top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
55:42
DARSA: التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُهُ🔴DARSA: Kushikamana na Sunnah (II) Abu Arqam
Darsa ilifanyika Swafar 25, 1448 H Jumamosi Agosti 08, 2026 SEHEMU YA PILI التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُ Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ na Athari Zake Sunnah ni shaqiqi -ndugu wa kwa baba na mama mmoja/mwenza- wa Qur aani katika kuwa hoja, hivyo basi ni wajibu kwetu kuifuata Sunnah kama ilivyo wajibu kwetu kuifuata Qur aani. Sunnah ni kila kilichothibiti kutokana na Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ kuanzia kauli yake, au kitendo chake , au kulikubaliNabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ jambo ambalo limefanywa mbele yake na yeye hakulikataza iliyopokelewa kwa usahihi kutoka kwa Mtume صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ. Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ni wajibu juu ya kila Muislamu kama vile ilivyo wajibu kwake kushikamana na Qur aani sawa kwa sawa. Hata hivyo, kwa yeyote yule anaeitumia Qur aani kama ni ushahidi wa mtazamo au hukumu fulani basi huwa anahitaji kuzingatia jambo moja pekee, walakini yule ambae anaitumia Sunnah kama ndio ushahidi wake basi huwa anahitaji kuzingatia mambo mawili. Mtu anapotoa Qur aani kama ndio ushahidi, huwa anapaswa kuangalia maana ya Aayah husika na jinsi inavyoashiria hukumu anayotafutia uthibitisho. Bila shaka yoyote ile, watu hutofautiana sana katika suala hili, kulingana na viwango vyao vya elimu na uelewa/ufahamu wao. Ama kwa yule mwenye kutohowa dalili kutoka katika Sunnah, huwa anahitaji kuangalia mambo mawili: Jambo la Kwanza: Uhalisi wa Hadithi husika, kwani kuna mapokezi mengi dhaifu na ya kubuni ambayo yameingia katika Sunnah. Hivyo, ni lazima kuihakiki Hadithi kabla ya kuitumia kama hoja. Kwa sababu hii, wanavyuoni رَحْمَهُمُ اللهُ waliandika vitabu kuhusu wapokezi wa Hadithi na istilahi zake na sanad zake, kwa lengo la kubainisha mapokezi sahihi na yale yasiyo sahihi. Jambo la Pili: Kama ilivyo katika suala la kutumia Qur aani kama hoja, yule anaetumia Sunnah kama hoja huwa anapaswa kuangalia maana inayoelekezwa na Hadithi husika na namna inavyoweza kutumika kuthibitisha hukumu husika; na watu hutofautiana sana katika jambo hili. Allah Akimhutubia Rasuli Wake صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ Amesema: ﴾وَأَنزَلَ اللَّـهُ عَلَيْكَ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَعَلَّمَكَ مَا لَمْ تَكُن تَعْلَمُ ۚ ... ﴿١١٣ "Na Allah Amekuteremshia Kitabu (Qur aani) na Hikmah (Sunnah) na Akakufunza yale ambayo hukuwa unayajua .." [An Nisaa 4:113]
Play Video
Play Video
01:05:06
DARSA:رُوْسٌ وَعِبَرٌمِنْ وُصُولِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ المَدِينةِ 🔴LIVE| DARSA
