top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
01:00:10
DARSA: التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُهُ🔴DARSA:Kushikamana na Sunnah (XI) Abu Arqam
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 13, 1448 H Jumatano Agosti 26, 2026 SEHEMU YA KUMI NA MOJA التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُ Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ na Athari Zake Athari za kushikamana na Sunnah آثَارُالتَّمَسُّكِ بالسُّنَّةِ Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ kunapatikana athari nyingi; zikiwemo: 🔸Miongoni mwake: أن يعرف الإنسان أنه أتخذ إماماً يقتدى به، وهو رسول الله عليه الصلاة والسلام ، وحينئذ ينشأ في قلبه محبته وإتباعه والتأسي به Kwamba mtu anapaswa kuelewa kwamba amejichukuliwa imamu anaemfuta, naye ni Rasuli wa Allah صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ, na kwa hilo basi yatachipuka -yataibuka- moyoni mwake mahaba -mapenzi kwa kumpenda- Rasuli wa Allah صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ, na kumfuata na kumuiga. 🔸Miongoni mwake: أن الإنسان يرفض البدعه وذلك لأن العبادات كلها لاتتم إلا بإخلاص النية المنافي للشرك وإخلاص الإتباع المنافي للبدعة Kwamba mtu hukataa bidaa kwa sababu (anaelewa yakini kuwa) ibada zote haziwezi kutimia isipokuwa kwa kupatikana nia safi, nia ambayo hupinga ushirikina, na ikhlasi ya kufuata kunapinga na bidaa. 🔸Na miongoni mwake: أن المتمسك بالسنة يكون قدوة ويكون إماماً Kwamba mwenye kushikamana na Sunnah anakuwa mfano wa kuigwa na anakuwa imamu. 🔸Na miongoni mwake: إكتساب الإنسان من أخلاق النبي صلى الله عليه وسلم Mtu kupata akhlaqi za Nabii صلى الله عليه وسلم. 🔸Na miongoni mwake: أن الإنسان يكون وسطاً بين الغالي في دين الله والجافي عنه فإن دين الإسلام دين وسط Kwamba mtu anakuwa wa wastani kati ya wale waliopindukia mipaka katika Dini ya Allah na wale ambao hawaijali, kwani Dini ya Kiislamu ni Dini ya kati na kati (wastani). 🔸Na miongoni mwake: مايدعو إلى الرحمة والعطف واللين والتواضع Kinacholingania kwenye rehema, na huruma, na upole, na unyenyekevu. 🔸Na miongoni mwake: ولْيُعلم أن حقيقة إتباع النبي يتطلب العلم بسنته والعمل بها والدعوة إليها Na inapaswa kueleweka kwamba kumfuata Nabii صلى الله عليه وسلم kikwelikweli kunahitaji elimu -ujuzi- wa Sunnah zake صلى الله عليه وسلم, na kuzitendea -kuzifanyia- kazi, na kuwalingania wengine (kuzifuata). 🔸Na miongoni mwake: وليحذر المؤمن أن يبتدع في دين الله تعالى ،فالتمسك بالسنة يعني كراهة البدعه ومن ذلك مايقال أو يفعل في شهر رجب Muumini anapaswa kuwa muangalifu dhidi ya kuzusha (jambo) katika Dini ya Allah, kwani kushikamana na Sunnah kunamaanisha kuchukia bidaa.
