top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
58:27
Darsa: حُقُوْقُ الزَّوْجَةِ عَلَى زَوْجِهَا 🔴LIVE |DARSA Haki za Mke juu ya Mume (I)Ust. Abu Raifah
Darsa ilifanyika Rabi' Awwal 03, 1448 H Jumapili Agosti 16, 2026 Haki za Mke juu ya Mumewe حُقُوْقُ الزَّوْجَةِ عَلَى زَوْجِهَا Kama ambayo Sharia imewajibisha -imelazimisha- kwa mke kutimiza fungu la haki kwa mumewe, kadhalika Sharia imempa -imemuwekea- mke haki zinazohifadhi Dini yake na hadhi yake. :قال تعالى ﴾وَلَهُنَّ مِثْلُ الَّذِي عَلَيْهِنَّ بِالْمَعْرُوفِ ۚ وَلِلرِّجَالِ عَلَيْهِنَّ دَرَجَةٌ ۗ وَاللَّـهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴿٢٢٨ "Nao wake wana haki kama ambayo (waume zao) iliyo juu yao kwa mujibu wa Sharia; na wanaume wana daraja zaidi juu yao; na Allah ni Mwenye Enzi ya Nguvu Asiyeshindika, Hakimu." [Al Baqarah 2:228] Na Rasuli wa Allah صَليَ اللَّهُ علَيْهِ وَآله وسَلَّم amesema: أَلَّا إِنَّ لَكُمْ عَلَى نِسَائِكُمْ حَقَا،ً وَلِنِسَائِكُمْ عَلَيْكُمْ حَقًا "Tanabahini! Hakika nyinyi mnazo haki juu ya wanawake wenu, na wanawake wenu wanazo haki juu yenu..." tirmidhi, katika Kitabu cha kuhusu Kunyonyesha; mlango wa Yaliyokuja Kuhusu Haki za mwanamke juu ya mumewe; Hadithi namba (1163) Na Rasuli wa Allah صَليَ اللَّهُ علَيْهِ وَآله وسَلَّم ameamuru kwamba haki za wake ziheshimiwe: فَاتَّقُوا اللَّهَ فِي النِّسَاءِ فَإِنَّكُمْ أَخَذْتُمُوهُنَّ بِأَمَانِ اللَّهِ وَاسْتَحْلَلْتُمْ فُرُوجَهُنَّ بِكَلِمَةِ اللَّهِ "...basi muogopeni Allah katika wake zenu! Kwani nyinyi mumewachukuwa kwa dhamana ya Allah, na mkahalalishiwa tupu zao kwa kalima ya Allah ...." Muslim, katika Kitabu cha Hajj; mlango wa Hija ya Nabii صَليَ اللَّهُ علَيْهِ وَآله وسَلَّم . Hadithi namba (1218a) Hivyo basi kwa kadiri mume atakavyotimiza haki za mke wake, maisha yatakuwa ya haki, yenye furaha na kuridhika. Haki za mke juu ya mumewe ni za aina mbili. حقوق الزوجة على الزوج قسمان Ya Kwanza: Haki za kifedha حقوق مالية Ya Pili: Haki zisizo za kifedha حقوق غير مالية
Play Video
Play Video
53:15
Darsa: Mirathi: أَقْسَامُ الوَرَثَةِ بِاعْتِبَارِالإِرْثِ 🔴 LIVE |DARSA الأخُ لأمِّ وَالأُخْتُ لأمّ
Darsa ilifanyika Rabi' Awwal 02, 1448 H Jumamosi Agosti 15, 2026 أَقْسَامُ الوَرَثَةِ بِاعْتِبَارِالإِرْثِ َMakundi (vigawanyo) vya Warithi kwa kuzingatia (namna za) KURITHI KUNDI LA KWANZA Wenye Kurithi kwa FAR-DHU PEKEE من يَرِثُ بِالْفَرْضِ فَقَط Warithi wenye kustahiki kurithi kwa FAR DHU PEKEE ni SABA (7) 1. UMMU أُمٌّ 2. MUME الزَّوْجُ 3. MKE زوْجَةٌ 4. BIBI (NYANYA) KWA MAMA جَدَّةٌ 5. BIBI (NYANYA) KWA BABA جَدَّةٌ 6. AKH KWA MAMA MMOJA الأخُ لأمِّ 7. UKHTI KWA MAMA MMOJA