top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
01:11:14
Darsa: حق الأولاد على الوالدين 🔴 LIVE | DARSA Haki za Watoto Juu ya Wazazi (I) Ust. Abu Raifah
Darsa ilifanyika Shawwal 24, 1447H Jumapili Aprili 12, 2026 Haki za Watoto Juu ya Wazazi Wawili حق الأولاد على الوالدين
Play Video
Play Video
02:09:15
Tadabburul Qur- aani تَدَبُّرُ القُرْآن 🔴LIVE DARSA دروس من سورة الأنعام وسورة يونس
Darsa ilifanyika Shawwal 24, 1447H Jumapili Aprili 12, 2026 Tadabburul Qur- aani تَدَبُّرُ القُرْآن Kuizingatia Qur aani :نظرتك للحياة بين الشدّة والنعمة Mtazamo wako kuhusu maisha kati ya shida (ugumu) na Neema (urahisi): Durusu kutokana na Surah Al-An'am na Surah Yunus دروس من سورة الأنعام وسورة يونس Aayah Mbili Zinazoweza kukusaidia katika kufikia kubadilisha mtazamo wako -namna unavyoona- baina ya Shida na Neema Katika Maisha. ﴾وَإِن يَمْسَسْكَ اللَّـهُ بِضُرٍّ فَلَا كَاشِفَ لَهُ إِلَّا هُوَ ۖ وَإِن يَمْسَسْكَ بِخَيْرٍ فَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١٧ "Na Allah Akikugusisha kwa dhara, basi hakuna yeyote wa kuiondoa isipokuwa Yeye, na Akikugusisha kheri, basi Yeye juu ya kila kitu ni Qadiru (Muweza)." [Al-An‘am 6:17] ﴾وَإِن يَمْسَسْكَ اللَّـهُ بِضُرٍّ فَلَا كَاشِفَ لَهُ إِلَّا هُوَ ۖ وَإِن يُرِدْكَ بِخَيْرٍ فَلَا رَادَّ لِفَضْلِهِ ۚ يُصِيبُ بِهِ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ ۚ وَهُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ﴿١٠٧ "Na Allah Akikugusisha dhara, basi hakuna wa kuiondosha isipokuwa Yeye; na Akikutakia kheri, basi hakuna wa kurudisha Fadhila Zake; Humfikishia (Fadhila Yake) Amtakaye katika Waja Wake; Naye Ghafurur Rahimu" [Yunus 10:107]
Play Video
Play Video
50:12
Darsa: صحيح البخاري 🔴 LIVE | DARSA (VI) رَاوِي الحَدِيثِ : مالك بن أنس Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Shawwal 23, 1447H Jumamosi Aprili 11, 2026 باب كَيْفَ كَانَ بَدْءُ الْوَحْىِ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم Mlango: Namna ya Wahyi Ulivyoanza kwa Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) HADITHI YA PILI حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ يُوسُفَ، قَالَ أَخْبَرَنَا مَالِكٌ، عَنْ هِشَامِ بْنِ عُرْوَةَ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ عَائِشَةَ أُمِّ الْمُؤْمِنِينَ ـ رضى الله عنها ـ أَنَّ الْحَارِثَ بْنَ هِشَامٍ ـ رضى الله عنه ـ سَأَلَ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ يَا رَسُولَ اللَّهِ كَيْفَ يَأْتِيكَ الْوَحْىُ فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم " أَحْيَانًا يَأْتِينِي مِثْلَ صَلْصَلَةِ الْجَرَسِ ـ وَهُوَ أَشَدُّهُ عَلَىَّ ـ فَيُفْصَمُ عَنِّي وَقَدْ وَعَيْتُ عَنْهُ مَا قَال وَأَحْيَانًا يَتَمَثَّلُ لِيَ الْمَلَكُ رَجُلاً فَيُكَلِّمُنِي فَأَعِي مَا يَقُولُ ". قَالَتْ عَائِشَةُ رضى الله عنها وَلَقَدْ رَأَيْتُهُ يَنْزِلُ عَلَيْهِ الْوَحْىُ فِي الْيَوْمِ الشَّدِيدِ الْبَرْدِ، فَيَفْصِمُ عَنْهُ وَإِنَّ جَبِينَهُ لَيَتَفَصَّدُ عَرَقًا. Ametuhadithia Abdullahi bin Yusuf, amesema: ametupasha habari Malik kutokana na Hishami bin 'Urwah kutokana na baba ake, kutokana na Aishah Mama wa Waumini (رضي الله عنها) kwamba: Al-Harith bin Hisham (رضي الله عنه) alimuuliza Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa kusema: 'Ewe Rasuli wa Allah! Vipi unakujia Wahyi?” Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamjibu kwa kusema: “Wakati mwengine unanijia kama sauti ya kengele, aina hii ya Wahyi ni shadidi -ngumu- zaidi kwangu kuliko zote na kisha hali hiyo hunipitia baada ya kuwa nimeshafahamu kile nilichofunuliwa; wakati mwingine Malaika huja katika umbile la rajuli, hunisemresha na kuyaelewa anayosema.” Aaishah (رضي الله عنها) amesema: 'Kwa hakika nilimwona (Rasuli wa Allah صلى الله عليه وآله وسلم) akiletewa Wahyi siku ya baridi kali na akaona jasho likimdondoka usoni (baada ya kumalizika Wahyi). Wapokezi wa Hadithi hii رُوَاةُ هَذَا الحَدِيثِ 1. Abdullahi bin Yusuf (Rahimahullahu) عَبْدُ اللَّهِ بْنُ يُوسُفَ 2. Malik bin Anas bin Malik (Rahimahullahu) مالك بن أنس بن مالك 3. Hishami bin 'Urwah (Rahimahullahu) هِشَامِ بْنِ عُرْوَةَ 4. 'Urwah bin Az Zubair (Rahimahullahu) عُرْوَةَ بنِ الزُّبَيْرِ بنِ العَوَّامِ 5. Aishah Ummul Muminina (Allah Awe Radhi Nae) عَائِشَةَ أُمِّ الْمُؤْمِنِينَ ـ رضى الله عنها Msimulizi wa Hadithi: Malik bin Anas bin Malik مالك بن أنس بن مالك : الاسم مالك بن أنس بن مالك (مالك بن أنس بن مالك بن أبي عامر بن عمرو بن الحارث بن غيمان بن خثيل بن عمرو بن الحارث) الكنية: أبو عبد الله النسب: الأصبحي، الحميري، المدني، التيمي، اليمني بلد الإقامة: المدينة علاقات الراوي: حليف عثمان بن عبيد الله القرشي، وكاتبه عيسى بن كنانة وأمه العالية بنت شريك بن عبد الرحمن بن شريك الأزدية، وأخوه النضر، وعمه أبو سهيل نافع بن مالك تاريخ الميلاد: 92 هـ، أو 93، أو 94 هـ، أو 95 هـ تاريخ الوفاة: 178 هـ، أو 179 هـ بلد الميلاد: ذي المروة بلد الوفاة: المدينة بلد الرحلة: مكة، مصر طبقة رواة التقريب: السابعة الرتبة عند ابن حجر: الفقيه، إمام دار الهجرة، رأس المتقنين، وكبير المتثبتين الرتبة عند الذهبي: الإمام
Play Video
Play Video
42:08
Mimbari ya Wazi مَاذَا بَعْدَ رَمَضَانَ 🔴 | MIMBARI: (II) Jitahmini: Nini Baada ya Ramadhani?
Darsa ilifanyika Shawwal 22, 1447H Ijumaa Aprili 10, 2026 Nini baada ya Ramadhani? مَاذَا بَعْدَ رَمَضَانَ Shahari ya Ramadhani imekwishatuaga, Shahari yenye kheri nyingi; michana yake ilikuwa ni subira ya Saumu, na nyakati za usiku wake zilikuwa ni nyakati za Qiyamul (kusimamo cha usiku). Shahari ya Qur-aani imetuaga, Shahari ya tak-wa, na Jihaad, na maghufira, Shahari ya kuomba dua kwa wingi, Shahari ya kutolewa Nari na kutunukiwa Jannah. Amefaulu aliyetimiza funga yake, na kisimamo chake na kisimamo cha Usiku wa Qadri kwa imani na kutarajia malipo Kwa bahati mbaya amehasirika yule aliyejinyima kuchangamkia fursa zilizokuwemo ndani ya Shahari ya Ramadhani kwa kutoweza kufikia kuelewa umuhimu wake na wala fadhila zake. Gharadhi kuu ya Shahari ilikuwa kutufikisha kwenye Taq-wa; kwa Kauli Yake Allah: ﴾يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣ "Enyi mlioamini! Mmefaridhishwa Siyamu kama ilivyofaradhishwa kwa wale ambao wa kabla yenu mpate