Play Video
Play Video
53:01
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير 🔴LIVE Aayah I85 Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 13, 1448 H Jumatatu Agosti 26, 2026 Tafsiri/Tarjama ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة SEHEMU YA PILI Fadhila za Qur aani فَضْلُ القُرْآنِ Wajibu wa kufunga Shahari -mwezi wa- Ramadhani إِيْجَابُ صَوْمِ شَهْرِ رَمَضَانَ Masuala kuhusiana na kufunga katika safari مَسَائِلُ عَنِ الصَّوْمِ فِي السَّفَرِ Fadhila za Ramadhani na Ushukaji wa Qur aani ndani yake فَضْلُ رَمَضَانَ وَنُزُوْلُ القُرْآنِ فِيهِ شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِي أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَىٰ وَالْفُرْقَانِ ۚ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ ﴾يُرِيدُ اللَّـهُ بِكُمُ الْيُسْرَ وَلَا يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ وَلِتُكْمِلُوا الْعِدَّةَ وَلِتُكَبِّرُوا اللَّـهَ عَلَىٰ مَا هَدَاكُمْ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴿١٨٥ "Shahari -mwezi wa- Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur-aani ili iwe mwongozo kwa watu na hoja bayana za mwongozo na pambanuo (la haki na batili); hivyo basi atakayeshuhudia miongoni mwenu mwezi basi afunge; na yule atakaekuwa mgonjwa au safarini, basi (inampasa kulipa) idadi sawa katika masiku mengineyo; Allah Anakutakieni mepesi na wala Hakutakieni magumu ili mkamilishe idadi na ili mumtukuze Allah kwa kuwa Amekuongozeni, na ili mpate kushukuru." [Al Baqarah 2:185]
Play Video
Play Video
01:05:27
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴LIVE DARSA باب فضل الاختلاط بالناس وحضور جُمَعِهم وجماعاتهم
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 13, 1448 H Jumatano Agosti 26, 2026 باب فضل الاختلاط بالناس وحضور جُمَعِهم وجماعاتهم ومشاهد الخير ، ومجالس الذكر معهم ، وعيادة مريضهم ، وحضور جنائزهم ، ومواساة محتاجهم ، وإرشاد جاهلهم ، وغير ذلك من مصالحهم لمن قدر عَلَى الأمر بالمعروف والنهي عن المنكر ، وقمع نفسه عن الإيذاء وصبر عَلَى الأذى Mlango wa Fadhila za Kutangamana na watu, na kuhudhuria (Sala za) Ijumaa zao (Sala za) Jamaa zao, na kushuhudia heri, na majilisi za Dhikri pamoja nao, na kutembelea wagonjwa wao, na kuhudhuria mazishi yao, na kukidhi haja zao, na kuwaongoza majahili wao na yasiyokuwa hayo katika yenye maslahi yao na kwa mwenye kuweza kuamrisha mema na kukataza munkari na ... na kuvumilia maudhi. اعْلم أنَّ الاختلاط بالنَّاسِ عَلَى الوجهِ الَّذِي ذَكَرْتُهُ هُوَ المختارُ الَّذِي كَانَ عَلَيْهِ رسول الله صلى الله عليه وسلم وسائر الأنبياء صلواتُ اللهِ وسلامه عَلَيْهِمْ ، وكذلك الخُلفاءُ الرَّاشدون ، ومن بعدَهُم مِنَ الصَّحَابَةِ وَالتَّابِعِينَ ، ومن بَعدَهُم من عُلَماءِ المُسلمين وأَخْيَارِهم ، وَهُوَ مَذْهَبُ أكثَرِ التَّابِعينَ وَمَنْ بَعدَهُمْ ، وبه قَالَ الشافعيُّ وأحمدُ وأكثَرُ الفقهاءِc أجمعين. قَالَ اللهُ تَعَالَى: ( وَتَعَاوَنُوا عَلَى البِرِّ وَالتَّقْوَى ) [ المائدة : 20 ] والآيات في معنى مَا ذكرته كثيرة معلومة . Elewa ya kwamba kutangamana na watu kwa njia niliyoitaja ndio yenye kupendeza, ndio njia iliyokuwa ikifuatwa na Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم na Manabii wote na hivyohivyo ndio njia ya Mahalifa waongofu na waliokuja baada yao miongoni mwa Sahaba na Taabi'ina; na pia hiyo ilikuwa ndio sifa ya waliokuja baada yao miongoni mwa wanazuoni wa Waislaamu na wabora wao, na hiyo ndiyo dhehebu la Taabi'ina wengi na wala waliokuja baada yao. Na kwayo ndio amesema imamu Shafi', na Ahmad na Mafakihi wengi. Amesema Allah: ﴾وَتَعَاوَنُوا عَلَى الْبِرِّ وَالتَّقْوَىٰ ۖ وَلَا تَعَاوَنُوا عَلَى الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۖ إِنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ ﴿٢ "Na shirikianeni katika wema na taqwa." [Al-Maaidah 5: 2].
