top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
01:03:40
Darsa: صحيح مسلم 🔴LIVE | DARSA (IV) رَاوِي الحَدِيثِ : حَمَّادُ بْنُ زَيْدٍ Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Dhul Qa'dah 02, 1447H Jumapili Aprili 19, 2026 Kitabu cha Imani كتاب الإيمان باب بيان الإيمان والإسلام والإحسان ووجوب الإيمان بإثبات قدر الله سبحانه وتعالى وبيان الدليل على التبري ممن لا يؤمن بالقدر وإغلاظ القول في حقه SANAD YA PILI YA HADITHI YA Jibril عليه السلام Wapokezi wa Hadithi hii رُوَاةُ هَذَا الحَدِيثِ Hadithi ina wapokezi wafuatao: 1. Muḥammad bin Ubayd al-Ghubari (Rahimahullahu) مُحَمَّدُ بْنُ عُبَيْدٍ الْغُبَرِيُّ 2. Abu Kamil al-Jaḥdari (Rahimahullahu) أَبُو كَامِلٍ الْجَحْدَرِيُّ 3. Aḥmad bin Abdah (Rahimahullahu) أَحْمَدُ بْنُ عَبْدَةَ 4. Ḥammad bin Zayd (Rahimahullahu) حَمَّادُ بْنُ زَيْدٍ 5. Maṭwar al-Warraq (Rahimahullahu) مَطَرٍ الْوَرَّاقِ 6. Abdullah bin Buraydah (Rahimahullahu) عَبْدِ اللَّهِ بْنِ بُرَيْدَةَ 7. Yaḥya bin Yaʿmar (Rahimahullahu) يَحْيَى بْنِ يَعْمَرَ Msimulizi wa Hadithi: Ḥammad bin Zayd (Rahimahullahu) حماد بن زيد بن درهم لاسم: حماد بن زيد بن درهم اللقب: الأزرق الكنية: أبو إسماعيل النسب: الأزدي، الجهضمي، البصري، الأزرق بلد الإقامة: البصرة علاقات الراوي: مولى آل جرير بن حازم الجهضمي، كان جده درهم من سبي سجستان، أخو سعيد بن زيد المذهب العقدي وقال عبيد الله بن يوسف الحبيري، عن فطر بن حماد بن واقد: سألت حماد بن زيد قلت: يا أبا إسماعيل إمام لنا يقول: القرآن مخلوق، أصلي خلفه ؟ قال: لا، ولا كرامة وقال أبو بكر بن أبي الدنيا، عن خالد بن خداش: سمعت حماد بن زيد يقول لئن قلت: إن عليا أفضل من عثمان، لقد قلت: إن أصحاب رسول الله صلى الله عليه وسلم قد خانوا تاريخ الميلاد: 98 هـ، أو زمن سليمان بن عبد الملك، أو زمن عمر بن عبد العزيز تاريخ الوفاة: 177 هـ، وقيل 179 هـ طبقة رواة التقريب: من كبار الثامنة الرتبة عند ابن حجر: ثقة ثبت، فقيه الرتبة عند الذهبي أحد الأعلام أضر، وكان يحفظ حديثه كالماء، قال ابن مهدي: ما رأيت أحدا لم يكتب أحفظ منه وما رأيت بالبصرة أفقه منه، ولم أر أعلم بالسنة منه
Play Video
Play Video
01:54:03
Darsa نَفْسِي بَعْدَ شَوَّال 🔴 DARSA: (II) Ust. Hassan
Darsa ilifanyika Dhul Qa'dah 02, 1447H Jumapili Aprili 19, 2026 SEHEMU YA PILI
Play Video
Play Video
16:51
Darsa نَفْسِي بَعْدَ شَوَّال 🔴 DARSA: (I) Ust. Hassan
Darsa ilifanyika Dhul Qa'dah 02, 1447H Jumapili Aprili 19, 2026 SEHEMU YA KWANZA
Play Video
Play Video
02:19:48
MHADHARA: تربية الاولاد في الإسلام 🔴 Malezi ya Watoto katika Uislamu (II) Ust Ali Masoud Abu Arqam
Darsa ilifanyika Dhul Qa'dah 02, 1447H Jumapili Aprili 19, 2026 SEHEMU YA PILI
Play Video
Play Video
01:06:16
Darsa: حق الأولاد على الوالدين 🔴 LIVE | DARSA Haki za Watoto Juu ya Wazazi (II) Ust. Abu Raifah