الأُخْت لأمّ Mrithi wa kwanza mwenye kustahiki kurithi kwa FAR DHU PEKEE MAMA/UMMU أُمٌّ UMMU hustahiki kurithi FAR DHU TATU (3) PEKEE: 1. SUDUSI (1/6) السُّدُسُ 2. THELUTHI (1/3) الثُّلُثُ 3. THELUTHI ILIYOBAKI ثلث الباقي UMMU/MAMA HUSTAHIKI KURITHI KWA FAR DHU KATIKA HALI NNE (4): HALI YA KWANZA ﴾وَلِأَبَوَيْهِ لِكُلِّ وَاحِدٍ مِّنْهُمَا السُّدُسُ مِمَّا تَرَكَ إِن كَانَ لَهُ وَلَدٌ ﴿١١ “Na WAZAZI WAKE WAWILI (UMMU/MAMA NI MMOJA WA HAO WAZAZI WAWILI) kila mmoja wao atastahiki SUDUSI (1/6) katika alichoacha (MRITHIEWA) IKIWA (MRITHIWA) ANA WALAD ....” [An Nisaa 4:11] HALI YA PILI : ﴾فَإِن كَانَ لَهُ إِخْوَةٌ فَلِأُمِّهِ السُّدُسُ ۚ ﴿١١ "Na ikiwa (mrithiwa) ana Ikhwah (yaani: ndugu: wa kike au wa kiume) basi UMMU/MAMA wake atastahiki SUDUSI (1/6) ..” [An Nisaa 4:11] HALI YA TATU: ﴾وَوَرِثَهُ أَبَوَاهُ فَلِأُمِّهِ الثُّلُثُ ۚ ﴿١١ “Na (ikiwa) WAZAZI WAKE WAWILI NDIO WARITHI WAKE (MRITHIWA: YAANI HAKUNA MRITHI ISIPOKUWA WAZAZI WAWILI PEKEE), BASI UMMU/MAMA YAKE ATASTAHIKI THELUTHI (1/3)..” [An Nisaa 4:11] HALI YA NNE: مسألة العمريتين MAS-ALA ZENYE KUELEWEKA KWA JINA LA: AL UMARIYYATAYNI AMBAYO YAKO NA HALI MBILI
Play Video
Play Video
58:23
DARSA: التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُهُ🔴DARSA: Kushikamana na Sunnah (V) Abu Arqam
Darsa ilifanyika Rabi' Awwal 02, 1448 H Jumamosi Agosti 15, 2026 SEHEMU YA TANO التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُ Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ na Athari Zake Sunnah ni shaqiqi -ndugu wa kwa baba na mama mmoja/mwenza- wa Qur aani katika kuwa hoja, hivyo basi ni wajibu kwetu kuifuata Sunnah kama ilivyo wajibu kwetu kuifuata Qur aani. Sunnah ni kila kilichothibiti kutokana na Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ kuanzia kauli yake, au kitendo chake , au kulikubaliNabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ jambo ambalo limefanywa mbele yake na yeye hakulikataza iliyopokelewa kwa usahihi kutoka kwa Mtume صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ. Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ni wajibu juu ya kila Muislamu kama vile ilivyo wajibu kwake kushikamana na Qur aani sawa kwa sawa. Hata hivyo, kwa yeyote yule anaeitumia Qur aani kama ni ushahidi wa mtazamo au hukumu fulani basi huwa anahitaji kuzingatia jambo moja pekee, walakini yule ambae anaitumia Sunnah kama ndio ushahidi wake basi huwa anahitaji kuzingatia mambo mawili. Mtu anapotoa Qur aani kama ndio ushahidi, huwa anapaswa kuangalia maana ya Aayah husika na jinsi inavyoashiria hukumu anayotafutia uthibitisho. Bila shaka yoyote ile, watu