kuwa na Taq-wa" [Baqarah 2:183]. Muislamu aliyejaaliwa kuingia katika Shahari ya Ramadhani na kutoka alitarajiwa aelewe kuwa aliingia katika madrasa ya Taq-wa. Na mwenye kuingia katika madrasa yoyote ile, hutarajiwa kutoka humo huku akiwa amepata manufaa au shahada ya lile somo alilolisoma, na baada ya hapo huitumia ile elimu aliyoisoma kumsaidia katika kuendesha maisha yake; pia huendelea kuitumia hiyo elimu katika maisha yake yote hadi kifo kumfikie. Anasema Allaah Subhanahu wa Ta’alaa: وَاعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّى يَأْتِيَكَ الْيَقِينُ "Na muabudu Rabi wako mpaka ikufikie yakini (mauti)" [Al-Hijr 16: 99]. Kuthibitika -kuendelea- katika ibada baada ya Shahari ya Ramadhani ni moja kati ya alama au sababu zenye kuonyesha kutakabaliwa kwa amali zilizikuwemo kwenye Shahari ya Ramadhani. Ni vyema tuwe tunajiuliza maswali kama haya: 1. Je, Umekufikia mchana mmoja ukiwa katika kufunga za Sunnah? 2. Je, Umekufikia usiku mmoja ukiwa katika kisimamo? 3. Je, Unaendelea kusoma Qur-aani kama ulivyokuwa ukisoma katika Ramadhani? 4. Je, Unaendelea kumdhukuru Allah kwa wingi kama ulivyokuwa ukimdhukuru katika Ramadhani? 5. Je, unaendelea kububujika machozi kwa kukumbuka dhambi zake na kuhofia adhabu za Allah kama ulivyokuwa kwenye Shahari ya Ramadhani? Je, tunaelewa kwamba Allah Anapenda zaidi amali zenye kuendeleza -zenye kudumu- japokuwa ni kalili -chache- kuliko amali nyingi zisizodumu?! قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((أَحَبَّ الْأَعْمَالِ إِلَى اللَّهِ أَدْوَمُهَا وَإِنْ قَلَّ)) متفق عليه Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم amesema kuwa: " Amali zinazopendeza zaidi mbele ya Allah ni zile zenye kudumu -zenye kuendelea-japokuwa ni kalili" [Wamewafikiana Bukhari na Muslim] Basi tujaribu kwa Tawfiki Yake Allah kuthibiti katika Shahari nyenginezo kwa amali ambazo tulikuwa tukizitekeleza kwenye Shahari ya Ramadhani ikiwemo kufunga Saumu za Sunnah: i-Siku Sita za Shawwal ستة أيام من شوال Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: "من صام رمضان ثم أتبعه ستاً من شوال، كان كصيام الدهر" "Yeyote yule ataliyefunga Shahari ya Ramadhani, kisha akafuatia (Siku) Sita za Shawwal atapata ujira wa aliyefunga dahari -mwaka mzima-". ii-Siku za Jumatatu na Alhamisi صيام أيام الاثنين والخميس Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: " تُعْرَضُ الْأَعْمَالُ يَوْمَ الِاثْنَيْنِ وَالْخَمِيسِ فَأُحِبُّ أَنْ يُعْرَضَ عَمَلِي وَأَنَا صَائِمٌ " "Amali huwekwa mbele ya Allah kila Siku ya Jumatatu na Alhamisi, basi napenda amali yangu iwekwe mbele ya Allah nikiwa nimefunga" iii-Siku tatu katika kila Shahari الأيام البيض: الثالث عشر، والرابع عشر، والخامس عشر من كل شهر هجري Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: "يَا أَبَا ذَرٍّ، إِذَا صُمْتَ مِنَ الشَّهْرِ ثَلاثَةَ أَيَّامٍ فَصُمْ ثَلاثَةَ عَشَرَ وَأَرْبَعَةَ عَشَرَ وَخَمْسَةَ" "Ewe Abu Dharr! Endapo utafunga Siku tatu za katika Shahari, basi funga Siku ya 13, ya 14, na ya 15" iv-Siku ya