Darsa ilifanyika Dhul Qa'dah 02, 1447H Jumapili Aprili 19, 2026 SEHEMU YA PILI Haki za Watoto Juu ya Wazazi Wawili حق الأولاد على الوالدين Kwa hakika Allah سبحانه Atamuuliza mzazi kuhusu waladi wake Siku ya Qiyamah, kabla ya kumuuliza walad kuhusu baba ake, kwani kama vile baba alivyo na haki juu ya waladi wake, basi pia walad naye ana haki juu ya baba yake; kama Alivyosema Allah تعالى: ﴾وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حُسْنًا ۖ وَإِن جَاهَدَاكَ لِتُشْرِكَ بِي مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ فَلَا تُطِعْهُمَا ۚ إِلَيَّ مَرْجِعُكُمْ فَأُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿٨ "Na Tumemuusia Insani -binadamu- kuwafanyia wema wazazi wake wawili; lakini wakikushikilia kuwa unishirikishe na ambayo huna ilimu nayo, basi usiwatii; Kwangu ni marejeo yenu, Nitakujulisheni yale mliyokuwa mkiyatenda." [Al Ankabut 29:8] Pia Amesema Allah تعالى: يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا قُوا أَنفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ نَارًا وَقُودُهَا النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ ﴾عَلَيْهَا مَلَائِكَةٌ غِلَاظٌ شِدَادٌ لَّا يَعْصُونَ اللَّـهَ مَا أَمَرَهُمْ وَيَفْعَلُونَ مَا يُؤْمَرُونَ﴿٦ "Enyi mlioamini! Jikingeni nafsi zenu pamoja na ahli zenu na Moto ambao kuni zake ni watu na mawe; wanaulinda Malaika washupavu wasio na huruma, shadidi, hawamuasi Allah kwa yale Anayowaamrisha na wanafanya yale wanayoamrishwa." [At Tah-rim 66:6] Basi usia/wasia wa Allah kwa wazazi kuhusu waladi wao umetangulia na wasia wa waladi kwa baba zao, hivyo basi yeyote yule atayepuuza na kuzemnbea kumfundisha waladi wake kile kitakachoweza kumnufaisha na kumwacha ajiamulie mwenyewe, huyo atakuwa amefanya kosa kubwa. Na kwa hakika kufisidika kwa watoto wengi huja kwa kule wazazi wao kupuuza na kushindwa kuwafundisha mambo ya lazima ya Dini yao na Sunnah zake. Waliwapuuza katika utotoni mwao, kwa hivyo hawakuwa na manufaa kwa wazazi wao katika uzee wao. Utangulizi unaohusiana na haki za walad مقدمات متعلقة بحق الولد .الولد أمانة سيسأل عنها الوالدان يوم القيامة Walad ni amana ambayo wazazi watawajibika kwayo Siku ya Qiyaamah :عَنْ عَبْدِ اللَّهِ ـ رضى الله عنه ـ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ "الرَّجُلُ رَاعٍ عَلَى أَهْلِ بَيْتِهِ وَهْوَ مَسْئُولٌ عَنْهُمْ، وَالْمَرْأَةُ رَاعِيَةٌ عَلَى بَيْتِ بَعْلِهَا وَوَلَدِهِ وَهْىَ مَسْئُولَةٌ عَنْهُمْ... ". Amesema Rasuli a Allah صلى الله عليه وسلم: "Rajuli -mume- ni mchungaji wa ahali wake -familia yake-, naye ataulizwa juu ya anaowachunga; na mwanamke -mke- ni mchungaji wa nyumba ya mumewe, naye (pia) ataulizwa juu ya anachokichunga.” [Wamewafikiana Bukhari na Muslim]. Usia/wasia kwa wazazi kuhusu watoto wao unatangulia usia wa watoto kuhusu wazazi wao. مسؤولية تربية الأبناء ورعايتهم تقع على الوالدين في المقام الأول Jukumu la kulea na kuwatunza watoto huwa liko juu ya wazazi hasa. الوالدان أشد الناس تأثيراً فيما يكون عليه الأولاد في المستقبل Wazazi ndio watu wenye ushawishi