Darsa ilifanyika Swafar 24, 1448 H Ijumaa Agosti 07, 2026 SEHEMU YA PILI :رُوْسٌ وَعِبَرٌمِنْ وُصُولِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ المَدِينةِ Durusu na Mazingatio kutokana na Kuwasili kwa Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ Madina Tariki -Njia- ya Hijrah -Uhamiaji- na Matukio Yake طريق الهجرة وأحداثها * Kwenda kwenye pango la Thuur لذهاب إلى غار ثور * Ujaji wa Asmaa binti Abu Bakri na chakula قدوم أسماء بنت أبي بكر بالطعام * Kisimamo pamoja na Umm Ma'bad al-Khuzaa'iyyah وقفة مع أمّ معبد الخزاعية * Kisimamo pamoja na Suraaqah bin Malik وقفة مع سراقة بن مالك * Kuwasili kwa Rasuli -صلَّى الله عليه وسلَّم- Qubaa نزول رسول الله -صلَّى الله عليه وسلَّم- في قُباء * Ujenzi wa Masjidi Qubaa بناء مسجد قباء * Rasuli -صلَّى الله عليه وسلَّم- nyumbani kwa Abu Ayyub مبيت رسول الله -عليه الصَّلاة والسَّلام- عند أبي أيوب الأنصاري * Kuwasili Rasuli -صلَّى الله عليه وسلَّم- Madina الوصول رسول الله -صلَّى الله عليه وسلَّم- المدينة المنوَّرة * Mahaba ya Ansari shadidi kwa Rasuli حب الأنصار الشديد للرسول -صلى الله عليه وسلم- * Kuanzisha uhusiano wa udugu kati ya Muhajirina na Ansari.. المؤاخاة بين المهاجرين والأنصار * Ujenzi wa Masjidi wa Nabii -صلَّى الله عليه وسلَّم- Madina بناء مسجد النبي -صلَّى الله عليه وسلَّم- بالمدينة المنوَّرة Matunda ya Hijrah ya Nabii ثمار الهجرة النبوية * Mshikamano wa Kijamii التكافل الاجتماعي * Kusimamisha Dola ya Kiislamu إقامة دولة الإسلام * Kuanzisha iktisadi ya Kiislamu بناء الاقتصاد الإسلامي * Kuunda jeshi تكوين قوة عسكريّة * Watu kuingia katika Dini ya Allah kwa makundi دخول النَّاس في دين الله أفواجاً وثيقة - دستور- المدينة (أو صحيفة المدينة) هي أول وثيقة دستورية في الإسلام Katiba ya Madina (au Hati ya Madina) ndiyo hati ya kwanza ya kikatiba katika Uislamu. Vipengele Muhimu vya Katiba ya Madina أهم مضامين وثيقة المدينة * Kuasisi Umma mmoja تأسيس الأمة * Mamlaka ya Juu المرجعية العليا * Uhuru wa Kuitakidi (kuabudu) حرية العقيدة * Ulinzi wa pamoja الدفاع المشترك
Play Video
Play Video
01:06:23
DARSA: التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُهُ🔴DARSA: Kushikamana na Sunnah (I) Abu Arqam
Darsa ilifanyika Swafar 24, 1448 H Ijumaa Agosti 07, 2026 SEHEMU YA KWANZA التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُ Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ na Athari Zake Sunnah ni shaqiqi -ndugu wa kwa baba na mama mmoja/mwenza- wa Qur aani katika kuwa hoja, hivyo basi ni wajibu kwetu kuifuata Sunnah kama ilivyo wajibu kwetu kuifuata Qur aani. Sunnah ni kila kilichothibiti kutokana na Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ kuanzia kauli yake, au kitendo chake , au kulikubaliNabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ jambo ambalo limefanywa mbele yake na yeye hakulikataza iliyopokelewa kwa usahihi kutoka kwa Mtume صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ. Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ni wajibu juu ya kila Muislamu kama vile ilivyo wajibu kwake kushikamana na Qur aani sawa kwa sawa. Hata hivyo, kwa yeyote yule anaeitumia Qur aani kama ni ushahidi wa mtazamo au hukumu fulani basi huwa anahitaji kuzingatia jambo moja pekee, walakini yule ambae anaitumia Sunnah kama ndio ushahidi wake basi huwa anahitaji kuzingatia mambo mawili. Mtu anapotoa Qur aani kama ndio ushahidi, huwa anapaswa kuangalia maana ya Aayah husika na jinsi inavyoashiria hukumu anayotafutia uthibitisho. Bila shaka yoyote ile, watu hutofautiana sana katika suala hili, kulingana na viwango vyao vya elimu na uelewa/ufahamu wao. Ama kwa yule mwenye kutohowa dalili kutoka katika Sunnah, huwa anahitaji kuangalia mambo mawili: Jambo la Kwanza: Uhalisi wa Hadithi husika, kwani kuna mapokezi mengi dhaifu na ya kubuni ambayo yameingia katika Sunnah. Hivyo, ni lazima kuihakiki Hadithi kabla ya kuitumia kama hoja. Kwa sababu hii, wanavyuoni رَحْمَهُمُ اللهُ waliandika vitabu kuhusu wapokezi wa Hadithi na istilahi zake na sanad zake, kwa lengo la kubainisha mapokezi sahihi na yale yasiyo sahihi. Jambo la Pili: Kama ilivyo katika suala la kutumia Qur aani kama hoja, yule anaetumia Sunnah kama hoja huwa anapaswa kuangalia maana inayoelekezwa na Hadithi husika na namna inavyoweza kutumika kuthibitisha hukumu husika; na watu hutofautiana sana katika jambo hili. Allah Akimhutubia Rasuli Wake صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ Amesema: ﴾وَأَنزَلَ اللَّـهُ عَلَيْكَ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَعَلَّمَكَ مَا لَمْ تَكُن تَعْلَمُ ۚ ... ﴿١١٣ "Na Allah Amekuteremshia Kitabu (Qur aani) na Hikmah (Sunnah) na Akakufunza yale ambayo hukuwa unayajua .." [An Nisaa 4:113]
Play Video
Play Video
01:06:36
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴 LIVE باب : ذكرالموت وقصر الأمل Sh Salim
Darsa ilifanyika Swafar 22, 1448 H Jumatano Agosti 05, 2026 باب ذكر الموت وقصر الأمل Mlango wa Kukumbuka Mauti na Kupunguza Matarajio :قَالَ الله تَعَالَى كُلُّ نَفْسٍ ذَائِقَةُ الْمَوْتِ ۗ وَإِنَّمَا تُوَفَّوْنَ أُجُورَكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ﴾فَمَن زُحْزِحَ عَنِ النَّارِ وَأُدْخِلَ الْجَنَّةَ فَقَدْ فَازَ ۗ وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا مَتَاعُ الْغُرُورِ ﴿١٨٥ "Kila nafsi itaonja mauti, na hakika mtalipwa kikamilifu ujira wenu Siku ya Qiyaamah, basi atakaewekwa mbali na Moto na akaingizwa Jannah kwa yakini amefuzu; na uhai wa dunia si lolote ila ni starehe ya udanganyifu." [Aal-'Imraan 3:185] ﴾وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ مَّاذَا تَكْسِبُ غَدًا ۖ وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ بِأَيِّ أَرْضٍ تَمُوتُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴿٣٤ "Na nafsi yoyote haielewi nini itachuma kesho, na nafsi yoyote haielewi itafia katika ardhi