Play Video
Play Video
01:01:21
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴LIVE DARSA باب استحباب العزلة عند فساد الناس والزمان
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 12, 1448 H Jumanne Agosti 25, 2026 استحباب العزلة عند فساد الناس والزمان أو الخَوف من فتنة في الدين أو وقوع في حرام وشبهات ونحوها Mlango wa kupendekeza Kujitenga Wakati wa kufisidika -kuharibika- watu na zama au kuhofia Fitina Katika Dini au Kujiingiza Katika Haramu na Shubuhati (vidanganyifu) :قَالَ الله تَعَالَى ﴾فَفِرُّوا إِلَى اللَّـهِ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ ﴿٥٠ "Basi kimbilieni kwa Allah, hakika mimi kwenu ni muonyaji bayana kutoka Kwake." [Adh-Dhaariyaat 50:51]
Play Video
Play Video
01:00:40
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير 🔴LIVE Aayah I85 Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 12, 1448 H Jumanne Agosti 25, 2026 Tafsiri/Tarjama ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة SEHEMU YA KWANZA Fadhila za Qur aani فَضْلُ القُرْآنِ Wajibu wa kufunga Shahari -mwezi wa- Ramadhani إِيْجَابُ صَوْمِ شَهْرِ رَمَضَانَ Masuala kuhusiana na kufunga katika safari مَسَائِلُ عَنِ الصَّوْمِ فِي السَّفَرِ Fadhila za Ramadhani na Ushukaji wa Qur aani ndani yake فَضْلُ رَمَضَانَ وَنُزُوْلُ القُرْآنِ فِيهِ شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِي أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَىٰ وَالْفُرْقَانِ ۚ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ ﴾يُرِيدُ اللَّـهُ بِكُمُ الْيُسْرَ وَلَا يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ وَلِتُكْمِلُوا الْعِدَّةَ وَلِتُكَبِّرُوا اللَّـهَ عَلَىٰ مَا هَدَاكُمْ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴿١٨٥ "Shahari -mwezi wa- Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur-aani ili iwe mwongozo kwa watu na hoja bayana za mwongozo na pambanuo (la haki na batili); hivyo basi atakayeshuhudia miongoni mwenu mwezi basi afunge; na yule atakaekuwa mgonjwa au safarini, basi (inampasa kulipa) idadi sawa katika masiku mengineyo; Allah Anakutakieni mepesi na wala Hakutakieni magumu ili mkamilishe idadi na ili mumtukuze Allah kwa kuwa Amekuongozeni, na ili mpate kushukuru." [Al Baqarah 2:185]
Play Video
Play Video
55:00
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير 🔴LIVE Aayah 183-184 Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 11, 1448 H Jumatatu Agosti 24, 2026 Tafsiri/Tarjama ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة SEHEMU YA TATU Amri ya Kufunga الأَمْرُ بِالصَّوْمِ ﴾يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣ "Enyi mlioamini! Mmefaridhishwa Siyamu kama ilivyofaridhishwa kwa wale walio kabla yenu mpate kuwa na taqwa." [Al Baqarah 2:183] Fidia ya Saumu kwa wasioweza na wazee sana فِدْيَةُ الصَّيَامِ لِلْعَجَزَةِ وَكِبَيْرِي السِّنِّ أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ ۚ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ ۚ ﴾وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ ۖ فَمَن تَطَوَّعَ خَيْرًا فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ ۚ وَأَن تَصُومُوا خَيْرٌ لَّكُمْ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿١٨٤ "(Siyamu yenyewe ni) Siku za kuhesabika, basi atakaekuwa mgonjwa miongoni mwenu, au yuko safarini, basi (itampasa kulipa) idadi sawa katika masiku mengineyo; na kwa wale wanaoiweza lakini kwa mashaka na kutaabika watoe fidia kulisha masikini; na atakayefanya wema kwa hiari yake, basi hivyo ni bora kwake; na mkifunga ni bora kwenu mkiwa mnaelewa." [Al Baqarah 2:184].