mkubwa katika kuutengeneza na kuuelekeza mustakabali wa watoto wao. :عَنِ أَبِي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه ـ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم " مَا مِنْ مَوْلُودٍ إِلاَّ يُولَدُ عَلَى الْفِطْرَةِ، فَأَبَوَاهُ يُهَوِّدَانِهِ أَوْ يُنَصِّرَانِهِ أَوْ يُمَجِّسَانِهِ " Amesimulia Abu Hurayrah (رضي الله عنه) kuwa: Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Hakuna kizazi kinachozaliwa (mtoto mchanga) isipokuwa anazaliwa katika 'fitwrah' kisha wazazi wake (humbadilisha na) humuingiza katika Uyahudi, au Unasara au Umajusi..." [Wamewafikiana Bukhari na Muslim] Haki za watoto juu ya wazazi wao ni za aina mbili حقوق الأولاد على الآباء قسمان Haki Ya Kwanza: Kabla ya Kuzaliwa الأول: قبل وجود الولد Haki Ya Pili: Baada ya Kuzaliwa الثاني: بعد وجود الولد Haki Ya Pili: Baada ya Kuzaliwa الثاني: بعد وجود الولد *Kuomba dua kutengenea kwa walad دعاء الله بصلاح الولد * Kumpa -kumwita- walad jina zuri تسمية الولد باسم حسن *Kumhurumia na kuwa na upole katika muamala nae رحمته والرفق به في التعامل *Kulinda heshima yake na kuepuka kumtusi, kumuumbua, na kumpiga الحفاظ على كرامته وتجنب سبه وتعنيفه وضربه *Kuchunga haki yake ya kucheza na kucheza naye kwa njia itayomfaidisha na wala haitomuudhi مراعاة حقه في اللعب واللعب معه بما يفيده ولا يؤذيه *Kuwa na pupa juu ya kumfunza walad na kumuadabisha الحرص على تعليم الولد وتأديبه *Kuwa na pupa -hamu- yakumfunza itikadi sahihi الحرص على تعليمه العقيدة السليمة *Kuwa na pupa ya kumfundisha Qur-aani utoto mwake الحرص على تعليمه القرآن في صغره *Kuwa na pupa ya kumfunza Faraadh za Dini, Halali na Haramu utotoni mwake
Play Video
Play Video
01:00:44
Darsa: صحيح البخاري 🔴 LIVE | DARSA (VII) رَاوِي الحَدِيثِ : مالك بن أنس Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Dhul Qa'dah 01, 1447H Jumamosi Aprili 18, 2026 باب كَيْفَ كَانَ بَدْءُ الْوَحْىِ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم Mlango: Namna ya Wahyi Ulivyoanza kwa Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) HADITHI YA PILI حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ يُوسُفَ، قَالَ أَخْبَرَنَا مَالِكٌ، عَنْ هِشَامِ بْنِ عُرْوَةَ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ عَائِشَةَ أُمِّ الْمُؤْمِنِينَ ـ رضى الله عنها ـ أَنَّ الْحَارِثَ بْنَ هِشَامٍ ـ رضى الله عنه ـ سَأَلَ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ يَا رَسُولَ اللَّهِ كَيْفَ يَأْتِيكَ الْوَحْىُ فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم " أَحْيَانًا يَأْتِينِي مِثْلَ صَلْصَلَةِ الْجَرَسِ ـ وَهُوَ أَشَدُّهُ عَلَىَّ ـ فَيُفْصَمُ عَنِّي وَقَدْ وَعَيْتُ عَنْهُ مَا قَال وَأَحْيَانًا يَتَمَثَّلُ لِيَ الْمَلَكُ رَجُلاً فَيُكَلِّمُنِي فَأَعِي مَا يَقُولُ ". قَالَتْ عَائِشَةُ رضى الله عنها وَلَقَدْ رَأَيْتُهُ يَنْزِلُ عَلَيْهِ الْوَحْىُ فِي الْيَوْمِ الشَّدِيدِ الْبَرْدِ، فَيَفْصِمُ عَنْهُ وَإِنَّ جَبِينَهُ لَيَتَفَصَّدُ عَرَقًا. Ametuhadithia Abdullahi bin Yusuf, amesema: ametupasha habari Malik kutokana na Hishami bin 'Urwah kutokana na baba ake, kutokana na Aishah Mama wa Waumini (رضي الله عنها) kwamba: Al-Harith bin Hisham (رضي الله عنه) alimuuliza Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa kusema: 'Ewe Rasuli wa Allah! Vipi unakujia Wahyi?” Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamjibu kwa kusema: “Wakati mwengine unanijia kama sauti ya kengele, aina hii ya Wahyi ni shadidi -ngumu- zaidi kwangu kuliko zote na kisha hali hiyo hunipitia baada ya kuwa nimeshafahamu kile nilichofunuliwa; wakati mwingine Malaika huja katika umbile la rajuli, hunisemresha na kuyaelewa anayosema.” Aaishah (رضي الله عنها) amesema: 'Kwa hakika nilimwona (Rasuli wa Allah صلى الله عليه وآله وسلم) akiletewa Wahyi siku ya baridi kali na akaona jasho likimdondoka usoni (baada ya kumalizika Wahyi). Wapokezi wa Hadithi hii رُوَاةُ هَذَا الحَدِيثِ 1. Abdullahi bin Yusuf (Rahimahullahu) عَبْدُ اللَّهِ بْنُ يُوسُفَ 2. Malik bin Anas bin Malik (Rahimahullahu) مالك بن أنس بن مالك 3. Hishami bin 'Urwah (Rahimahullahu) هِشَامِ بْنِ عُرْوَةَ 4. 'Urwah bin Az Zubair (Rahimahullahu) عُرْوَةَ بنِ الزُّبَيْرِ بنِ العَوَّامِ 5. Aishah Ummul Muminina (Allah Awe Radhi Nae) عَائِشَةَ أُمِّ الْمُؤْمِنِينَ ـ رضى الله عنها Msimulizi wa Hadithi: Malik bin Anas bin Malik مالك بن أنس بن مالك : الاسم مالك بن أنس بن مالك (مالك بن أنس بن مالك بن أبي عامر بن عمرو بن الحارث بن غيمان بن خثيل بن عمرو بن الحارث) الكنية: أبو عبد الله النسب: الأصبحي، الحميري، المدني، التيمي، اليمني بلد الإقامة: المدينة علاقات الراوي: حليف عثمان بن عبيد الله القرشي، وكاتبه عيسى بن كنانة وأمه العالية بنت شريك بن عبد الرحمن بن شريك الأزدية، وأخوه النضر، وعمه أبو سهيل نافع بن مالك تاريخ الميلاد: 92 هـ، أو 93، أو 94 هـ، أو 95 هـ تاريخ الوفاة: 178 هـ، أو 179 هـ بلد الميلاد: ذي المروة بلد الوفاة: المدينة بلد الرحلة: مكة، مصر طبقة رواة التقريب: السابعة الرتبة عند ابن حجر: الفقيه، إمام دار الهجرة، رأس المتقنين، وكبير المتثبتين الرتبة عند الذهبي: الإمام
Play Video
Play Video
44:15
Mhadhara: مُكَفِّرَاتُ الذُّنُوبِ وَالْخَطَايَا 🔴 LIVE |Mhadhara Ust. Ahmed Haydar Kutokea Zanzibar
Darsa ilifanyika Dhul Qa'dah 01, 1447H Jumamosi Aprili 18, 2026 Vifuta Dhambi na Makosa مُكَفِّرَاتُ الذُّنُوبِ وَالْخَطَايَا مكفرات الذنوب هي الأعمال الصالحة والعبادات التي تمحو السيئات وتستر الخطايا Yenye Kufuta Dhambi na Makosa ni: Amali njema na ibada ambazo kwayo zinazofuta maovu na kusitiri makosa. Nukta muhimu: Ni vyema ielemeke kuwa DHAMBI inayofutwa na vifuta dhambi ni dhambi ndogo الصغائر ; dhambi kubwa الكبائر (kama vile ushirikina, mauaji, na uzinzi na kadhalika) huwa zinahitaji Toba. ﴾وَالَّذِينَ لَا يَدْعُونَ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ وَلَا