gani" [Luqmaan 31: 34] ﴾فَإِذَا جَاءَ أَجَلُهُمْ لَا يَسْتَأْخِرُونَ سَاعَةً ۖ وَلَا يَسْتَقْدِمُونَ ﴿٣٤ "Basi utakapofika muda wao huo, hawatataahari saa na wala hawatatangulia saa." [Al-A'raaf 7:34] ﴾يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُلْهِكُمْ أَمْوَالُكُمْ وَلَا أَوْلَادُكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْخَاسِرُونَ﴿٩ "Enyi mlioamini! Zisikupurukusheni mali zenu na wala watoto wenu mkaacha kumdhukuru Allah; na yeyote atakaefanya hivyo basi hao ndio waliohasirika." [Al-Munaafiquna 63:9] ﴾وَأَنفِقُوا مِن مَّا رَزَقْنَاكُم مِّن قَبْلِ أَن يَأْتِيَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ فَيَقُولَ رَبِّ لَوْلَا أَخَّرْتَنِي إِلَىٰ أَجَلٍ قَرِيبٍ فَأَصَّدَّقَ وَأَكُن مِّنَ الصَّالِحِينَ﴿١٠ "Na toeni katika yale Tuliyokuruzukuni kabla hayajamfikia mmoja wenu mauti akasema: Rabi wangu! Lau Ungeliniahirisha mpaka muda wa karibu hivi, basi ningetoa Sadaka na ningelikuwa miongoni mwa Swalihina." [Al-Munaafiquna 63:10] ﴾وَلَن يُؤَخِّرَ اللَّـهُ نَفْسًا إِذَا جَاءَ أَجَلُهَا ۚ وَاللَّـهُ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ﴿١١ "(Lakini) Allah Haiahirishi kamwe nafsi yeyote inapokuja ajali yake; na Allah ni Khabiru kwa yale myatendayo." [Al-Munaafiquna 63:11] ﴾حَتَّىٰ إِذَا جَاءَ أَحَدَهُمُ الْمَوْتُ قَالَ رَبِّ ارْجِعُونِ ﴿٩٩ "Mpaka yatakapomfikia mmoja wao mauti, atasema: Rabi wangu! Nirejeshe (duniani)." [Al-Muuminuna 23: 99-115] أَلَمْ يَأْنِ لِلَّذِينَ آمَنُوا أَن تَخْشَعَ قُلُوبُهُمْ لِذِكْرِ اللَّـهِ وَمَا نَزَلَ مِنَ الْحَقِّ وَلَا يَكُونُوا كَالَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلُ فَطَالَ عَلَيْهِمُ الْأَمَدُ فَقَسَتْ ﴾ قُلُوبُهُمْ ۖ وَكَثِيرٌ مِّنْهُمْ فَاسِقُونَ ﴿١٦ "Je, haujafika wakati kwa walioamini kwamba zinyenyekee nyoyo zao kwa kumdhukuru Allah na yale yaliyoteremka ya haki, na wala wasiwe kama wale waliopewa Kitabu kabla, ukawatawilikia muda, kisha zikawa ngumu nyoyo zao? Na wengi miongoni mwao ni mafasiki." [Al-Hadid 57:16].
Play Video
Play Video
01:02:38
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴 LIVE باب فضل الغَنِيّ الشاكر Sh Salim
Darsa ilifanyika Swafar 21, 1448 H Jumanne Agosti 04, 2026 باب فضل الغَنِيّ الشاكر وهو من أخذ المال من وجهه وصرفه في وجوهه المأمور بِهَا Mlango wa Fadhila/Ubora wa Tajiri mwenye kushukuru na ambae kuchuma Mali na njia itakiwayo (Halali) na kuitumia katika njia Iliyoamriwa kwayo :قَالَ الله تَعَالَى ﴾فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَاتَّقَىٰ ﴿٥﴾ وَصَدَّقَ بِالْحُسْنَىٰ ﴿٦﴾ فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْيُسْرَىٰ ﴿٧ "Basi yule anayetoa (mali) na akamcha Allah. Na akasadikisha Al-Husnaa (jazaa na laa ilaha illallah). Basi Tutamuwepesishia kwa yaliyo mepesi." [Al-Layl 92:5-7] ﴾وَسَيُجَنَّبُهَا الْأَتْقَى ﴿١٧﴾ الَّذِي يُؤْتِي مَالَهُ يَتَزَكَّىٰ ﴿١٨﴾ وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُ مِن نِّعْمَةٍ تُجْزَىٰ ﴿١٩﴾ إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ رَبِّهِ الْأَعْلَىٰ ﴿٢٠ ﴾وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ ﴿٢١ "Na ataepushwa nao mwenye taqwa kabisa. Ambaye anatoa mali yake kujitakasa. Na hali hakuna mmoja yeyote aliyemfanyia fadhila yoyote hata amlipe. Isipokuwa kutaka Wajihi wa Rabi wake Aliyetukuka. Na bila shaka atakuja kuridhika." [Al-Layl 92:17-21] ﴾إِن تُبْدُوا الصَّدَقَاتِ فَنِعِمَّا هِيَ ۖ وَإِن تُخْفُوهَا وَتُؤْتُوهَا الْفُقَرَاءَ فَهُوَ خَيْرٌ لَّكُمْ ۚ وَيُكَفِّرُ عَنكُم مِّن سَيِّئَاتِكُمْ ۗ وَاللَّـهُ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ ﴿٢٧١ "Mkidhihirisha Sadaka basi ni vizuri hivyo, na mkizificha na kuwapa mafakiri, basi hilo ni heri kwenu; na Atakufutieni katika maovu yenu; na Allah kwa yale myatendayo, ni Khabir (Mwenye upeo wa habari za dhahiri na za batini.)" [Al-Baqarah 2:271] ﴾لَن تَنَالُوا الْبِرَّ حَتَّىٰ تُنفِقُوا مِمَّا تُحِبُّونَ ۚ وَمَا تُنفِقُوا مِن شَيْءٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٩٢ "Hamtoweza kuufikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda; na kitu chochote mnachotoa basi hakika Allah kwacho ni Alimu (Mjuzi)." [Aal-'Imraan 3:92]
Play Video
Play Video
01:02:52
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴LIVE باب الإيثار والمواساة Sh Salim
Darsa ilifanyika Swafar 20, 1448 H Jumatatu Agosti 03, 2026 Mlango wa Kupendelea wengine na kusaidiana باب الإيثار والمواساة :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَيُؤْثِرُونَ عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ وَلَوْ كَانَ بِهِمْ خَصَاصَةٌ ۚ ﴿٩ "Na wanawapendelea kuliko nafsi zao japokuwa wao wenyewe wanahitaji." [Al-Hashr 59:9] ﴾وَيُطْعِمُونَ الطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِ مِسْكِينًا وَيَتِيمًا وَأَسِيرًا ﴿٨ "Na wanalisha chakula juu ya kukipenda kwao, masikini na mayatima na mateka." [Al-Insan 76:8] باب التنافس في أمور الآخرة والاستكثار مما يتبرك بِهِ Mlango wa Kushindana Katika Mambo Yanayohusu Akhera na Kukithirisha (kutaka) Vitu vya Baraka :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَفِي ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ الْمُتَنَافِسُونَ ﴿٢٦ "Na katika hayo basi washindane wenye kushindana. "[Al-Mutwaffifina 83: 26]
Play Video
Play Video
01:16:12
Mhadhara: أهمية القرآن العظيم في حياة المسلم 🔴 LIVE | Ust Badr S Ja'far kutoka Nairobi, Kenya
Darsa ilifanyika Swafar 18, 1448 H Jumamosi Agosti 01, 2026 أهمية القرآن العظيم في حياة المسلم اليومية Umuhimu wa Qur aani katika Maisha ya Muislamu ya kila Siku :قال تعالى ﴾إِنَّ هَـٰذَا الْقُرْآنَ يَهْدِي لِلَّتِي هِيَ أَقْوَمُ وَيُبَشِّرُ الْمُؤْمِنِينَ الَّذِينَ يَعْمَلُونَ الصَّالِحَاتِ أَنَّ لَهُمْ أَجْرًا كَبِيرًا ﴿٩ "Hakika hii Qur aani inaongoza katika yaliyonyooka kabisa, na inawabashiria Waumini wanaotenda mema kwamba watapata ujira mkubwa." [Al