Play Video
Play Video
01:02:53
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴 LIVE DARSA (III) باب الورع وترك الشبهات Sh Salim
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 11, 1448 H Jumatatu Agosti 24, 2026 SEHEMU YA TATU باب الورع وترك الشبهات Mlango wa Kujichunga na Kuacha Mambo Yenye Shaka (vidanganyifu) :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَتَحْسَبُونَهُ هَيِّنًا وَهُوَ عِندَ اللَّـهِ عَظِيمٌ ﴿١٥ "Na mnalidhania ni jambo jepesi; na hali hili mbele ya Allah ni adhimu (kubwa mno)". [An-Nur 24: 15] ﴾إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ ﴿١٤ "Hakika Rabi wako bila shaka Yu tayari Awavizia." [Al-Fajr 89: 14]
Play Video
Play Video
58:27
DARSA: التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُهُ🔴DARSA:Kushikamana na Sunnah (X) Abu Arqam
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 10, 1448 H Jumapili Agosti 23, 2026 SEHEMU YA KUMI التَّمَسُّكُ بِالسُّنَّةِ النَّبَوِيَّةِ وآثارُ Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ na Athari Zake Athari za kushikamana na Sunnah آثَارُالتَّمَسُّكِ بالسُّنَّةِ Kushikamana na Sunnah za Nabii صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ kunapatikana athari nyingi; zikiwemo: 🔸Miongoni mwake: أن يعرف الإنسان أنه أتخذ إماماً يقتدى به، وهو رسول الله عليه الصلاة والسلام ، وحينئذ ينشأ في قلبه محبته وإتباعه والتأسي به Kwamba mtu anapaswa kuelewa kwamba amejichukuliwa imamu anaemfuta, naye ni Rasuli wa Allah صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ, na kwa hilo basi yatachipuka -yataibuka- moyoni mwake mahaba -mapenzi kwa kumpenda- Rasuli wa Allah صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ, na kumfuata na kumuiga. 🔸Miongoni mwake: أن الإنسان يرفض البدعه وذلك لأن العبادات كلها لاتتم إلا بإخلاص النية المنافي للشرك وإخلاص الإتباع المنافي للبدعة Kwamba mtu hukataa bidaa kwa sababu (anaelewa yakini kuwa) ibada zote haziwezi kutimia isipokuwa kwa kupatikana nia safi, nia ambayo hupinga ushirikina, na ikhlasi ya kufuata kunapinga na bidaa. 🔸Na miongoni mwake: أن المتمسك بالسنة يكون قدوة ويكون إماماً Kwamba mwenye kushikamana na Sunnah anakuwa mfano wa kuigwa na anakuwa imamu. 🔸Na miongoni mwake: إكتساب الإنسان من أخلاق النبي صلى الله عليه وسلم Mtu kupata akhlaqi za Nabii صلى الله عليه وسلم. 🔸Na miongoni mwake: أن الإنسان يكون وسطاً بين الغالي في دين الله والجافي عنه فإن دين الإسلام دين وسط Kwamba mtu anakuwa wa wastani kati ya wale waliopindukia mipaka katika Dini ya Allah na wale ambao hawaijali, kwani Dini ya Kiislamu ni Dini ya kati na kati (wastani). 🔸Na miongoni mwake: مايدعو إلى الرحمة والعطف واللين والتواضع Kinacholingania kwenye rehema, na huruma, na upole, na unyenyekevu. 🔸Na miongoni mwake: ولْيُعلم أن حقيقة إتباع النبي يتطلب العلم بسنته والعمل بها والدعوة إليها Na inapaswa kueleweka kwamba kumfuata Nabii صلى الله عليه وسلم kikwelikweli kunahitaji elimu -ujuzi- wa Sunnah zake صلى الله عليه وسلم, na kuzitendea -kuzifanyia- kazi, na kuwalingania wengine (kuzifuata). 🔸Na miongoni mwake: وليحذر المؤمن أن يبتدع في دين الله تعالى ،فالتمسك بالسنة يعني كراهة البدعه ومن ذلك مايقال أو يفعل في شهر رجب Muumini anapaswa kuwa muangalifu dhidi ya kuzusha (jambo) katika Dini ya Allah, kwani kushikamana na Sunnah kunamaanisha kuchukia bidaa.
Contact
bottom of page