يَقْتُلُونَ النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّـهُ إِلَّا بِالْحَقِّ وَلَا يَزْنُونَ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ يَلْقَ أَثَامًا ﴿٦٨ "Na wale ambao hawaombi pamoja na Allah muabudiwa mwengine yoyote yule na wala hawaui nafsi ambayo Allah Ameiharamisha isipokuwa kwa haki, na wala hawazini; na atakayefanya hivyo atakutana na adhabu." ﴾يُضَاعَفْ لَهُ الْعَذَابُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَيَخْلُدْ فِيهِ مُهَانًا ﴿٦٩ "Ataongezewa adhabu maradufu Siku ya Qiyaamah, na atadumu humo akidhalilishwa." ﴾إِلَّا مَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ عَمَلًا صَالِحًا فَأُولَـٰئِكَ يُبَدِّلُ اللَّـهُ سَيِّئَاتِهِمْ حَسَنَاتٍ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٧٠ "Isipokuwa yule aliyetubu na akaamini na akatenda amali njema; basi hao Allah Atawabadilishia maovu yao kuwa mema; na Allah daima ni Ghafuru Rahimu" Hivyo basi kifuta dhambi cha juu kabisa ni Toba ya kweli وأعظمها التوبة النصوح Vifuta dhambi na makosa vilivyomashuhuri katika Uislamu أبرز مكفرات الذنوب والخطايا في الإسلام التوبة والاستغفار: التوبة الصادقة تمحو ما قبلها، والاستغفار يرفع الدرجات ويمحو السيئات * Toba *Kuleta Is-tigh-fari *Kutekeleza Sala tano za kila siku, na Sala ya Ijumaa hadi Ijumaa nyengine, na Ramadhani hadi Ramadhani nyengine. * Amali njema ﴾إِنَّ الْحَسَنَاتِ يُذْهِبْنَ السَّيِّئَاتِ ۚ ذَٰلِكَ ذِكْرَىٰ لِلذَّاكِرِينَ ﴿١١٤ "Na simamisha Sala katika ncha mbili za mchana na sehemu ya kwanza ya usiku, hakika Hasanati -mema- yanaondosha sayyiaati -maovu-, haya ni ukumbusho kwa wanaokumbuka." [Huud 10:114] *Kutia Udhu إسباغ الوضوء على المكاره عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم إِذَا تَوَضَّأَ الْعَبْدُ الْمُسْلِمُ أَوِ الْمُؤْمِنُ فَغَسَلَ وَجْهَهُ خَرَجَتْ مِنْ وَجْهِهِ كُلُّ خَطِيئَةٍ نَظَرَ إِلَيْهَا بِعَيْنَيْهِ مَعَ الْمَاءِ أَوْ مَعَ آخِرِ قَطْرِ الْمَاءِ أَوْ نَحْوِ هَذَا وَإِذَا غَسَلَ يَدَيْهِ خَرَجَتْ مِنْ يَدَيْهِ كُلُّ خَطِيئَةٍ بَطَشَتْهَا يَدَاهُ مَعَ الْمَاءِ أَوْ مَعَ آخِرِ قَطْرِ الْمَاءِ حَتَّى يَخْرُجَ نَقِيًّا مِنَ الذُّنُوبِ .” Amesimulia Abu Hurayrahh (رضي الله عنه) kuwa Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ”Atapotawadha mja Muislam au Muumini, akaosha uso wake, basi hutoka kwenye uso wake kila dhambi aliyoyapata kwa kuangalia, pamoja na maji ama pamoja na tone la mwisho la maji au mfano wake, na akiosha mikono yake miwili, basi yatatoka mikononi mwake kila dhambi aliyoyapata kwa mikono yake pamoja na maji au pamoja na tone la mwisho la maji, mpaka anatoka akiwa safi kutokana na dhambi.” * Kusubiri Sala baada ya Sala. انتظار الصلاة بعد الصلاة *Kukithirisha hatua kwenda Masjid كثرة الخطا إلى المساجد عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ " أَلاَ أَدُلُّكُمْ عَلَى مَا يَمْحُو اللَّهُ بِهِ الْخَطَايَا وَيَرْفَعُ بِهِ الدَّرَجَاتِ " . قَالُوا بَلَى يَا رَسُولَ اللَّهِ . قَالَ " إِسْبَاغُ الْوُضُوءِ عَلَى الْمَكَارِهِ وَكَثْرَةُ الْخُطَا إِلَى الْمَسَاجِدِ وَانْتِظَارُ الصَّلاَةِ بَعْدَ الصَّلاَةِ فَذَلِكُمُ الرِّبَاطُ " . Amesimulia Abu Hurayrah (رضي الله عنه) kuwa Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Hivi nisiwajulishe juu ya lile ambalo Allah Hufuta makosa -dhambi- kwalo, na Hunyanyua daraja?” Wakasema: “Naam tujulishe ewe Rasuli wa Allah! Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Kukamilisha utiaji wa Udhu nyakati za kuchukiza, kukithirisha hatua za kwenda Masjidi, kungojea Sala baada ya Sala, hiyo kwenu ndio Ribaatw (Jambo bora la kushikamana nalo).” *Majaribu na dhiki: magonjwa, wasiwasi, huzuni, na hata mwiba unaomchoma mwamini *Kuleta Dhikr na Tasbihi ذكر الله والتسبيح *Kutoa Sadaka
Play Video
Play Video
01:00:42
Mimbari ya Wazi مَاذَا بَعْدَ رَمَضَانَ 🔴 | MIMBARI: (III) Jitahmini: Nini Baada ya Ramadhani?
Darsa ilifanyika Shawwal 29, 1447H Ijumaa Aprili 17, 2026 Nini baada ya Ramadhani? مَاذَا بَعْدَ رَمَضَانَ Shahari ya Ramadhani imekwishatuaga, Shahari yenye kheri nyingi; michana yake ilikuwa ni subira ya Saumu, na nyakati za usiku wake zilikuwa ni nyakati za Qiyamul (kusimamo cha usiku). Shahari ya Qur-aani imetuaga, Shahari ya tak-wa, na Jihaad, na maghufira, Shahari ya kuomba dua kwa wingi, Shahari ya kutolewa Nari na kutunukiwa Jannah. Amefaulu aliyetimiza funga yake, na kisimamo chake na kisimamo cha Usiku wa Qadri kwa imani na kutarajia malipo Kwa bahati mbaya amehasirika yule aliyejinyima kuchangamkia fursa zilizokuwemo ndani ya Shahari ya Ramadhani kwa kutoweza kufikia kuelewa umuhimu wake na wala fadhila zake. Gharadhi kuu ya Shahari ilikuwa kutufikisha kwenye Taq-wa; kwa Kauli Yake Allah: ﴾يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣ "Enyi mlioamini! Mmefaridhishwa Siyamu kama ilivyofaradhishwa kwa wale ambao wa kabla yenu mpate kuwa na Taq-wa" [Baqarah 2:183]. Muislamu aliyejaaliwa kuingia katika Shahari ya Ramadhani na kutoka alitarajiwa aelewe kuwa aliingia katika madrasa ya Taq-wa. Na mwenye kuingia katika madrasa yoyote ile, hutarajiwa kutoka humo huku akiwa amepata manufaa au shahada ya lile somo alilolisoma, na baada ya hapo huitumia ile elimu aliyoisoma kumsaidia katika kuendesha maisha yake; pia huendelea kuitumia hiyo elimu katika maisha yake yote hadi kifo kumfikie. Anasema Allaah Subhanahu wa Ta’alaa: وَاعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّى يَأْتِيَكَ الْيَقِينُ "Na muabudu Rabi wako mpaka ikufikie yakini (mauti)" [Al-Hijr 16: 99]. Kuthibitika -kuendelea- katika ibada baada ya Shahari ya Ramadhani ni moja kati ya alama au sababu zenye kuonyesha kutakabaliwa kwa amali zilizikuwemo kwenye Shahari ya Ramadhani. Ni vyema tuwe tunajiuliza maswali kama haya: 1. Je, Umekufikia mchana mmoja ukiwa katika kufunga za Sunnah? 