Is-raa 17:9.] Umuhimu wa Qur aani unatokana na yale yaliyokusanyika ndani yake katika kuelekeza na kutoa uongofu/mwongozo katika itikadi sahihi, na mambo ya ibada za hali na kweli, na maadili mema na tabia njema, na miamalati na sharia za kiadilifu na haki, pamoja na mafundisho yake ya kujenga jamii yenye maadili mema na kuimarisha dola imara. Iwapo Waislamu watajadidi imani yao juu ya umuhimu wa Qur aani tukufu katika maisha yao, na wakawa makini katika kushikamana na kufuata bali kutii Amri na Maagizo/maelekezo ya Kiungu yenye hekima yaliyomo ndani ya Qur aani; kwani wanapata kile wanachohitaji kutoka katika maisha ya kiroho yaliyosafi, na nguvu za kisiasa na kijeshi, utajiri na ustaarabu, pamoja na neema na baraka zisizohesabika. :قال تعالى ﴾وَلَوْ أَنَّ أَهْلَ الْقُرَىٰ آمَنُوا وَاتَّقَوْا لَفَتَحْنَا عَلَيْهِم بَرَكَاتٍ مِّنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ وَلَـٰكِن كَذَّبُوا فَأَخَذْنَاهُم بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ ﴿٩٦ "Na lau kama watu wa miji wangeliamimi na (wakashikamana na) taqwa, kwa yakini Tungeliwafungulia baraka nyingi kutoka mbinguni na ardhini, walakini walikadhibisha; basi Tuliwachukua (Tuliwaadhibu/Tuliwaangamiza) kwa sababu ya yale waliyokuwa wakiyachuma." [Al A'raaf 7:96] Ikiwa Waislamu wanataka heri, na kutengamaa na utukufu, na heshima kwa ajili ya nafsi zao wenyewe na kwa ajili ya umma wao, basi ni juu yao kuifuata Qur aani Takatifu katika maisha yao ya kila siku kulingana na mwongozo wa Mtume Muhammad صلّى الله عليه وسلّم na Swahaba zake رضي الله عنهم na kuhakikisha kuwa wanaipa Qur aani nafasi, na hadhi na heshima yake iliyopewa na Allah na Rasuli Wake صلّى الله عليه وسلّم kwa kuyatekeleza na kuyafanyia kazi maamrisho na maagizo yake na kujikataza kwa kujiweka mbali na makatazo yake. لن يصلح آخر هذه الأمة إلا بما صلح به أوّلها Kwani hakuna njia wala uwezekano wa kutengamaa na wala kufanikiwa na kufaulu wa mwisho wa umma huu isipokuwa kwa kilekile kilichopelekea kutengemaa, kufanikiwa na kufaulu wa mwanzo wake.
Play Video
Play Video
01:03:15
Darsa: (VII) الشرك في عبادة الله 🔴 اعْلَمْ أنَّ مِنْ أَعْظَمِ نَوَاقِضِ الإِسْلَامِ
Darsa ilifanyika Swafar 17, 1448 H Ijumaa Julai 31, 2026 SEHEMU YA SABA Utangulizi تَمْهِيد Vitenguzi vya kalimat -neno laTawhidi نَوَاقِضُ لَا إِلَهَ إِلاَّ اللهِ Vitenguzi vya Tawhidi نَوَاقِضُ التَّوْحِيد Vitenguzi vya Uislamu نَوَاقِضُ الِإسْلاَم اعْلَمْ أنَّ مِنْ أَعْظَمِ نَوَاقِضِ الإِسْلَامِ عَشْرَةَ Elewa kwamba katika vitenguzi VIKUBWA kabisa vya Uislamu ni mambo KUMI. Elewa na tambua na uwe na yakini ya kwamba Uislamu wa mtu unatenguka kwa kufanya moja lolote lile miongoni mwa mambo kumi yenye kutengua Uislamu. Vitenguzi vya KUMI Uislamu النواقض الِإسْلاَم العشرة Kitenguzi cha Kwanza: Kumshirikisha Allah katika Ibada الأول: الشرك في عبادة الله
Contact
bottom of page