْرًا فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ ۚ وَأَن تَصُومُوا خَيْرٌ لَّكُمْ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿١٨٤ "(Siyamu yenyewe ni) Siku za kuhesabika, basi atakaekuwa mgonjwa miongoni mwenu, au yuko safarini, basi (itampasa kulipa) idadi sawa katika masiku mengineyo; na kwa wale wanaoiweza lakini kwa mashaka na kutaabika watoe fidia kulisha masikini; na atakayefanya wema kwa hiari yake, basi hivyo ni bora kwake; na mkifunga ni bora kwenu mkiwa mnaelewa." [Al Baqarah 2:184].
Play Video
Play Video
01:04:17
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴 LIVE باب استحباب زيارة القبور للرجال وما يقوله الزائر
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 04, 1448 H Jumatatu Agosti 17, 2026 SEHEMU YA PILI باب استحباب زيارة القبور للرجال وما يقوله الزائر Mlango wa Kupendeza Kuzuru Makaburi kwa Wanaume na Anachosema Mwenye Kuzuru SEHEMU YA KWANZA بابُ كراهة تمنّي الموت بسبب ضُرّ نزل بِهِ وَلاَ بأس بِهِ لخوف الفتنة في الدين Mlango wa Karaha ya Kutamani Mauti Kwa Sababu ya Dhara Iliyomkumba na Haina Tatizo Ikiwa Anahofia Fitna Katika Dini
Play Video
Play Video
49:13
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير 🔴LIVE Aayah 180-182 Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 04, 1448 H Jumatatu Agosti 17, 2026 Tafsiri/Tarjama ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة SEHEMU YA NNE الأَمْرُ بِالوَصِيِّةِ لِلْوَالِدَيْنِ وَالْأَقْرَبِينَ، ثُمَّ نَسْخُهَا فِي حَقِّ الوَرَثَةِ Amri ya kutoa wasia kwa wazazi na jamaa wa karibu, kisha ikafutwa kuhusiana na warithi. Wasia kwa namna inayoeleweka kisharia الْوَصِيَّةُ بِالْمَعْرُوفِ Wasia/usia kwa jamaa ambae harithi (yaani: si mrithi). الوَصِيَّةُ لِقَرِيبٍ لاَ يََرِثُ Fadhila za uadilifu katika Wasia/Usia فَضْلُ العَدْلِ فِي الوَصِيَّةِ ﴾كُتِبَ عَلَيْكُمْ إِذَا حَضَرَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ إِن تَرَكَ خَيْرًا الْوَصِيَّةُ لِلْوَالِدَيْنِ وَالْأَقْرَبِينَ بِالْمَعْرُوفِ ۖ حَقًّا عَلَى الْمُتَّقِينَ ﴿١٨٠ "Mmeandikiwa sharia kuwa anapofikiwa mmoja wenu na mauti kama ameacha mali, kufanya wasia kwa wazazi wawili, na jamaa wa karibu kwa namna inayoeleweka katika sharia; (haya) ni haki -wajibu- kwa wenye taqwa." [Al Baqarah 2:180] ﴾فَمَن بَدَّلَهُ بَعْدَ مَا سَمِعَهُ فَإِنَّمَا إِثْمُهُ عَلَى الَّذِينَ يُبَدِّلُونَهُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ ﴿١٨١ "Atakaeubadilisha (wasia) baada ya kuusikia, basi hakika dhambi yake ni juu ya wale watakaoubadilisha; hakika Allah ni Mwenye Kusikia yote, Alimu wa yote." [Al Baqarah 2:181] ﴾فَمَنْ خَافَ مِن مُّوصٍ جَنَفًا أَوْ إِثْمًا فَأَصْلَحَ بَيْنَهُمْ فَلَا إِثْمَ عَلَيْهِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿١٨٢ "Na mwenye kumhofia muusiaji kwamba kaenda kombo bila kukusudia, au kakusudia dhambi kisha akasuluhisha baina yao, basi hana dhambi juu yake; hakika Allah ni Ghafurur Rahimu." [Al Baqarah 2:182]
Play Video
Play Video
01:07:35
DARSA: التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُهُ🔴DARSA: Kushikamana na Sunnah (VI) Abu Arqam
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 03, 1448 H Jumapili Agosti 16, 2026 SEHEMU YA SITA التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُ Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ na Athari Zake Sunnah ni shaqiqi -ndugu wa kwa baba na mama mmoja/mwenza- wa Qur aani katika kuwa hoja, hivyo basi ni wajibu kwetu kuifuata Sunnah kama ilivyo wajibu kwetu kuifuata Qur aani. Sunnah ni kila kilichothibiti kutokana na Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ kuanzia kauli yake, au kitendo chake , au kulikubaliNabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ jambo ambalo limefanywa mbele yake na yeye hakulikataza iliyopokelewa kwa usahihi kutoka kwa Mtume صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ. Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ni wajibu juu ya kila Muislamu kama vile ilivyo wajibu kwake kushikamana na Qur aani sawa kwa sawa. Hata hivyo, kwa yeyote yule anaeitumia Qur aani kama ni ushahidi wa mtazamo au hukumu fulani basi huwa anahitaji kuzingatia jambo moja pekee, walakini yule ambae anaitumia Sunnah kama ndio ushahidi wake basi huwa anahitaji kuzingatia mambo mawili. Mtu anapotoa Qur aani kama ndio ushahidi, huwa anapaswa kuangalia maana ya Aayah husika na jinsi inavyoashiria hukumu anayotafutia uthibitisho. Bila shaka yoyote ile, watu hutofautiana sana katika suala hili, kulingana na viwango vyao vya elimu na uelewa/ufahamu wao. Ama kwa yule mwenye kutohowa dalili kutoka katika Sunnah, huwa anahitaji kuangalia mambo mawili: Jambo la Kwanza: Uhalisi wa Hadithi husika, kwani kuna mapokezi mengi dhaifu na ya kubuni ambayo yameingia katika Sunnah. Hivyo, ni lazima kuihakiki Hadithi kabla ya kuitumia kama hoja. Kwa sababu hii, wanavyuoni رَحْمَهُمُ اللهُ waliandika vitabu kuhusu wapokezi wa Hadithi na istilahi zake na sanad zake, kwa lengo la kubainisha mapokezi sahihi na yale yasiyo sahihi. Jambo la Pili: Kama ilivyo katika suala la kutumia Qur aani kama hoja, yule anaetumia Sunnah kama hoja huwa anapaswa kuangalia maana inayoelekezwa na Hadithi husika na namna inavyoweza kutumika kuthibitisha hukumu husika; na watu hutofautiana sana katika jambo hili. Allah Akimhutubia Rasuli Wake صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ Amesema: ﴾وَأَنزَلَ اللَّـهُ عَلَيْكَ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَعَلَّمَكَ مَا لَمْ تَكُن تَعْلَمُ ۚ ... ﴿١١٣ "Na Allah Amekuteremshia Kitabu (Qur aani) na Hikmah (Sunnah) na Akakufunza yale ambayo hukuwa unayajua .." [An Nisaa 4:113]
Contact
bottom of page