hutofautiana sana katika suala hili, kulingana na viwango vyao vya elimu na uelewa/ufahamu wao. Ama kwa yule mwenye kutohowa dalili kutoka katika Sunnah, huwa anahitaji kuangalia mambo mawili: Jambo la Kwanza: Uhalisi wa Hadithi husika, kwani kuna mapokezi mengi dhaifu na ya kubuni ambayo yameingia katika Sunnah. Hivyo, ni lazima kuihakiki Hadithi kabla ya kuitumia kama hoja. Kwa sababu hii, wanavyuoni رَحْمَهُمُ اللهُ waliandika vitabu kuhusu wapokezi wa Hadithi na istilahi zake na sanad zake, kwa lengo la kubainisha mapokezi sahihi na yale yasiyo sahihi. Jambo la Pili: Kama ilivyo katika suala la kutumia Qur aani kama hoja, yule anaetumia Sunnah kama hoja huwa anapaswa kuangalia maana inayoelekezwa na Hadithi husika na namna inavyoweza kutumika kuthibitisha hukumu husika; na watu hutofautiana sana katika jambo hili. Allah Akimhutubia Rasuli Wake صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ Amesema: ﴾وَأَنزَلَ اللَّـهُ عَلَيْكَ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَعَلَّمَكَ مَا لَمْ تَكُن تَعْلَمُ ۚ ... ﴿١١٣ "Na Allah Amekuteremshia Kitabu (Qur aani) na Hikmah (Sunnah) na Akakufunza yale ambayo hukuwa unayajua .." [An Nisaa 4:113]
Play Video
Play Video
01:02:15
Darsa: (VIII) الشرك في عبادة الله 🔴 اعْلَمْ أنَّ مِنْ أَعْظَمِ نَوَاقِضِ الإِسْلَامِ عَشْرَةَ
Darsa ilifanyika Rabi' Awwal 01, 1448 H Ijumaa Agosti 14, 2026 SEHEMU YA NANE Vitenguzi vya kalimat -neno laTawhidi نَوَاقِضُ لَا إِلَهَ إِلاَّ اللهِ Vitenguzi vya Tawhidi نَوَاقِضُ التَّوْحِيد Vitenguzi vya Uislamu نَوَاقِضُ الِإسْلاَم اعْلَمْ أنَّ مِنْ أَعْظَمِ نَوَاقِضِ الإِسْلَامِ عَشْرَةَ Elewa kwamba katika vitenguzi VIKUBWA kabisa vya Uislamu ni mambo KUMI. Elewa na tambua na uwe na yakini ya kwamba Uislamu wa mtu unatenguka kwa kufanya moja lolote lile miongoni mwa mambo kumi yenye kutengua Uislamu. Vitenguzi vya KUMI Uislamu النواقض الِإسْلاَم العشرة Kitenguzi cha Kwanza: Kumshirikisha Allah katika Ibada ya Allah الأول: الشرك في عبادة الله Allah تَعَالَى Amesema: ﴾إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ ... ﴿٤٨ "Hakika Allah Haghufurii kushirikishwa, lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae..." [An Nisaa 4:47] Allah تَعَالَى Amesema: ﴾ إِنَّهُ مَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللَّـهُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ وَمَأْوَاهُ النَّارُ ۖ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ﴿٧٢ "Hakika mwenye kumshirikisha Allah bila shaka Allah Atamharamishia Jannah, na makazi yake yatakuwa ni Nari (Motoni), na madhalimu hawatopata yeyote yule mwenye kunusuru.” [Al Maaidah 5: 72].