Arafah صيام يوم عرفة (9 ذي الحجة): لغير الحاج Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: " يكفِّرُ السَّنَةَ المَاضِيةَ وَالبَاقِيَةَ" "Inafuta dhambi za mwaka uliopita na mwaka uliopo" v-Siku ya Ashuraa na Tasu'aa صيام يوم عاشوراء (10 محرم): ويستحب صيام يوم قبله (تاسوعاء) أو بعده Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: "صِيَامُ يَوم عاشوراء إنِّي أحْتَسبُ علَى اللهِ أن يُكفِّرَ السَّنةَ التِي قبلَه" "Saumu ya siku ya Ashuraa, nategemea kutoka kwa Allah Ayafute madhambi ya mwaka uliotangulia." vi- Kufunga Shahari ya Muharram " صيام شهر محرم: "أَفْضَلُ الصِّيَامِ بَعْدَ رَمَضَانَ شَهْرُ اللَّهِ الْمُحَرَّمُ
Play Video
Play Video
51:24
MHADHARA: تربية الاولاد في الإسلام 🔴 Malezi ya Watoto katika Uislamu Ust Ali Masoud Abu Arqam
Darsa ilifanyika Shawwal 22, 1447H Ijumaa Aprili 10, 2026 Malezi ya Watoto katika Uislamu تربية الاولاد في الإسلام Malezi ya Kiislamu si kujifunza kwa kukariri tu, bali ni juhudi jabari zinazo takiwa kuandaliwa kutokana na mafundisho yaliyokuja kwenye Qur aani na kuwepo utekelezaja wake sahihi kupitia Sunnah za Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم kwa gharadhi ya kuweza kukifikisha kizazi kinachochipuka kuwa ni chenye kushikamana na Qur-aani na Sunnah katika kushikamana na Dini yake hususan na katika maisha yake kwa ujumla. Umuhimu wa malezi ya Kiislamu أهمية التربية الإسلامية Umuhimu wa malezi ya Kiislamu upo katika kujenga shakh-siyah ya Kiislamu yenye uwiano na jumuishi (kiakili, kiroho, kimaadili, na kimwili) wenye kulingana na kwenda sambamba na manhaji a Qur-aani na Sunnah sahihi za Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم, ili kuweza kufikia kumpwekesha Allah kwa kuhakiki utumwa Kwake Pekee. Vipengele Muhimu vya Umuhimu wa Malezi ya Kiislamu: 1. Kupandikiza Itikadi sahihi: Kupandikiza Tawhidi; Mahaba -kumpenda Allah na Rasuli Wake صلى الله عليه وسلم. 2.Utakaso wa Maadili: Kukuza na kuimarisha sifa njema : Ikhlasi, uaminifu, ukweli), kwa kuzingatia Sharia za Kiislamu. 3. Utambulisho: Kuimarisha utambulisho wa Kiislamu. 4. Kuhakiki lengo/kusudio la kuumba.
Play Video
Play Video
01:07:04
Darsa: المنظومة الحائيةِ 🔴LIVE | (I) وَلاَ تَكُ فِي القُرْآنِ بِالوَقْفِ قَائِلاً Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Shawwal 22, 1447H Ijumaa Aprili 10, 2026 شرح المنظومة الحائية في عقيدة أَهْلِ السُّنَّةِ وَالجَمَاعَةِ لابن أبي داود لابن أبي داود Sharhu ya shairi (utenzi wa) Haaiyyah kuhusiana na Itikadi/Aqidah ya Ahali wa Sunnah na Jamaa’h وَلاَ تَكُ فِي القُرْآنِ بِالوَقْفِ قَائِلاً * كَمَا قَالَ أَتْبَاعٌ لِجَهْمٍ وَأَسْجَحُوا Na wala usiwe kuhusiana na (suala zima la) Qur-aani mwenye kusema kwa kusitasita- (geugeu: kwa kutokuwa na msimamo), kama walivyosema wafuasi wa Jahm na wakafurahia kauli hii, wakaikubali/wakairidhia na wakaichukua/wakaitakidi (wakaifanya kuwa ndio itikadi yao), na kwa hiari yao wakawa wanaitetea/wanailingania na kusema waziwazi bila kuwa na kigugumizi –usemaji wa kusitasita- kuwa:Qur aani ni mahuluku.