2. Je, Umekufikia usiku mmoja ukiwa katika kisimamo? 3. Je, Unaendelea kusoma Qur-aani kama ulivyokuwa ukisoma katika Ramadhani? 4. Je, Unaendelea kumdhukuru Allah kwa wingi kama ulivyokuwa ukimdhukuru katika Ramadhani? 5. Je, unaendelea kububujika machozi kwa kukumbuka dhambi zake na kuhofia adhabu za Allah kama ulivyokuwa kwenye Shahari ya Ramadhani? Je, tunaelewa kwamba Allah Anapenda zaidi amali zenye kuendeleza -zenye kudumu- japokuwa ni kalili -chache- kuliko amali nyingi zisizodumu?! قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((أَحَبَّ الْأَعْمَالِ إِلَى اللَّهِ أَدْوَمُهَا وَإِنْ قَلَّ)) متفق عليه Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم amesema kuwa: " Amali zinazopendeza zaidi mbele ya Allah ni zile zenye kudumu -zenye kuendelea-japokuwa ni kalili" [Wamewafikiana Bukhari na Muslim] Basi tujaribu kwa Tawfiki Yake Allah kuthibiti katika Shahari nyenginezo kwa amali ambazo tulikuwa tukizitekeleza kwenye Shahari ya Ramadhani ikiwemo kufunga Saumu za Sunnah: i-Siku Sita za Shawwal ستة أيام من شوال Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: "من صام رمضان ثم أتبعه ستاً من شوال، كان كصيام الدهر" "Yeyote yule ataliyefunga Shahari ya Ramadhani, kisha akafuatia (Siku) Sita za Shawwal atapata ujira wa aliyefunga dahari -mwaka mzima-". ii-Siku za Jumatatu na Alhamisi صيام أيام الاثنين والخميس Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: " تُعْرَضُ الْأَعْمَالُ يَوْمَ الِاثْنَيْنِ وَالْخَمِيسِ فَأُحِبُّ أَنْ يُعْرَضَ عَمَلِي وَأَنَا صَائِمٌ " "Amali huwekwa mbele ya Allah kila Siku ya Jumatatu na Alhamisi, basi napenda amali yangu iwekwe mbele ya Allah nikiwa nimefunga" iii-Siku tatu katika kila Shahari الأيام البيض: الثالث عشر، والرابع عشر، والخامس عشر من كل شهر هجري Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: "يَا أَبَا ذَرٍّ، إِذَا صُمْتَ مِنَ الشَّهْرِ ثَلاثَةَ أَيَّامٍ فَصُمْ ثَلاثَةَ عَشَرَ وَأَرْبَعَةَ عَشَرَ وَخَمْسَةَ" "Ewe Abu Dharr! Endapo utafunga Siku tatu za katika Shahari, basi funga Siku ya 13, ya 14, na ya 15" iv-Siku ya Arafah صيام يوم عرفة (9 ذي الحجة): لغير الحاج Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: " يكفِّرُ السَّنَةَ المَاضِيةَ وَالبَاقِيَةَ" "Inafuta dhambi za mwaka uliopita na mwaka uliopo" v-Siku ya Ashuraa na Tasu'aa صيام يوم عاشوراء (10 محرم): ويستحب صيام يوم قبله (تاسوعاء) أو بعده Kwa kauli yake Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم: "صِيَامُ يَوم عاشوراء إنِّي أحْتَسبُ علَى اللهِ أن يُكفِّرَ السَّنةَ التِي قبلَه" "Saumu ya siku ya Ashuraa, nategemea kutoka kwa Allah Ayafute madhambi ya mwaka uliotangulia." vi- Kufunga Shahari ya Muharram " صيام شهر محرم: "أَفْضَلُ الصِّيَامِ بَعْدَ رَمَضَانَ شَهْرُ اللَّهِ الْمُحَرَّمُ
Contact
bottom of page