Play Video
Play Video
48:34
DARSA: التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُهُ🔴DARSA: Kushikamana na Sunnah (IV) Abu Arqam
Darsa ilifanyika Rabi' Awwal 01, 1448 H Ijumaa Agosti 14, 2026 SEHEMU YA NNE التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُ Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ na Athari Zake Sunnah ni shaqiqi -ndugu wa kwa baba na mama mmoja/mwenza- wa Qur aani katika kuwa hoja, hivyo basi ni wajibu kwetu kuifuata Sunnah kama ilivyo wajibu kwetu kuifuata Qur aani. Sunnah ni kila kilichothibiti kutokana na Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ kuanzia kauli yake, au kitendo chake , au kulikubaliNabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ jambo ambalo limefanywa mbele yake na yeye hakulikataza iliyopokelewa kwa usahihi kutoka kwa Mtume صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ. Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ni wajibu juu ya kila Muislamu kama vile ilivyo wajibu kwake kushikamana na Qur aani sawa kwa sawa. Hata hivyo, kwa yeyote yule anaeitumia Qur aani kama ni ushahidi wa mtazamo au hukumu fulani basi huwa anahitaji kuzingatia jambo moja pekee, walakini yule ambae anaitumia Sunnah kama ndio ushahidi wake basi huwa anahitaji kuzingatia mambo mawili. Mtu anapotoa Qur aani kama ndio ushahidi, huwa anapaswa kuangalia maana ya Aayah husika na jinsi inavyoashiria hukumu anayotafutia uthibitisho. Bila shaka yoyote ile, watu hutofautiana sana katika suala hili, kulingana na viwango vyao vya elimu na uelewa/ufahamu wao. Ama kwa yule mwenye kutohowa dalili kutoka katika Sunnah, huwa anahitaji kuangalia mambo mawili: Jambo la Kwanza: Uhalisi wa Hadithi husika, kwani kuna mapokezi mengi dhaifu na ya kubuni ambayo yameingia katika Sunnah. Hivyo, ni lazima kuihakiki Hadithi kabla ya kuitumia kama hoja. Kwa sababu hii, wanavyuoni رَحْمَهُمُ اللهُ waliandika vitabu kuhusu wapokezi wa Hadithi na istilahi zake na sanad zake, kwa lengo la kubainisha mapokezi sahihi na yale yasiyo sahihi. Jambo la Pili: Kama ilivyo katika suala la kutumia Qur aani kama hoja, yule anaetumia Sunnah kama hoja huwa anapaswa kuangalia maana inayoelekezwa na Hadithi husika na namna inavyoweza kutumika kuthibitisha hukumu husika; na watu hutofautiana sana katika jambo hili. Allah Akimhutubia Rasuli Wake صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ Amesema: ﴾وَأَنزَلَ اللَّـهُ عَلَيْكَ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَعَلَّمَكَ مَا لَمْ تَكُن تَعْلَمُ ۚ ... ﴿١١٣ "Na Allah Amekuteremshia Kitabu (Qur aani) na Hikmah (Sunnah) na Akakufunza yale ambayo hukuwa unayajua .." [An Nisaa 4:113]
Play Video
Play Video
51:54
Darsa: المنظومة الحائيةِ 🔴LIVE |DARSA (III) َلَيْسَ بِمَوْلُوْدٍ، وَلَيْسَ بِوَالِدٍ Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Rabi' Awwal 01, 1448 H Ijumaa Agosti 14, 2026 SEHEMU YA TATU شرح المنظومة الحائية في عقيدة أَهْلِ السُّنَّةِ وَالجَمَاعَةِ لابن أبي داود لابن أبي داود Sharhu ya shairi (utenzi wa) Haaiyyah kuhusiana na Itikadi/Aqidah ya Ahali wa Sunnah na Jamaa’h وَلَيْسَ بِمَوْلُوْدٍ، وَلَيْسَ بِوَالِدٍ Na wala Hakuzaliwa na wala Hakuzaa وَلَيْسَ لَهُ شِبْهٌ، تَعَالَى المُسَبَّحُ Na wala Hana shabihi yeyote yule, Ametukuka Mwenye Kustahiki Kusabihiwa (Kutukuzwa) Qur aani imegawanyika vigawanyo VITATU القرانُ على ثَلٌاثَةِ أَقْسَامٍ ١- إِمَّا تَوْحِيدٌ، وَهُوَ الإِخْبَارُ عَن اللهِ وَعِبَادَتِهِ، وَالنَّهْيُ عَنِ الشِّرْكِ بِهِ 1- Ima ni Tawhidi, ambayo ni kuhabarisha kuhusu Allah na ibada Yake, na kukataza kumshirikisha Allah. ٢- وَإِمَّا أوَامِرٌ وَنَواهٍ، وَهِيَ الحَلَالُ وَالْحَرَامُ وَالأَحْكَامُ الشَّرْعِيَّةُ 2- Na ima ni Maamrisho na makatazo, ambayo ni halali na haramu, na hukumu za kisharia. ٣- وَإِمَّا إِخْبَارٌعَن الرُّسُلِ وَالأُمَمِ، وَالمَاضِي وَالْمُسْتَقْبَلِ، وَالْجَنَّةِ وَالنَّارِِ 3- Na ima ni kuhabarisha kuhusiana na Rusuli -Wajumbu- na mataifa, na yale yaliyopita na yale ya mustakbali (yajayo), na Jannah na Nari (Moto).