Play Video
Play Video
01:03:55
Darsa: سنن ابن ماجه 🔴 LIVE | DARSA (II) رَاوِي الحَدِيثِ : أبو معاوية الضرير Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Shawwal 21, 1447H Alhamisi Aprili 09, 2026 HADITHI YA TATU Sunan Ibn Maajah سنن ابن ماجه Kitabu cha Utangulizi كتاب المقدمة باب اتِّبَاعِ سُنَّةِ رَسُولِ اللَّهِ ـ صلى الله عليه وسلم ـ Mlango wa kufuata Sunnah za Rasuli wa Allah ـ صلى الله عليه وسلم ـ حَدَّثَنَا أَبُو بَكْرِ بْنُ أَبِي شَيْبَةَ، حَدَّثَنَا أَبُو مُعَاوِيَةَ، وَوَكِيعٌ، عَنِ الأَعْمَشِ، عَنْ أَبِي صَالِحٍ، عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ ـ صلى الله عليه وسلم ـ " مَنْ أَطَاعَنِي فَقَدْ أَطَاعَ اللَّهَ وَمَنْ عَصَانِي فَقَدْ عَصَى اللَّهَ " . Abu Hurayrah (رضي الله عنه) amesimulia kuwa Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Atakayenitii basi atakuwa amemtii Allah, na atakayeniasi atakuwa amemuasi Allah.” Wapokezi wa Hadithi hii رُوَاةُ هَذَا الحَدِيثِ 1.Abu Bakr bin Abu Shaybah (Rahimahullahu) أَبُو بَكْرِ بْنُ أَبِي شَيْبَةَ 2. Abu Mu'awayah (Rahimahullahu) أَبُو مُعَاوِيَةَ 3. Waki'u (Rahimahullahu) وَكِيعٌ 4. Al A'mash (Rahimahullahu) الأَعْمَشِ 5. Abu Saleh (Rahimahullahu) أَبُوصَالِحٍ 6. Abu Hurayrah (Allah Awe Radhi Nae) أَبُو هُرَيْرَةَ رضي الله عنه Msimulizi wa Hadithi: Abu Mu'awayah (Rahimahullahu) أَبُو مُعَاوِيَةَ الاسم: محمد بن خازم اللقب: الضرير، فافاه، الحافظ الكنية: أبو معاوية النسب: التميمي السعدي مولاهم، الضرير، الكوفي، الحافظ علاقات الراوي: مولى بني سعد بن زيد مناة بن تميم، ابنه إبراهيم المذهب العقدي: رمي بالإرجاء تاريخ الميلاد: 113 ه تاريخ الوفاة: 194 هـ، أو 195هـ بلد الرحلة: بغداد طبقة رواة التقريب: كبار التاسعة الرتبة عند ابن حجر: ثقة، أحفظ الناس لحديث الأعمش، وقد يهم في حديث غيره الرتبة عند الذهبي: ثبت في الأعمش وكان مرجئا
Play Video
Play Video
59:11
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير 🔴 LIVE Aayah 148 -150 Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Shawwal 21, 1447H Alhamisi Aprili 09, 2026 Tafsiri ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة Kila Ummah una Qiblah لِكُلِّ أُمَّةٍ قِبْلَةٌ Kwa nini utajo wa kufutwa Qiblah umekaririwa mara tatu? لِمَاذَا تَكَرَّرَ ذِكْرُ نَسْخِ القِبلةِ ثَلاَثَ مَرَّاتٍ ﴾وَلِكُلٍّ وِجْهَةٌ هُوَ مُوَلِّيهَا ۖ فَاسْتَبِقُوا الْخَيْرَاتِ ۚ أَيْنَ مَا تَكُونُوا يَأْتِ بِكُمُ اللَّـهُ جَمِيعًا ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١٤٨ "Na kila mmoja ana upande wa kuuelekea; basi shindaneni (katika) mambo ya kheri; popote mtakapokuwa Allah Atakuleteni pamoja jamia (Siku ya Qiyaamah); hakika Allah juu ya kila kitu ni Qadiru (Muweza)." [Al Baqarah 2:147] ﴾وَمِنْ حَيْثُ خَرَجْتَ فَوَلِّ وَجْهَكَ شَطْرَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ ۖ وَإِنَّهُ لَلْحَقُّ مِن رَّبِّكَ ۗ وَمَا اللَّـهُ بِغَافِلٍ عَمَّا تَعْمَلُونَ ﴿١٤٩ "Na popote utokako (ili kuswali), basi elekeza uso wako upande wa Masjidil-Haraam; na hiyo ni haki kutoka kwa Rabi wako; na Allah si Mwenye Kughafilika na yale myatendayo." [Al Baqarah 2:149] وَمِنْ حَيْثُ خَرَجْتَ فَوَلِّ وَجْهَكَ شَطْرَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ ۚ وَحَيْثُ مَا كُنتُمْ فَوَلُّوا وُجُوهَكُمْ شَطْرَهُ لِئَلَّا يَكُونَ لِلنَّاسِ عَلَيْكُمْ حُجَّةٌ إِلَّا الَّذِينَ ﴾ظَلَمُوا مِنْهُمْ فَلَا تَخْشَوْهُمْ وَاخْشَوْنِي وَلِأُتِمَّ نِعْمَتِي عَلَيْكُمْ وَلَعَلَّكُمْ تَهْتَدُونَ ﴿١٥٠ "Na popote utokako (ili kuswali), elekeza uso wako upande wa Masjidil-Haraam, na popote mtakapokuwa, elekezeni nyuso zenu upande wake, ili watu wasiwe na hoja juu yenu isipokuwa wale waliodhulumu miongoni mwao; basi msiwaogope bali Niogopeni Mimi, na ili Nitimize Neema Yangu juu yenu na ili mpate kuhidika." [Al Baqarah 2:150]
Contact
bottom of page