Play Video
Play Video
49:33
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير 🔴LIVE Aayah 180-182 Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Swafar 29, 1448 H Jumatano Agosti 12, 2026 Tafsiri/Tarjama ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة SEHEMU YA TATU الأَمْرُ بِالوَصِيِّةِ لِلْوَالِدَيْنِ وَالْأَقْرَبِينَ، ثُمَّ نَسْخُهَا فِي حَقِّ الوَرَثَةِ Amri ya kutoa wasia kwa wazazi na jamaa wa karibu, kisha ikafutwa kuhusiana na warithi. Wasia kwa namna inayoeleweka kisharia الْوَصِيَّةُ بِالْمَعْرُوفِ Wasia/usia kwa jamaa ambae harithi (yaani: si mrithi). الوَصِيَّةُ لِقَرِيبٍ لاَ يََرِثُ ﴾كُتِبَ عَلَيْكُمْ إِذَا حَضَرَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ إِن تَرَكَ خَيْرًا الْوَصِيَّةُ لِلْوَالِدَيْنِ وَالْأَقْرَبِينَ بِالْمَعْرُوفِ ۖ حَقًّا عَلَى الْمُتَّقِينَ ﴿١٨٠ "Mmeandikiwa sharia kuwa anapofikiwa mmoja wenu na mauti kama ameacha mali, kufanya wasia kwa wazazi wawili, na jamaa wa karibu kwa namna inayoeleweka katika sharia; (haya) ni haki -wajibu- kwa wenye taqwa." [Al Baqarah 2:180] ﴾فَمَن بَدَّلَهُ بَعْدَ مَا سَمِعَهُ فَإِنَّمَا إِثْمُهُ عَلَى الَّذِينَ يُبَدِّلُونَهُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ ﴿١٨١ "Atakaeubadilisha (wasia) baada ya kuusikia, basi hakika dhambi yake ni juu ya wale watakaoubadilisha; hakika Allah ni Mwenye Kusikia yote, Alimu wa yote." [Al Baqarah 2:181] ﴾فَمَنْ خَافَ مِن مُّوصٍ جَنَفًا أَوْ إِثْمًا فَأَصْلَحَ بَيْنَهُمْ فَلَا إِثْمَ عَلَيْهِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿١٨٢ "Na mwenye kumhofia muusiaji kwamba kaenda kombo bila kukusudia, au kakusudia dhambi kisha akasuluhisha baina yao, basi hana dhambi juu yake; hakika Allah ni Ghafurur Rahimu." [Al Baqarah 2:182]
Play Video
Play Video
01:00:18
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴 LIVE (III) باب : ذكرالموت وقصر الأمل Sh Salim
Darsa ilifanyika Swafar 28, 1448 H Jumanne Agosti 11, 2026 SEHEMU YA TATU باب ذكر الموت وقصر الأمل Mlango wa Kukumbuka Mauti na Kupunguza Matarajio :قَالَ الله تَعَالَى كُلُّ نَفْسٍ ذَائِقَةُ الْمَوْتِ ۗ وَإِنَّمَا تُوَفَّوْنَ أُجُورَكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ﴾فَمَن زُحْزِحَ عَنِ النَّارِ وَأُدْخِلَ الْجَنَّةَ فَقَدْ فَازَ ۗ وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا مَتَاعُ الْغُرُورِ ﴿١٨٥ "Kila nafsi itaonja mauti, na hakika mtalipwa kikamilifu ujira wenu Siku ya Qiyaamah, basi atakaewekwa mbali na Moto na akaingizwa Jannah kwa yakini amefuzu; na uhai wa dunia si lolote ila ni starehe ya udanganyifu." [Aal-'Imraan 3:185] ﴾وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ مَّاذَا تَكْسِبُ غَدًا ۖ وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ بِأَيِّ أَرْضٍ تَمُوتُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴿٣٤ "Na nafsi yoyote haielewi nini itachuma kesho, na nafsi yoyote haielewi itafia katika ardhi gani" [Luqmaan 31: 34] ﴾فَإِذَا جَاءَ أَجَلُهُمْ لَا يَسْتَأْخِرُونَ سَاعَةً ۖ وَلَا يَسْتَقْدِمُونَ ﴿٣٤ "Basi utakapofika muda wao huo, hawatataahari saa na wala hawatatangulia saa." [Al-A'raaf 7:34] ﴾يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُلْهِكُمْ أَمْوَالُكُمْ وَلَا أَوْلَادُكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْخَاسِرُونَ﴿٩ "Enyi mlioamini! Zisikupurukusheni mali zenu na wala watoto wenu mkaacha kumdhukuru Allah; na yeyote atakaefanya hivyo basi hao ndio waliohasirika." [Al-Munaafiquna 63:9] ﴾وَأَنفِقُوا مِن مَّا رَزَقْنَاكُم مِّن قَبْلِ أَن يَأْتِيَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ فَيَقُولَ رَبِّ لَوْلَا أَخَّرْتَنِي إِلَىٰ أَجَلٍ قَرِيبٍ فَأَصَّدَّقَ وَأَكُن مِّنَ الصَّالِحِينَ﴿١٠ "Na toeni katika yale Tuliyokuruzukuni kabla hayajamfikia mmoja wenu mauti akasema: Rabi wangu! Lau Ungeliniahirisha mpaka muda wa karibu hivi, basi ningetoa Sadaka na ningelikuwa miongoni mwa Swalihina." [Al-Munaafiquna 63:10] ﴾وَلَن يُؤَخِّرَ اللَّـهُ نَفْسًا إِذَا جَاءَ أَجَلُهَا ۚ وَاللَّـهُ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ﴿١١ "(Lakini) Allah Haiahirishi kamwe nafsi yeyote inapokuja ajali yake; na Allah ni Khabiru kwa yale myatendayo." [Al-Munaafiquna 63:11] ﴾حَتَّىٰ إِذَا جَاءَ أَحَدَهُمُ الْمَوْتُ قَالَ رَبِّ ارْجِعُونِ ﴿٩٩ "Mpaka yatakapomfikia mmoja wao mauti, atasema: Rabi wangu! Nirejeshe (duniani)." [Al-Muuminuna 23: 99-115] أَلَمْ يَأْنِ لِلَّذِينَ آمَنُوا أَن تَخْشَعَ قُلُوبُهُمْ لِذِكْرِ اللَّـهِ وَمَا نَزَلَ مِنَ الْحَقِّ وَلَا يَكُونُوا كَالَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلُ فَطَالَ عَلَيْهِمُ الْأَمَدُ فَقَسَتْ ﴾ قُلُوبُهُمْ ۖ وَكَثِيرٌ مِّنْهُمْ فَاسِقُونَ ﴿١٦ "Je, haujafika wakati kwa walioamini kwamba zinyenyekee nyoyo zao kwa kumdhukuru Allah na yale yaliyoteremka ya haki, na wala wasiwe kama wale waliopewa Kitabu kabla, ukawatawilikia muda, kisha zikawa ngumu nyoyo zao? Na wengi miongoni mwao ni mafasiki." [Al-Hadid 57:16].
Contact
bottom of page